< 2 Nyakati 31 >
1 Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.
A kad se sve ovo svrši, svi sinovi Izrailjevi što se naðoše ondje, zaðoše po gradovima Judinijem, i izlomiše likove i isjekoše lugove, i oboriše visine i oltare po svoj zemlji Judinoj i Venijaminovoj i po zemlji Jefremovoj i Manasijinoj, dokle sve ne svršiše; potom se vratiše svi sinovi Izrailjevi svak na svoje našljedstvo, u svoje gradove.
2 Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana.
A Jezekija opet uredi redove sveštenièke i Levitske po redovima njihovijem, svakoga po službi njegovoj, sveštenike i Levite, za žrtve paljenice i zahvalne, da služe, i da slave i hvale Gospoda na vratima okola njegova.
3 Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana.
I odredi dio carski od blaga svojega za žrtve paljenice, što se prinose jutrom i veèerom i za žrtve paljenice što se prinose u subote i na mladine i na praznike, kako je napisano u zakonu Gospodnjem.
4 Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana.
I zapovjedi narodu, Jerusalimljanima, da daju dio sveštenicima i Levitima, da se jaèe drže zakona Gospodnjega.
5 Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu.
A èim se to razglasi, stadoše donositi sinovi Izrailjevi silu prvina od žita i od vina i od ulja i od meda i svakoga roda zemaljskoga; i desetka od svega donosiše vrlo mnogo.
6 Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo.
I sinovi Izrailjevi i Judini koji življahu po gradovima Judinijem, donosiše i oni desetak od goveda i ovaca, i desetak od svetijeh stvari posveæenijeh Gospodu Bogu njihovu, i metaše u gomile.
7 Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba.
Treæega mjeseca poèeše metati u gomile, a sedmoga mjeseca svršiše.
8 Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.
I doðe Jezekija s knezovima, i vidjevši gomile blagosloviše Gospoda i narod njegov Izrailja.
9 Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo,
I Jezekija zapita sveštenike i Levite za gomile.
10 naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”
A Azarija poglavar sveštenièki od doma Sadokova reèe mu: otkad poèeše donositi ove priloge u dom Gospodnji, jedemo i siti smo i pretjeèe mnogo, jer je Gospod blagoslovio svoj narod, te je preteklo ovo mnoštvo.
11 Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika.
Tada zapovjedi Jezekija da se naèine klijeti u domu Gospodnjem; i naèiniše;
12 Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake.
I ondje ostavljahu vjerno priloge i desetke i stvari posveæene; i nad tijem bješe poglavar Honanija Levit i Simej brat mu, drugi do njega.
13 Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.
A Jehilo i Azazija i Nahat i Asailo i Jerimot i Jozavad i Elilo i Ismahija i Mat i Venaja bijahu nastojnici pod rukom Honanije i brata mu Simeja po naredbi cara Jezekije i Azarije starješine u domu Božijem.
14 Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu.
A Korej sin Jemne Levita, vratar na istoku, bijaše nad onijem što se dragovoljno prinošaše Bogu, da bi razdjeljivao prinos Gospodnji i stvari svete nad svetijem.
15 Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.
A pod njim bješe Eden i Minijamin i Isus i Semaja i Amarija i Sehanija po gradovima sveštenièkim, ljudi pouzdani, da razdaju braæi svojoj dijelove, velikomu i malomu,
16 Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao.
Osim muškinja u rodu njihovu od tri godine i više, svakomu koji ulažaše u dom Gospodnji na posao svakidašnji po dužnosti njihovoj u službi njihovoj po redu njihovu,
17 Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao.
I onima koji biše izbrojeni u rodu sveštenièkom po domovima otaca njihovijeh, i Levitima od dvadeset godina i više po službi njihovoj po redovima njihovijem,
18 Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.
I porodici njihovoj, svoj djeci njihovoj, ženama njihovijem, sinovima njihovijem i kæerima njihovijem, svemu mnoštvu; jer se vjerno posvetiše svetinji;
19 Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.
I sinovima Aronovijem sveštenicima u podgraðima gradova njihovijeh, po svijem gradovima, ljudi imenovani davahu dijelove svakome muškarcu izmeðu sveštenika i svakomu roda Levitskoga.
20 Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake.
I tako uèini Jezekija u svoj zemlji Judinoj; i èinjaše što je dobro i pravo i istinito pred Gospodom Bogom njegovijem.
21 Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.
I u svakom poslu koji poèe za službu doma Božijega i u zakonu i u zapovijesti tražeæi Boga svojega, truðaše se svijem srcem svojim, i sreæan bijaše.