< 2 Nyakati 33 >

1 Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na mitano.
Manasus bija divpadsmit gadus vecs, kad palika par ķēniņu, un valdīja piecdesmit pieci gadus Jeruzālemē,
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana, akafuata desturi za machukizo za mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
Un darīja, kas Tam Kungam nepatika, pēc to tautu negantībām, ko Tas Kungs Israēla bērnu priekšā bija izdzinis.
3 Akajenga upya mahali pa juu pa kuabudia miungu ambapo Hezekia baba yake, alikuwa amepabomoa, pia akasimamisha madhabahu za Mabaali na nguzo za Maashera. Akalisujudia jeshi lote la angani na kuliabudu.
Jo tas uztaisīja atkal kalnu altārus, ko viņa tēvs Hizkija bija nolauzījis, un uztaisīja altārus Baāliem un taisīja Ašeras un metās zemē priekš visa debess spēka un tiem kalpoja.
4 Akajenga madhabahu katika Hekalu la Bwana ambamo Bwana alikuwa amesema, “Jina langu litadumu Yerusalemu milele.”
Viņš taisīja altārus arī Tā Kunga namā, par ko Tas Kungs bija sacījis: Jeruzālemē lai ir mans vārds mūžīgi.
5 Katika nyua zote mbili za Hekalu la Bwana akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la angani.
Un visam debess spēkam viņš cēla altārus Tā Kunga nama abējos pagalmos.
6 Akawatoa wanawe kuwa kafara kwa kuwapitisha katika moto katika Bonde la Ben-Hinomu, akafanya ulozi, uaguzi na uchawi, akataka ushauri kwa wenye pepo wa utambuzi na wenye kuwasiliana na mizimu. Akafanya maovu mengi machoni pa Bwana, akaichochea hasira yake.
Un viņš lika saviem dēliem caur uguni iet Ben-Inoma ielejā un zīlēja un vārdoja un būra un turēja zīlniekus un pūšļotājus; viņš darīja ļoti daudz, kas Tam Kungam nepatika, viņu kaitinādams.
7 Akachukua ile sanamu aliyoichonga na kuiweka katika Hekalu la Mungu ambalo Mungu alikuwa amemwambia Daudi na mwanawe Solomoni, “Katika Hekalu hili na katika Yerusalemu niliouchagua kutoka kabila zote za Israeli, nitaliweka Jina langu milele.
Arī elka tēlu, ko bija taisījis, viņš uzcēla Dieva namā, par ko Dievs uz Dāvidu un viņa dēlu Salamanu bija sacījis: šinī namā un Jeruzālemē, ko Es esmu izredzējis no visām Israēla ciltīm, Es Savu vārdu iecelšu mūžīgi.
8 Sitaifanya tena miguu ya Waisraeli iondoke tena katika nchi niliyowapa baba zenu, ikiwa watakuwa waangalifu kufanya kila kitu nilichowaamuru kuhusu sheria zote, maagizo na amri zilizotolewa kwa mkono wa Mose.”
Un Israēla kājai Es vairs nelikšu kustēt no tās zemes, ko Es jūsu tēviem esmu nolicis, ja tie visu turēs un darīs, ko Es tiem esmu pavēlējis, pēc visas bauslības un likumiem un tiesām caur Mozu.
9 Lakini Manase akawaongoza Yuda na watu wa Yerusalemu katika upotovu, kiasi kwamba walifanya maovu mengi kuliko mataifa ambayo Bwana aliwaangamiza mbele ya Waisraeli.
Tā Manasus Jūdu un Jeruzālemes iedzīvotājus vedināja uz ļaunu, ka tie niknāki darīja, nekā tie pagāni, ko Tas Kungs Israēla bērnu priekšā bija izdeldējis.
10 Bwana akasema na Manase pamoja na watu wake, lakini hawakumjali.
Un Tas Kungs gan runāja uz Manasu un uz viņa ļaudīm, bet tie neņēma vērā.
11 Hivyo Bwana akaleta juu yao majemadari wa jeshi la mfalme wa Ashuru, ambao walimchukua Manase kwenda kifungoni, wakaweka ndoana katika pua yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
Tāpēc Tas Kungs tiem sūtīja Asīrijas ķēniņa kara virsniekus; tie gūstīja Manasu saitēm un to apcietināja ar divām vara ķēdēm un to noveda uz Bābeli.
12 Katika dhiki yake akamsihi Bwana Mungu wake na kujinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake.
Kad tas nu tā bija spaidos, tad tas pielūdza To Kungu, savu Dievu, un pazemojās ļoti priekš savu tēvu Dieva
13 Naye alipomwomba, Bwana akaguswa na kule kusihi kwake na akasikiliza kilio chake, kwa hiyo akamrudisha Yerusalemu na kwenye ufalme wake. Ndipo Manase akatambua kwamba Bwana ndiye Mungu.
Un lūdza Viņu. Un Viņš no tā ļāvās pielūgties un paklausīja viņa sirsnīgo lūgšanu un pārveda to atkal uz Jeruzālemi viņa valstībā. Tad Manasus atzina, ka Tas Kungs ir Dievs.
14 Baadaye akajenga ukuta wa nje wa Mji wa Daudi, magharibi mwa chemchemi ya Gihoni katika bonde, hadi kufikia ingilio la Lango la Samaki na akakizunguka kilima cha Ofeli, pia akaufanya kuwa mrefu zaidi. Akawaweka majemadari katika miji yote ya Yuda iliyokuwa imejengewa ngome.
Un pēc tam viņš uztaisīja Dāvida pilsētas āra mūri uz Ģiona pusi pret vakariem ielejā līdz tai vietai, kur ieiet pa Zivju vārtiem, un apkārt Ofelam, un to taisīja ļoti augstu, un ielika arīdzan kara virsniekus visās stiprās Jūda pilsētās.
15 Akaondolea mbali miungu ya kigeni na kuondoa sanamu kutoka Hekalu la Bwana pamoja na madhabahu zote alizozijenga katika kile kilima kilichojengwa Hekalu na katika Yerusalemu, akazitupa nje ya mji.
Un viņš nopostīja tos svešos dievus un to elku no Tā Kunga nama, ar visiem altāriem, ko viņš bija uztaisījis Tā Kunga nama kalnā un Jeruzālemē un izmeta tos ārā no pilsētas.
16 Kisha akarudisha madhabahu ya Bwana na kutolea juu yake dhabihu za sadaka za amani pamoja na sadaka za shukrani, naye akawaamuru Yuda wamtumikie Bwana, Mungu wa Israeli.
Un viņš uzkopa Tā Kunga altāri un upurēja uz tā pateicības upurus un slavas upurus, un pavēlēja Jūda ļaudīm, kalpot Tam Kungam, Israēla Dievam.
17 Lakini hata hivyo watu wakaendelea kutoa dhabihu mahali pa juu pa kuabudia miungu, lakini wakimtolea Bwana Mungu wao peke yake.
Taču tie ļaudis vēl upurēja kalnos, bet Tam Kungam savam Dievam.
18 Matukio mengine ya utawala wa Manase, maombi yake kwa Mungu wake na maneno aliyoambiwa na waonaji walionena naye kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Un kas vēl par Manasu stāstāms, un viņa lūgšana uz savu Dievu un to redzētāju vārdi, kas uz viņu runājuši Tā Kunga, Israēla Dieva, vārdā, redzi, tas ir Israēla ķēniņu stāstos.
19 Maombi yake, pamoja na jinsi Mungu alivyoguswa na kusihi kwake, pia dhambi zake zote na kukosa kwake uaminifu pamoja na sehemu alizojenga mahali pa juu pa kuabudia miungu, kule kusimamisha nguzo za Ashera na sanamu kabla ya kujinyenyekeza kwake, yote yameandikwa katika kumbukumbu za waonaji.
Un viņa lūgšana un kā Dievs viņu paklausījis, arī visi viņa grēki un viņa pārkāpumi, un tās vietas, kur viņš uztaisījis elku altārus un uzcēlis Ašeras un elku tēlus, pirms tapa pazemots, tas rakstīts Kazaja stāstos.
20 Manase akalala pamoja na baba zake akazikwa katika jumba lake la kifalme. Naye Amoni mwanawe akawa mfalme baada yake.
Un Manasus aizmiga pie saviem tēviem, un to apraka viņa namā, un viņa dēls Amons palika par ķēniņu viņa vietā.
21 Amoni alikuwa na miaka ishirini na miwili, alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka miwili.
Amons bija divdesmit divus gadus vecs, kad palika par ķēniņu, un valdīja divus gadus Jeruzālemē.
22 Akatenda maovu machoni mwa Bwana, kama baba yake Manase alivyofanya. Amoni akaabudu na kutoa dhabihu kwa sanamu zote alizokuwa ametengeneza Manase.
Un viņš darīja, kas Tam Kungam nepatika, tā kā viņa tēvs Manasus bija darījis, un Amons upurēja visiem elku tēliem, ko viņa tēvs Manasus bija taisījis, un tiem kalpoja.
23 Lakini tofauti na Manase baba yake, hakujinyenyekeza mbele za Bwana, badala yake Amoni aliongeza hatia zaidi na zaidi.
Bet viņš nepazemojās Tā Kunga priekšā, tā kā viņa tēvs Manasus bija pazemojies; bet šis Amons vairoja noziegumu.
24 Watumishi wa Amoni wakafanya fitina juu yake, nao wakamuulia kwake nyumbani.
Un viņa kalpi sacēlās pret viņu un to nokāva viņa namā.
25 Kisha watu wa nchi wakawaua wale wote waliokuwa wamefanya hila dhidi ya Mfalme Amoni. Wakamfanya Yosia mwanawe kuwa mfalme mahali pake.
Un tie zemes ļaudis nokāva visus, kas bija sacēlušies pret ķēniņu Amonu, un tie zemes ļaudis cēla Josiju, viņa dēlu, par ķēniņu viņa vietā.

< 2 Nyakati 33 >