< 2 Nyakati 32 >
1 Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaja na kuvamia Yuda. Akaizunguka miji yenye ngome kwa jeshi, akifikiri kuiteka iwe yake.
Après ces choses si fidèlement exécutées, Sennachérib, roi des Assyriens, vint et entra dans Juda; il assiégea les villes fortifiées, voulant les prendre.
2 Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu,
Lorsqu’Ezéchias eut vu cela, savoir que Sennachérib était venu, et que tout l’effort de la guerre était tourné contre Jérusalem,
3 akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia.
Il tint conseil avec les princes et les hommes les plus braves, pour boucher les sources des fontaines qui étaient hors de la ville: l’avis de tous l’ayant décidé,
4 Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?”
Il assembla une très grande multitude, et il boucha toutes les sources, et le ruisseau qui coulait au milieu du pays, disant: C’est de peur que les rois des Assyriens ne viennent, et ne trouvent une abondance d’eau.
5 Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha Milo katika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.
Il bâtit aussi avec grand soin tout le mur qui avait été ruiné, et il construisit les tours au dessus, et en dehors de l’autre mur; il restaura Mello dans la cité de David, et il fit des armes de tout genre et des boucliers;
6 Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya:
Et il établit ensuite des chefs de combattants dans l’armée; puis il les convoqua sur la place de la porte de la cité, et il parla à leur cœur, disant:
7 “Kuweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye.
Agissez courageusement, et fortifiez-vous: ne craignez point, et ne redoutez point le roi des Assyriens, ni toute cette multitude qui est avec lui; car il y a un plus grand nombre avec nous qu’avec lui.
8 Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yuko Bwana Mungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.
Car avec lui est un bras de chair; avec nous le Seigneur notre Dieu, qui est notre aide et combat pour nous. Et le peuple fut fortifié par ces paroles d’Ezéchias, roi de Juda.
9 Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akawatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda, na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo, kusema:
Après que ces choses se furent passées, Sennachérib, roi des Assyriens, envoya ses serviteurs à Jérusalem (car lui-même assiégeait Lachis avec toute son armée) vers Ezéchias, roi de Juda, et vers tout le peuple qui était dans la ville, disant:
10 “Hili ndilo asemalo Senakeribu mfalme wa Ashuru: Je, mmeweka tumaini lenu wapi, hata mnaendelea kukaa katika Yerusalemu, hali mmezungukwa na jeshi?
Voici ce que dit Sennachérib, roi des Assyriens: En qui avez-vous confiance, pour demeurer ainsi assiégés dans Jérusalem?
11 Hezekia asemapo, ‘Bwana Mungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, naye atawaacha mfe kwa njaa na kiu.
Est-ce qu’Ézéchias ne vous trompe pas pour vous livrer à la mort par la faim et la soif, vous assurant que le Seigneur votre Dieu vous délivrera de la main du roi des Assyriens?
12 Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?
N’est-ce pas cet Ezéchias qui a détruit ses hauts lieux et ses autels, et qui a ordonné à Juda et à Jérusalem, disant: C’est devant un seul autel que vous adorerez, et c’est sur cet autel que vous brûlerez de l’encens?
13 “Je, hamjui yale mimi na baba zangu tuliyoyafanya kwa mataifa yote ya nchi zingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu?
Est-ce que vous ignorez ce que j’ai fait, moi et mes pères, à tous les peuples de la terre? Est-ce que les dieux des nations et de toute la terre ont été assez forts pour délivrer leur pays de ma main?
14 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza ameweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Mungu wenu kuwaokoa mkononi mwangu?
Quel est celui de tous les dieux des nations que mes pères ont ravagées, qui ait pu délivrer son peuple de ma main, pour que même votre Dieu puisse vous délivrer de ma main?
15 Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye na kuwapotosha namna hii. Msimwamini, kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lolote wala wa ufalme wowote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”
Qu’Ézéchias ne vous trompe donc point, et que par une vaine persuasion il ne vous joue point: ne le croyez pas. Car si aucun dieu de toutes les nations et de tous les royaumes n’a pu délivrer son peuple de ma main ni de celle de mes pères, conséquemment même votre Dieu ne pourra pas vous délivrer de ma main.
16 Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi ya Bwana aliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia.
Mais les serviteurs de Sennachérib dirent encore beaucoup d’autres choses contre le Seigneur Dieu et contre Ezéchias, son serviteur.
17 Mfalme pia aliandika barua akimtukana Bwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.”
Il écrivit aussi des lettres pleines de blasphèmes contre le Seigneur Dieu d’Israël, et il dit contre lui: Comme les dieux des autres nations n’ont pu délivrer leur peuple de ma main, ainsi même le Dieu d’Ezéchias ne pourra pas délivrer son peuple de cette main.
18 Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji.
De plus, d’une voix forte et en langue judaïque, il criait contre le peuple qui était sur les murs de Jérusalem, pour l’épouvanter et prendre la ville.
19 Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.
Ainsi il parla contre le Dieu de Jérusalem comme contre les dieux des peuples de la terre, ouvrages des mains des hommes.
20 Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili.
Le roi Ezéchias donc, et Isaïe, le prophète, fils d’Amos, prièrent en opposition à ce blasphème, et poussèrent des cris jusqu’au ciel.
21 Naye Bwana akamtuma malaika ambaye aliangamiza wanajeshi wote, na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akarudi nchini mwake kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua kwa upanga.
Et le Seigneur envoya un ange qui frappa tout homme vigoureux, guerrier et le prince de l’armée du roi des Assyriens; et Sennachérib retourna avec ignominie en son pays. Or, lorsqu’il fut entré dans la maison de son dieu, ses fils, qui étaient sortis de ses entrailles, le tuèrent par le glaive.
22 Hivyo Bwana akamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote. Bwana akawastarehesha kila upande.
Le Seigneur sauva ainsi Ezéchias et les habitants de Jérusalem de la main de Sennachérib, roi des Assyriens, et de la main de tous, et il leur donna le repos alentour.
23 Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili ya Bwana na zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.
Beaucoup même portaient des hosties et des sacrifices au Seigneur à Jérusalem, et des présents à Ezéchias, roi de Juda, qui a été exalté après cela devant toutes les nations.
24 Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Akamwomba Bwana, ambaye alimjibu na kumpa ishara.
En ces jours-là, Ezéchias fut malade jusqu’à la mort, et il pria le Seigneur, et le Seigneur l’exauça, et il lui en donna un signe.
25 Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana ikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu.
Mais Ezéchias ne rendit pas à Dieu selon les biens qu’il avait reçus, parce que son cœur s’éleva, et la colère du Seigneur s’alluma contre lui, contre Juda et contre Jérusalem.
26 Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana haikuja juu yao katika siku za Hezekia.
Mais ensuite il s’humilia autant lui-même que les habitants de Jérusalem, de ce que son cœur s’était exalté: et c’est pourquoi la colère du Seigneur ne vint point sur eux dans les jours d’Ezéchias.
27 Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani.
Or Ezéchias fut riche et très illustre; il s’amassa beaucoup de trésors d’argent, d’or, de pierres précieuses, d’aromates, d’armes de tout genre, et de vases de grand prix.
28 Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi.
Il avait aussi des magasins de blé, devin et d’huile, des écuries pour toute sorte de gros bétail, et des parcs pour des troupeaux.
29 Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ngʼombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.
Et il bâtit des villes pour lui; car il avait des troupeaux de brebis et de gros bétail innombrables, parce que le Seigneur lui avait donné des biens en très grande abondance.
30 Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya.
C’est ce même Ezéchias qui boucha la fontaine supérieure des eaux de Gihon, et les détourna sous terre vers l’occident de la ville de David; en toutes ses œuvres il fit heureusement ce qu’il voulut.
31 Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumuuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.
Cependant dans le message des princes de Babylone qui avaient été envoyés vers lui pour s’informer du prodige qui était arrivé sur la terre. Dieu l’abandonna pour le tenter et pour faire connaître tout ce qui était en son cœur.
32 Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
Mais le reste des actions d’Ezéchias et de ses miséricordes est écrit dans la vision d’Isaïe, le prophète, fils d’Amos, et dans le Livre des rois de Juda et d’Israël.
33 Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipofariki. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.
Ezéchias dormit avec ses pères, et on l’ensevelit au dessus du sépulcre des fils de David: tout Juda célébra ses funérailles, et tous les habitants de Jérusalem; et Manassé son fils régna en sa place.