< 2 Nyakati 34 >

1 Yosia alikuwa na miaka minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka thelathini na mmoja.
Jozjasz miał osiem lat, kiedy zaczął królować, i królował trzydzieści jeden lat w Jerozolimie.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana na kuenenda katika njia za Daudi baba yake, hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.
Czynił on to, co prawe w oczach PANA, chodząc drogami swego ojca Dawida, i nie zbaczał [z nich] ani na prawo, ani na lewo.
3 Katika mwaka wa nane wa utawala wake, alipokuwa angali bado mdogo, alianza kumtafuta Mungu wa Daudi baba yake. Katika mwaka wake wa kumi na mbili alianza kusafisha mahali pa juu pa kuabudia miungu pa Yuda na Yerusalemu, akiondoa nguzo za Ashera, sanamu za kuchonga na vinyago vya kusubu.
Bo w ósmym roku swojego królowania, gdy był jeszcze chłopcem, zaczął szukać Boga swego ojca Dawida, a w dwunastym roku zaczął oczyszczać Judę i Jerozolimę z wyżyn, gajów, rzeźbionych i odlewanych posągów.
4 Mbele ya macho yake, wakazibomoa madhabahu za Mabaali, wakazivunja madhabahu za kufukizia uvumba zilizokuwa zimesimama juu yake, wakazivunja nguzo za Ashera, sanamu na vinyago. Hivi alivivunja vipande vipande na kuvisambaza juu ya makaburi ya waliokuwa wamevitolea kafara.
Na jego oczach zburzono ołtarze Baalów i ściął posągi słoneczne umieszczone wysoko nad nimi. Także gaje oraz rzeźbione i odlewane posągi pokruszył i starł, a ich [pył] rozsypał po grobach tych, którzy im składali ofiary.
5 Akachoma mifupa ya makuhani wao juu ya madhabahu zao na kwa njia hiyo akaitakasa Yuda na Yerusalemu.
Kości kapłanów spalił na ich ołtarzach i oczyścił Judę i Jerozolimę.
6 Katika miji ya Manase, Efraimu na Simeoni, hadi Naftali na kwenye magofu yanayoizunguka,
Podobnie czynił w miastach Manassesa, Efraima i Symeona, aż do Neftalego, wszędzie dokoła za pomocą kilofów.
7 akavunja madhabahu na nguzo za Ashera na kuzipondaponda hizo sanamu hadi zikawa unga na kukata vipande vipande madhabahu zote za kufukizia uvumba katika Israeli yote. Kisha akarudi Yerusalemu.
A kiedy zburzył ołtarze i gaje, starł posągi na proch i ściął wszystkie posągi słoneczne w całej ziemi Izraela, wtedy wrócił do Jerozolimy.
8 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yosia, ili kutakasa nchi na Hekalu, akawatuma Shafani, mwana wa Azalia na Maaseya mtawala wa mji, pamoja na Yoa mwana wa Yoahazi, mwandishi ili kukarabati Hekalu la Bwana Mungu wake.
A w osiemnastym roku swego panowania, po oczyszczeniu ziemi i domu [PANA], posłał Szafana, syna Azaliasza, Maasejasza, namiestnika miasta, oraz Joacha, syna Joachaza, kronikarza, aby naprawili dom PANA, jego Boga.
9 Wakamwendea Hilkia kuhani mkuu na kumpa fedha ambazo zilikuwa zimeletwa ndani ya Hekalu la Bwana ambazo Walawi waliokuwa mabawabu walikuwa wamezikusanya kutoka kwa watu wa Manase, Efraimu na mabaki wote wa Israeli kutoka kwa watu wote wa Yuda na Benyamini na wakazi wa Yerusalemu.
Kiedy przybyli do najwyższego kapłana Chilkiasza, oddali pieniądze przyniesione do domu Bożego – które Lewici, stróże bram, zebrali [od] synów Manassesa i Efraima, od całej reszty Izraela i od całej Judy i Beniamina – po czym wrócili do Jerozolimy.
10 Kisha wakazikabidhi hizo fedha kwa watu waliowekwa ili kusimamia kazi ya Hekalu la Bwana. Hawa watu waliwalipa wafanyakazi waliokarabati na kutengeneza Hekalu lipate kurudi katika hali yake.
I oddali [je] w ręce rzemieślników, którzy mieli nadzór nad pracami w domu PANA, a oni je wypłacili robotnikom, którzy pracowali w domu PANA, naprawiając i umacniając dom.
11 Wakawapa pia mafundi seremala na waashi fedha ili kununua mawe yaliyochongwa, mbao kwa ajili ya kufungia na boriti kwa ajili ya majengo ambayo wafalme wa Yuda walikuwa wameyaacha yakawa magofu.
Wypłacili je cieślom i murarzom na zakup kamienia ciosanego i drzewa na wiązania i na podłogi domów, które zniszczyli królowie Judy.
12 Watu wakafanya kazi kwa uaminifu. Waliokuwa wamewekwa juu yao ili kuwaelekeza ni Yahathi na Obadia, Walawi wa uzao wa Merari, Zekaria na Meshulamu, waliotoka kwenye uzao wa Kohathi. Walawi wote waliokuwa na ufundi wa kupiga ala za uimbaji,
Ci mężczyźni wykonywali tę pracę wiernie. Ich przełożonymi [byli]: Jachat i Obadiasz, Lewici, z synów Merariego, oraz Zachariasz i Meszullam, z synów Kehata, aby kierowali pracami, oraz każdy Lewita, który umiał grać na instrumentach muzycznych.
13 wakawa wasimamizi wa vibarua na kuwaongoza wale waliofanya kila aina ya kazi. Baadhi ya Walawi walikuwa waandishi, maafisa na mabawabu.
Postawieni byli też nad tymi, którzy nosili ciężary, i nadzorowali robotników przy każdej pracy, a spośród Lewitów [byli] pisarze, dozorcy i odźwierni.
14 Wakati walikuwa wakizitoa nje fedha zilizokuwa zimetolewa kwenye Hekalu la Bwana, kuhani Hilkia akakipata kile Kitabu cha Sheria ya Bwana kilichokua kimetolewa kwa mkono wa Mose.
A gdy wynoszono pieniądze przyniesione do domu PANA, kapłan Chilkiasz znalazł księgę Prawa PANA, [przekazaną] przez Mojżesza.
15 Hilkia akamwambia Shafani mwandishi, “Nimekipata Kitabu cha Sheria ndani ya Hekalu la Bwana.” Akampa Shafani kile Kitabu.
Wtedy Chilkiasz powiedział do pisarza Szafana: Znalazłem księgę Prawa w domu PANA. I Chilkiasz dał księgę Szafanowi.
16 Kisha Shafani akakipeleka kile Kitabu kwa mfalme na kumwambia, “Maafisa wako wanafanya kila kitu kama walivyokabidhiwa kufanya.
Szafan zaniósł księgę królowi i zdał mu sprawę, mówiąc: Twoi słudzy wykonują wszystko, co im poleciłeś;
17 Wamelipa fedha zilizokuwa katika Hekalu la Bwana na wamewakabidhi wasimamizi na wafanyakazi.”
Zebrali bowiem pieniądze, które znajdowały się w domu PANA, i oddali je do rąk nadzorców i robotników.
18 Kisha Shafani mwandishi akamwarifu mfalme kuwa, “Kuhani Hilkia amenipa Kitabu.” Naye Shafani akakisoma mbele ya mfalme.
Ponadto pisarz Szafan powiedział królowi: Kapłan Chilkiasz dał mi księgę. I czytał ją Szafan przed królem.
19 Mfalme aliposikia yale maneno ya Sheria, akayararua mavazi yake.
A gdy król usłyszał słowa prawa, rozdarł swoje szaty.
20 Akatoa maagizo haya kwa Hilkia, Ahikamu mwana wa Shafani, Abdoni mwana wa Mika, Shafani mwandishi na Asaya mtumishi wa mfalme,
Potem król rozkazał Chilkiaszowi, synowi Szafana, Achikamowi, synowi Micheasza, Abdonowi, a także pisarzowi Szafanowi oraz słudze króla Asajaszowi:
21 “Nendeni mkamuulize Bwana kwa ajili yangu na kwa ajili ya mabaki walioko Israeli na Yuda kuhusu yale yaliyoandikwa ndani ya kitabu hiki ambacho kimepatikana. Hasira ya Bwana ni kubwa mno ambayo imemwagwa juu yetu kwa sababu baba zetu hawakulishika neno la Bwana wala hawajatenda kulingana na yale yote yaliyoandikwa katika Kitabu hiki.”
Idźcie, poradźcie się PANA co do mnie i co do reszty [ludu] w Izraelu i Judzie w związku ze słowami tej księgi, którą znaleziono. Wielki bowiem jest gniew PANA, który został wylany na nas za to, że nasi ojcowie nie strzegli słowa PANA, aby czynić wszystko, co jest napisane w tej księdze.
22 Hilkia pamoja na wale wote mfalme aliokuwa amewatuma pamoja naye wakaenda kuzungumza na nabii mke aitwaye Hulda, aliyekuwa mke wa Shalumu mwana wa Tokhathi, mwana wa Hasra mtunzaji wa chumba cha mavazi. Hulda aliishi Yerusalemu, katika Mtaa wa Pili.
Tak więc poszedł Chilkiasz wraz z tymi, którzy byli przy królu, do prorokini Chuldy, żony Szalluma, syna Tikwy, syna Chasry, strażnika szat – mieszkała ona w Jerozolimie, po drugiej stronie [miasta] – i opowiedzieli jej [o tej sprawie].
23 Akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambieni yule mtu aliyewatuma ninyi kwangu,
Ona zaś powiedziała im: Tak mówi PAN, Bóg Izraela: Powiedzcie mężczyźnie, który was posłał do mnie:
24 ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Nitaleta maafa juu ya mahali hapa na watu wake, laana zote zilizoandikwa ndani ya hicho kitabu ambazo zimesomwa mbele ya mfalme wa Yuda.
Tak mówi PAN: Oto sprowadzę nieszczęście na to miejsce i na jego mieszkańców, wszystkie przekleństwa zapisane w tej księdze, którą czytali przed królem Judy;
25 Kwa sababu wameniacha mimi na kufukiza uvumba kwa miungu mingine na kunighadhibisha kwa kazi yote ya mikono yao, hivyo hasira yangu itamwagwa juu ya mahali hapa, wala haitatulizwa.’
Za to, że mnie opuścili i palili kadzidło innym bogom, aby pobudzić mnie do gniewu wszystkimi dziełami swoich rąk. Dlatego mój gniew zostanie wylany na to miejsce i nie zagaśnie.
26 Mwambieni mfalme wa Yuda, ambaye amewatuma kumuuliza Bwana, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli kuhusu maneno uliyoyasikia:
A królowi Judy, który was posłał po radę do PANA, powiedzcie: Tak mówi PAN, Bóg Izraela, o słowach, które słyszałeś:
27 Kwa kuwa moyo wako ulikuwa msikivu na ulijinyenyekeza mbele za Mungu uliposikia kile nilichosema dhidi ya mahali hapa na watu wake na kwa sababu ulijinyenyekeza mbele zangu na uliyararua mavazi yako na kulia mbele zangu, nimekusikia, asema Bwana.
Ponieważ twoje serce zmiękło i ukorzyłeś się przed obliczem Boga, gdy usłyszałeś jego słowa przeciwko temu miejscu i przeciwko jego mieszkańcom, a ukorzyłeś się przede mną, rozdarłeś swoje szaty i płakałeś przede mną, to również i ja wysłuchałem [ciebie], mówi PAN;
28 Basi nitakukusanya kwa baba zako, nawe utazikwa kwa amani. Macho yako hayataona maafa yote nitakayoleta juu ya mahali hapa na juu ya wote wanaoishi hapa.’” Kwa hiyo wakampelekea mfalme jibu lake.
Oto przyłączę cię do twoich ojców i będziesz złożony w swoim grobie w pokoju, aby twoje oczy nie oglądały całego nieszczęścia, które sprowadzam na to miejsce i jego mieszkańców. I zanieśli tę odpowiedź królowi.
29 Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
Wtedy król posłał po wszystkich starszych Judy i Jerozolimy i zgromadził [ich].
30 Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na Walawi, watu wote, wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
Następnie udał się do domu PANA, a wraz z nim wszyscy mężczyźni Judy, mieszkańcy Jerozolimy, kapłani i Lewici oraz cały lud, od największych do najmniejszych. I czytał do ich uszu wszystkie słowa księgi przymierza, którą znaleziono w domu PANA.
31 Mfalme akasimama karibu na nguzo yake na kufanya upya Agano mbele za Bwana ili kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote na ili kuyatii maneno ya Agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
Potem król stanął na swoim miejscu i zawarł przymierze przed PANEM, że będą szli za PANEM i będą przestrzegać jego przykazań, świadectw, nakazów z całego serca, całą swoją duszą i wypełniać słowa tego przymierza, które zostały zapisane w tej księdze.
32 Ndipo akamtaka kila mmoja katika Yerusalemu na Benyamini kuweka ahadi zao wenyewe kwa hilo Agano, watu wa Yerusalemu wakafanya hivyo kwa kufuata Agano la Bwana, Mungu wa baba zao.
Wtedy król nakazał przystąpić do [przymierza] wszystkim, którzy znajdowali się w Jerozolimie i Beniaminie. I mieszkańcy Jerozolimy postąpili zgodnie z przymierzem Boga, Boga swoich ojców.
33 Yosia akaondoa machukizo yote ya sanamu kutoka nchi yote iliyokuwa mali ya Waisraeli na akawataka wale wote waliokuwako katika Israeli wamtumikie Bwana Mungu wao. Kwa muda wote alioishi, hawakushindwa kumfuata Bwana, Mungu wa baba zao.
Wówczas Jozjasz usunął wszystkie obrzydliwości ze wszystkich ziem synów Izraela i zobowiązał wszystkich, którzy się znajdowali w Izraelu, aby służyli PANU, swemu Bogu. Przez wszystkie jego dni nie odstąpili od naśladowania PANA, Boga swoich ojców.

< 2 Nyakati 34 >