< 2 Nyakati 33 >

1 Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na mitano.
Manasses miał dwanaście lat, kiedy zaczął królować, i królował pięćdziesiąt pięć lat w Jerozolimie.
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana, akafuata desturi za machukizo za mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
Czynił on to, co złe w oczach PANA, według obrzydliwości tych narodów, które PAN wypędził przed synami Izraela.
3 Akajenga upya mahali pa juu pa kuabudia miungu ambapo Hezekia baba yake, alikuwa amepabomoa, pia akasimamisha madhabahu za Mabaali na nguzo za Maashera. Akalisujudia jeshi lote la angani na kuliabudu.
Odbudował bowiem wyżyny, które zburzył jego ojciec Ezechiasz, wznosił ołtarze dla Baalów, posadził gaje i oddawał pokłon całemu zastępowi nieba, i służył im.
4 Akajenga madhabahu katika Hekalu la Bwana ambamo Bwana alikuwa amesema, “Jina langu litadumu Yerusalemu milele.”
Zbudował też ołtarze w domu PANA, o którym PAN powiedział: W Jerozolimie będzie moje imię na wieki.
5 Katika nyua zote mbili za Hekalu la Bwana akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la angani.
Ponadto zbudował ołtarze całemu zastępowi nieba w obydwu dziedzińcach domu PANA.
6 Akawatoa wanawe kuwa kafara kwa kuwapitisha katika moto katika Bonde la Ben-Hinomu, akafanya ulozi, uaguzi na uchawi, akataka ushauri kwa wenye pepo wa utambuzi na wenye kuwasiliana na mizimu. Akafanya maovu mengi machoni pa Bwana, akaichochea hasira yake.
Przeprowadził swoich synów przez ogień w dolinie syna Hinnom. Uprawiał wróżbiarstwo, czary i magię, ustanowił czarowników i czarnoksiężników. Bardzo dużo złego czynił w oczach PANA, pobudzając go do gniewu.
7 Akachukua ile sanamu aliyoichonga na kuiweka katika Hekalu la Mungu ambalo Mungu alikuwa amemwambia Daudi na mwanawe Solomoni, “Katika Hekalu hili na katika Yerusalemu niliouchagua kutoka kabila zote za Israeli, nitaliweka Jina langu milele.
Postawił też posąg rzeźbiony, który wykonał, w domu Bożym, o którym Bóg powiedział do Dawida i do jego syna Salomona: W tym domu i w Jerozolimie, które wybrałem spośród wszystkich pokoleń Izraela, umieszczę swoje imię na wieki;
8 Sitaifanya tena miguu ya Waisraeli iondoke tena katika nchi niliyowapa baba zenu, ikiwa watakuwa waangalifu kufanya kila kitu nilichowaamuru kuhusu sheria zote, maagizo na amri zilizotolewa kwa mkono wa Mose.”
A już nie dopuszczę, by noga Izraela opuściła ziemię, którą przeznaczyłem waszym ojcom, jeśli tylko pilnie będą przestrzegali wszystkiego, co im nakazałem, [według] całego prawa, nakazów i ustaw [przekazanych] przez Mojżesza.
9 Lakini Manase akawaongoza Yuda na watu wa Yerusalemu katika upotovu, kiasi kwamba walifanya maovu mengi kuliko mataifa ambayo Bwana aliwaangamiza mbele ya Waisraeli.
Manasses zwiódł Judę i mieszkańców Jerozolimy tak, że postępowali gorzej niż narody, które PAN wytracił przed synami Izraela.
10 Bwana akasema na Manase pamoja na watu wake, lakini hawakumjali.
[Chociaż] bowiem PAN mówił do Manassesa i do jego ludu, oni nie słuchali.
11 Hivyo Bwana akaleta juu yao majemadari wa jeshi la mfalme wa Ashuru, ambao walimchukua Manase kwenda kifungoni, wakaweka ndoana katika pua yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
Dlatego PAN sprowadził na nich dowódców wojska króla Asyrii, którzy pojmali Manassesa spośród cierni, zakuli go w łańcuchy i zaprowadzili do Babilonu.
12 Katika dhiki yake akamsihi Bwana Mungu wake na kujinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake.
Kiedy znalazł się w ucisku, modlił się do PANA, swego Boga, i bardzo się ukorzył przed Bogiem swoich ojców;
13 Naye alipomwomba, Bwana akaguswa na kule kusihi kwake na akasikiliza kilio chake, kwa hiyo akamrudisha Yerusalemu na kwenye ufalme wake. Ndipo Manase akatambua kwamba Bwana ndiye Mungu.
I modlił się do niego. A on dał się przebłagać, wysłuchał jego modlitwy i przywrócił go do Jerozolimy, do jego królestwa. Wtedy Manasses uznał, że PAN [jest] Bogiem.
14 Baadaye akajenga ukuta wa nje wa Mji wa Daudi, magharibi mwa chemchemi ya Gihoni katika bonde, hadi kufikia ingilio la Lango la Samaki na akakizunguka kilima cha Ofeli, pia akaufanya kuwa mrefu zaidi. Akawaweka majemadari katika miji yote ya Yuda iliyokuwa imejengewa ngome.
Potem zbudował zewnętrzny mur miasta Dawida, na zachód w kierunku Gichonu, w dolinie, aż do wejścia do Bramy Rybnej, otoczył [nim] Ofel i wzniósł go bardzo wysoko. Ustanowił też dowódców we wszystkich warownych miastach Judy.
15 Akaondolea mbali miungu ya kigeni na kuondoa sanamu kutoka Hekalu la Bwana pamoja na madhabahu zote alizozijenga katika kile kilima kilichojengwa Hekalu na katika Yerusalemu, akazitupa nje ya mji.
Usunął również cudzych bogów i posąg z domu PANA oraz wszystkie ołtarze, które zbudował na górze domu PANA i w Jerozolimie, następnie wyrzucił poza miasto.
16 Kisha akarudisha madhabahu ya Bwana na kutolea juu yake dhabihu za sadaka za amani pamoja na sadaka za shukrani, naye akawaamuru Yuda wamtumikie Bwana, Mungu wa Israeli.
Odnowił ołtarz PANA i złożył na nim ofiary pojednawcze i dziękczynne, a nakazał Judzie służyć PANU, Bogu Izraela.
17 Lakini hata hivyo watu wakaendelea kutoa dhabihu mahali pa juu pa kuabudia miungu, lakini wakimtolea Bwana Mungu wao peke yake.
Lud jednak jeszcze składał ofiary na wyżynach, ale tylko PANU, swemu Bogu.
18 Matukio mengine ya utawala wa Manase, maombi yake kwa Mungu wake na maneno aliyoambiwa na waonaji walionena naye kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
A pozostałe dzieje Manassesa, jego modlitwa do swojego Boga i słowa widzących, którzy przemawiali do niego w imię PANA, Boga Izraela, [są zapisane] w księdze królów Izraela.
19 Maombi yake, pamoja na jinsi Mungu alivyoguswa na kusihi kwake, pia dhambi zake zote na kukosa kwake uaminifu pamoja na sehemu alizojenga mahali pa juu pa kuabudia miungu, kule kusimamisha nguzo za Ashera na sanamu kabla ya kujinyenyekeza kwake, yote yameandikwa katika kumbukumbu za waonaji.
Jego modlitwa, to, [jak] został wysłuchany, każdy jego grzech, [każde] przewinienie oraz miejsca, na których zbudował wyżyny i wystawił gaje i posągi, zanim się ukorzył, są zapisane w księgach widzących.
20 Manase akalala pamoja na baba zake akazikwa katika jumba lake la kifalme. Naye Amoni mwanawe akawa mfalme baada yake.
Potem Manasses zasnął ze swoimi ojcami i pogrzebano go w jego domu, a jego syn Amon królował w jego miejsce.
21 Amoni alikuwa na miaka ishirini na miwili, alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka miwili.
Amon miał dwadzieścia dwa lata, kiedy zaczął królować, i królował dwa lata w Jerozolimie.
22 Akatenda maovu machoni mwa Bwana, kama baba yake Manase alivyofanya. Amoni akaabudu na kutoa dhabihu kwa sanamu zote alizokuwa ametengeneza Manase.
I czynił to, co złe w oczach PANA, tak jak czynił jego ojciec Manasses. Amon bowiem składał ofiary wszystkim posągom, które sporządził jego ojciec Manasses, i służył im.
23 Lakini tofauti na Manase baba yake, hakujinyenyekeza mbele za Bwana, badala yake Amoni aliongeza hatia zaidi na zaidi.
A nie ukorzył się przed PANEM, tak jak ukorzył się jego ojciec Manasses. Przeciwnie, Amon grzeszył coraz bardziej.
24 Watumishi wa Amoni wakafanya fitina juu yake, nao wakamuulia kwake nyumbani.
I jego słudzy sprzysięgli się przeciwko niemu, i zabili go w jego domu.
25 Kisha watu wa nchi wakawaua wale wote waliokuwa wamefanya hila dhidi ya Mfalme Amoni. Wakamfanya Yosia mwanawe kuwa mfalme mahali pake.
Ale lud tej ziemi zabił wszystkich, którzy sprzysięgli się przeciw królowi Amonowi, a potem ustanowił jego syna Jozjasza królem w jego miejsce.

< 2 Nyakati 33 >