< 2 Nyakati 32 >
1 Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaja na kuvamia Yuda. Akaizunguka miji yenye ngome kwa jeshi, akifikiri kuiteka iwe yake.
Efter disse Handeler og denne Troskab kom Senakerib, Kongen af Assyrien, og drog ind i Juda og lejrede sig imod de faste Stæder og tænkte at rive dem til sig.
2 Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu,
Der Ezekias saa, at Senakerib kom, og at hans Hu var til Krig imod Jerusalem,
3 akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia.
da raadførte han sig med sine Øverster og sine vældige om at tilstoppe Vandet fra Kilderne, som vare uden for Staden; og de hjalp ham.
4 Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?”
Thi meget Folk samlede sig og tilstoppede alle Kilder og den Bæk, som flød midt igennem Landet, og han sagde: Hvorfor skulde Assyriens Konger komme og finde meget Vand?
5 Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha Milo katika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.
Og han tog Mod til sig og byggede den ganske Mur, som var nedreven, og førte den op indtil Taarnene og en anden Mur der udenfor; og han befæstede Millo i Davids Stad og lod gøre Vaaben i Mangfoldighed og Skjolde.
6 Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya:
Og han satte Krigsøverster over Folket og samlede dem til sig paa Pladsen ved Stadens Port og talte kærligt med dem og sagde:
7 “Kuweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye.
Værer frimodige og værer stærke, frygter ikke og ræddes ikke for Kongen af Assyrien, ej heller for hele den Hob, som er med ham; thi der er en større med os end med ham.
8 Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yuko Bwana Mungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.
Med ham er en kødelig Arm, men med os er Herren vor Gud, som vil hjælpe os og stride i vore Krige; og Folket forlod sig fast paa Ezekias, Judas Konges, Ord.
9 Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akawatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda, na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo, kusema:
Derefter sendte Senakerib, Kongen af Assyrien, sine Tjenere til Jerusalem, medens han laa for Lakis med hele sit Riges Magt, til Ezekias, Judas Konge, og til al Juda, som var i Jerusalem, og lod sige:
10 “Hili ndilo asemalo Senakeribu mfalme wa Ashuru: Je, mmeweka tumaini lenu wapi, hata mnaendelea kukaa katika Yerusalemu, hali mmezungukwa na jeshi?
Saa siger Senakerib, Kongen af Assyrien: Hvorpaa forlade I eder, at I blive i Jerusalem under en Belejring?
11 Hezekia asemapo, ‘Bwana Mungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, naye atawaacha mfe kwa njaa na kiu.
Tilskynder ikke Ezekias eder for at give eder hen til at dø af Hunger og af Tørst og siger: Herren vor Gud skal fri os af Kongen af Assyriens Haand?
12 Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?
Er det ikke Ezekias, som har borttaget hans Høje og hans Altre og sagt til Juda og til Jerusalem: I skulle tilbede for et eneste Alter og derpaa gøre Røgelse?
13 “Je, hamjui yale mimi na baba zangu tuliyoyafanya kwa mataifa yote ya nchi zingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu?
Vide I ikke, hvad jeg og mine Fædre have gjort ved alle Folk i Landene? Kunde vel Hedningernes Guder i Landene fri deres Land fra min Haand?
14 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza ameweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Mungu wenu kuwaokoa mkononi mwangu?
Hvo iblandt alle Guderne hos disse Hedninger, hvilke mine Fædre have bandlyst, var den, som kunde fri sit Folk fra min Haand, saa at eders Gud skulde kunne fri eder fra min Haand?
15 Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye na kuwapotosha namna hii. Msimwamini, kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lolote wala wa ufalme wowote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”
Saa lader nu Ezekias ikke bedrage eder og ikke tilskynde eder paa denne Maade, og tror ham ikke; thi ingen Gud hos noget Folk eller Rige har kunnet fri sit Folk fra min Haand og fra mine Fædres Haand; hvor meget mindre skulde eders Guder fri eder fra min Haand?
16 Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi ya Bwana aliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia.
Tilmed talte hans Tjenere ydermere imod Gud Herren og imod hans Tjener Ezekias.
17 Mfalme pia aliandika barua akimtukana Bwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.”
Han skrev og Breve for at forhaane Herren, Israels Gud, og at tale imod ham, sigende: Ligesom Guderne hos Hedningerne i Landene ikke friede deres Folk fra min Haand, saaledes skal ikke heller Ezekias's Gud fri sit Folk fra min Haand.
18 Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji.
Og de raabte med høj Røst paa jødisk til Jerusalems Folk, som var paa Muren, for at gøre dem frygtagtige og forfærde dem, for at de kunde indtage Staden.
19 Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.
Og de talte om Jerusalems Gud ligesom om Jordens Folks Guder, der ere Menneskens Hænders Gerning.
20 Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili.
Men Kong Ezekias og Esajas, Amoz's Søn, Profeten, bade angaaende denne Sag, og de raabte til Himmelen.
21 Naye Bwana akamtuma malaika ambaye aliangamiza wanajeshi wote, na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akarudi nchini mwake kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua kwa upanga.
Og Herren sendte en Engel, og han tilintetgjorde alle de vældige til Strid og Fyrsterne og de Øverste i Kongen af Assyriens Lejr; og denne drog tilbage til sit Land med sit Ansigts Blusel, og der han gik ind i sin Guds Hus, da fældede de, som vare udkomne af hans Liv, ham der med Sværd.
22 Hivyo Bwana akamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote. Bwana akawastarehesha kila upande.
Saa frelste Herren Ezekias og Indbyggerne i Jerusalem fra Senakeribs, Kongen af Assyriens, Haand og fra alles Haand og beskærmede dem trindt omkring.
23 Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili ya Bwana na zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.
Og mange bragte Gaver til Herren til Jerusalem og dyrebar Skænk til Ezekias, Judas Konge, saa at denne derefter kom til at staa højt i alle Hedningernes Øjne.
24 Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Akamwomba Bwana, ambaye alimjibu na kumpa ishara.
I de samme Dage blev Ezekias dødssyg, og han bad til Herren, og denne talte til ham og gav ham et underfuldt Tegn.
25 Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana ikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu.
Men Ezekias gengældte ikke den Velgerning, som var bevist ham, thi hans Hjerte ophøjede sig; derfor kom en Vrede over ham og over Juda og Jerusalem.
26 Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana haikuja juu yao katika siku za Hezekia.
Dog ydmygede Ezekias sig, efter at hans Hjerte havde ophøjet sig, han og Indbyggerne i Jerusalem; derfor kom Herrens Vrede ikke over dem i Ezekias's Dage.
27 Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani.
Og Ezekias havde saare stor Rigdom og Ære, og han gjorde sig Skatkamre til Sølv og Guld og kostbare Stene og vellugtende Urter og Skjolde og alle Haande kostelige Redskaber
28 Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi.
og Forraadshuse til, hvad der kom ind af Korn og Most og Olie, og Stalde for alle Haande Kvæg og skaffede sig Hjorde til Staldene.
29 Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ngʼombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.
Og han byggede sig Stæder og havde Fæ af smaat og stort Kvæg i Mangfoldighed; thi Gud gav ham saare meget Gods.
30 Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya.
Og denne Ezekias tilstoppede ogsaa det øverste Vandløb fra Gihon og ledede det ned, Vest for Davids Stad; og Ezekias var lykkelig i al sin Gerning.
31 Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumuuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.
Men det skete saa, da der var sendt Tolke til ham fra Fyrsterne i Babel for at spørge om det underfulde Tegn, som var sket i Landet, da forlod Gud ham for at forsøge ham og for at kende alt det, som var i hans Hjerte.
32 Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
Men det øvrige af Ezekias's Handeler og hans fromme Gerninger, se, de Ting ere skrevne i Profeten Esajas's, Amoz's Søns Syn, i Judas og Israels Kongers Bog.
33 Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipofariki. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.
Og Ezekias laa med sine Fædre, og de begrove ham oven for Davids Børns Grave; og det ganske Juda og Jerusalems Indbyggere beviste ham Ære i hans Død, og hans Søn Manasse blev Konge i hans Sted.