< 2 Nyakati 31 >

1 Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.
بعد از پایان عید پِسَح، اسرائیلی‌هایی که برای شرکت در عید به اورشلیم آمده بودند به شهرهای یهودا، بنیامین، افرایم و منسی رفتند و بتکده‌های روی تپه‌ها را ویران کرده، تمام بتها، مذبحها و مجسمه‌های شرم‌آور اشیره را در هم کوبیدند. سپس همگی به خانه‌های خود بازگشتند.
2 Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana.
حِزِقیا دسته‌های کاهنان و لاویان را برحسب نوع خدمتی که داشتند دوباره سر خدمت قرار داد. خدمات ایشان عبارت بودند از: تقدیم قربانیهای سوختنی و قربانیهای سلامتی، رهبری مراسم عبادتی و شکرگزاری و خواندن سرود در خانهٔ خداوند.
3 Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana.
همچنین برای قربانیهای سوختنی صبح و عصر، قربانیهای روزهای شَبّات و جشنهای ماه نو و سایر عیدها که در تورات خداوند مقرر شده بود، پادشاه از اموال خود حیواناتی هدیه کرد.
4 Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana.
علاوه بر این، برای اینکه کاهنان و لاویان بتوانند تمام وقت مشغول انجام وظیفه‌ای باشند که در تورات خدا برای آنها مقرر شده بود، از مردم اورشلیم خواست تا سهم مقرر شدهٔ کاهنان و لاویان را به آنها بدهند.
5 Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu.
به محض صدور فرمان پادشاه، مردم اسرائیل با کمال سخاوتمندی نوبر غله، شراب، روغن زیتون و عسل و نیز ده‌یک تمام محصولات زمین خود را آورده، هدیه کردند.
6 Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo.
تمام کسانی که در یهودا ساکن بودند علاوه بر ده‌یک گله‌ها و رمه‌ها، مقدار زیادی هدایای دیگر آوردند و برای خداوند، خدای خود وقف کردند.
7 Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba.
این کار را از ماه سوم شروع کردند و در ماه هفتم به پایان رساندند.
8 Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.
وقتی حِزِقیا و بزرگان قوم آمدند و این هدایا را دیدند خداوند را شکر و سپاس گفتند و برای قوم اسرائیل برکت طلبیدند.
9 Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo,
حِزِقیا از کاهنان و لاویان دربارهٔ هدایا سؤال کرد،
10 naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”
و عزریا، کاهن اعظم، که از طایفهٔ صادوق بود جواب داد: «از وقتی که مردم شروع کردند به آوردن این هدایای خوراکی به خانهٔ خداوند، ما از آنها خوردیم و سیر شدیم و مقدار زیادی نیز باقی مانده است، زیرا خداوند قوم خود را برکت داده است.»
11 Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika.
حِزِقیا دستور داد که در خانهٔ خداوند انبارهایی بسازند.
12 Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake.
پس از آماده شدن انبارها، تمام مواد خوراکی اهدا شده را در آنجا انبار کردند. مسئولیت نگهداری انبارها به عهدهٔ کننیای لاوی بود و برادرش شمعی نیز او را کمک می‌کرد.
13 Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.
ده لاوی دیگر نیز از طرف حِزِقیای پادشاه و عزریا، کاهن اعظم، تعیین شدند تا زیر نظر این دو برادر خدمت کنند. این لاویان عبارت بودند از: یحی‌ئیل، عزریا، نحت، عسائیل، یریموت، یوزاباد، ایلی‌ئیل، یسمخیا، محت و بنایا.
14 Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu.
قوری (پسر یمنهٔ لاوی) که نگهبان دروازهٔ شرقی بود، مسئول توزیع هدایا در میان کاهنان شد. دستیاران او اینها بودند: عیدن، منیامین، یشوع، شمعیا، امریا و شکنیا. ایشان هدایا را به شهرهای کاهنان بردند و میان گروه‌های مختلف کاهنان تقسیم می‌کردند و سهم پیر و جوان را به طور مساوی می‌دادند.
15 Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.
16 Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao.
در ضمن به خانوادهٔ کاهنان نیز سهمی تعلق می‌گرفت.
17 Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao.
نام کاهنان برحسب طایفه‌هایشان و نام لاویان بیست ساله و بالاتر نیز برحسب وظایفی که در گروه‌های مختلف داشتند، ثبت شده بود.
18 Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.
به خانواده‌های کاهنانی که نامشان ثبت شده بود، به طور مرتب سهمیه‌ای داده می‌شد زیرا این کاهنان خود را وقف خدمت خدا کرده بودند.
19 Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.
افرادی نیز تعیین شدند تا هدایای خوراکی را بین کاهنان نسل هارون که در مزارع اطراف شهرها زندگی می‌کردند و نیز بین کسانی که نامشان در نسب نامهٔ لاویان ثبت شده بود، توزیع کنند.
20 Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake.
به این ترتیب حِزِقیای پادشاه در مورد توزیع هدایا در سراسر یهودا اقدام نمود و آنچه در نظر خداوند، خدایش پسندیده و درست بود بجا آورد.
21 Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.
او با تمام دل و جان آنچه برای خانهٔ خدا لازم بود انجام می‌داد و از شریعت و احکام خدا پیروی می‌نمود و به همین جهت همیشه موفق بود.

< 2 Nyakati 31 >