< 2 Nyakati 32 >

1 Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaja na kuvamia Yuda. Akaizunguka miji yenye ngome kwa jeshi, akifikiri kuiteka iwe yake.
Aftir whiche thingis and sich treuthe, Senacherib, the kyng of Assiriens, cam and entride in to Juda; and he bisegide stronge citees, and wolde take tho.
2 Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu,
And whanne Ezechie hadde herd this thing, that is, that Senacherib was comun, and that al the fersnesse of batel was turned ayens Jerusalem,
3 akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia.
he took counsel with the princes and strongest men, that thei schulden stoppe the heedis of wellis, that weren without the citee; and whanne the sentence of alle men demyde this,
4 Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?”
he gaderide togidere a ful greet multitude, and thei stoppiden alle the wellis, and the ryuer, that flowide in the myddis of the lond; and seiden, Lest the kyngis of Assiriens comen, and fynden abundance of watris.
5 Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha Milo katika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.
Also he dide wittili, and bildide al the wal that was distride, and he bildide touris aboue, and an other wal withoutforth. And he reparilide Mello in the citee of Dauid; and made armure of al kynde, and scheldis.
6 Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya:
And he ordeynede princes of werriouris in the oost; and he clepide togidere alle men in the street of the yate of the citee, and spake to the herte of hem,
7 “Kuweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye.
and seide, Do ye manli, and be ye coumfortid; nyle ye drede, nether be ye aferd of the kyng of Assiriens, and of al the multitude which is with him; for many mo ben with vs than with him.
8 Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yuko Bwana Mungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.
Fleischli arm is with him; `oure Lord God is with vs, which is oure helpere, and schal fiyte for vs. And the puple was coumfortid with sich wordis of Ezechie, kyng of Juda.
9 Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akawatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda, na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo, kusema:
And aftir that these thingis weren doon, Sennacherib sente hise seruauntis to Jerusalem; for he `with al the oost bisegide Lachis. He sente to Ezechie, kyng of Juda, and to al the puple that was in the citee,
10 “Hili ndilo asemalo Senakeribu mfalme wa Ashuru: Je, mmeweka tumaini lenu wapi, hata mnaendelea kukaa katika Yerusalemu, hali mmezungukwa na jeshi?
and seide, Sennacherib, the kyng of Assiriens, seith these thingis, In whom han ye trist, and sitten bisegid in Jerusalem?
11 Hezekia asemapo, ‘Bwana Mungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, naye atawaacha mfe kwa njaa na kiu.
Whether Ezechie disseyueth you, that he bitake you to deeth in hungur and thirst, and affermeth, that `youre Lord God schal delyuere you fro the hond of the kyng of Assyriens?
12 Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?
Whether not this is Ezechie, that distriede hiy places, and auteris of hym, and comaundide to Juda and to Jerusalem, and seide, Ye schulen worschipe bifor oon auter, and therynne ye schulen brenne encense?
13 “Je, hamjui yale mimi na baba zangu tuliyoyafanya kwa mataifa yote ya nchi zingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu?
Whether ye witen not what thingis Y haue do, and my fadir, to alle the puplis of londis? Whether the goddis of folkis and of alle londis myyten delyuere her cuntrei fro myn hond?
14 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza ameweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Mungu wenu kuwaokoa mkononi mwangu?
Who is of alle goddis of folkis, whiche my fadris distrieden, that myyte delyuere his puple fro myn hond, that also youre God may delyuere you fro this hond?
15 Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye na kuwapotosha namna hii. Msimwamini, kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lolote wala wa ufalme wowote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”
Therfor Ezechie disseyue not you, nether scorne bi veyn counselyng, nethir bileue ye to hym; for if no god of alle folkis and cuntreis myyte delyuere his puple fro myn hond, and fro the hond of my fadris, suyngli nether youre God schal mowe delyuere you fro this myn hond.
16 Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi ya Bwana aliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia.
But also hise seruauntis spaken many othir thingis ayenus the Lord God, and ayens Ezechie, his seruaunte.
17 Mfalme pia aliandika barua akimtukana Bwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.”
Also he wroot epistlis ful of blasfemye ayens the Lord God of Israel, and he spak ayens God, As the goddis of othere folkis myyten not delyuere her puple fro myn hond, so and the God of Ezechie may not delyuere his puple fro myn hond.
18 Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji.
Ferthermore and with greet cry in the langage of Jewis he sownede ayens the puple, that sat on the wallis of Jerusalem, to make hem aferd, and to take the citee.
19 Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.
And he spake ayens God of Israel, as ayens the goddis of the puplis of erthe, the werkis of mennus hondis.
20 Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili.
Therfor Ezechie, the kyng, and Ysaie, the profete, the sone of Amos, preieden ayens this blasfemye, and crieden til in to heuene.
21 Naye Bwana akamtuma malaika ambaye aliangamiza wanajeshi wote, na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akarudi nchini mwake kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua kwa upanga.
And the Lord sente his aungel, that killide ech strong man and werriour, and the prince of the oost of the kyng of Assiriens; and he turnede ayen with schenship `in to his lond. And whanne he hadde entrid in to the hows of his god, the sones, that yeden out of his wombe, killiden hym with swerd.
22 Hivyo Bwana akamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote. Bwana akawastarehesha kila upande.
And the Lord sauyde Ezechie, and the dwelleris of Jerusalem, fro the hond of Senacherib, kyng of Assiriens, and fro the hond of alle men; and yaf to hem reste bi cumpas.
23 Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili ya Bwana na zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.
Also many men brouyten offryngis and sacrifices to the Lord in to Jerusalem, and yiftis to Ezechie, kyng of Juda; which was enhaunsid aftir these thingis bifor alle folkis.
24 Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Akamwomba Bwana, ambaye alimjibu na kumpa ishara.
In tho daies Ezechie was sijk `til to the deth, and he preiede the Lord; and he herde hym, and yaf to hym a signe;
25 Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana ikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu.
but he yeldide not bi the benefices whiche he hadde take, for his herte was reisid; and ire was maad ayens hym, and ayens Juda, and ayens Jerusalem.
26 Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana haikuja juu yao katika siku za Hezekia.
And he was mekid aftirward, for his herte was reisid; bothe he was mekid, and the dwelleris of Jerusalem; and therfor the ire of the Lord cam not on hem in the daies of Ezechie.
27 Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani.
Forsothe Ezechie was riche, and ful noble, and gaderide to hym silf ful many tresours of siluer, of gold, and of preciouse stoon, of swete smellynge spices, and of armuris of al kynde, and of vessels of greet prijs.
28 Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi.
Also he bildide large housis of wheete, of wyn, and of oile, and cratchis of alle beestis,
29 Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ngʼombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.
and fooldis to scheep, and sixe citees. For he hadde vnnoumbrable flockis of scheep and of grete beestis; for the Lord hadde youe to hym ful myche catel.
30 Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya.
Thilke is Ezechie, that stoppide the hiyere welle of the watris of Gion, and turnede tho awei vndur the erthe at the west of the citee of Dauid; in alle hise werkis he dide `bi prosperite, what euer thing he wolde.
31 Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumuuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.
Netheles in the message of the princes of Babiloyne, that weren sent to hym for to axe of the grete wondir, that bifelde on the lond, God forsook hym, that he were temptid, and that alle thingis weren knowun that weren in his herte.
32 Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
Sotheli the residue of wordis of Ezechie, and of hise mercies, ben writun in the profesie of Ysaie, the profete, sone of Amos, and in the book of kyngis of Juda and of Israel.
33 Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipofariki. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Ezechie slepte with hise fadris, and thei birieden hym aboue the sepulcris of the sones of Dauid. And al Juda and alle the dwelleris of Jerusalem maden solempne the seruyces of his biriyng; and Manasses, his sone, regnide for him.

< 2 Nyakati 32 >