< 2 Nyakati 31 >
1 Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.
And whanne these thingis weren doon riytfuli, al Israel yede out, that was foundun in the citees of Juda; and thei braken simylacris, and kittiden doun woodis, and wastiden hiy places, and distrieden auteris, not oneli of al Juda and Beniamyn, but also and of Effraym and Manasses, til thei distrieden outirli. And alle the sones of Israel turneden ayen in to her possessiouns and citees.
2 Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana.
Forsothe Ezechie ordeynede cumpenyes of preestis and of dekenes bi her departyngis, ech man in his owne office, that is, as wel of preestis as of dekenes, to brent sacrifices and pesible sacrifices, that thei schulden mynystre, and knowleche, and synge in the yatis of the castels of the Lord.
3 Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana.
Sotheli the part of the kyng was, that of his owne catel brent sacrifice schulde be offrid euere in the morewtid and euentide, also in sabatis, and calendis, and othere solempnytees, as it is writun in the lawe of Moises.
4 Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana.
Also he comaundide to the puple of hem that dwelliden in Jerusalem, to yyue partis to the preestis and dekenes, that thei myyten yyue tent to the lawe of the Lord.
5 Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu.
And whanne this was knowun in the eeris of the multitude, the sones of Israel offriden ful many firste fruytis of wheete, of wyn, of oyle, and of hony; and of alle thingis whiche the erthe bringith forth, thei offriden tithis.
6 Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo.
But also the sones of Israel and of Juda, that dwelliden in the citees of Juda, offriden tithis of oxis and of scheep, and the tithis of holi thingis, whiche thei avowiden to `her Lord God, and thei brouyten alle thingis, and maden ful many heepis.
7 Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba.
In the thridde monethe thei bigunnen to leie the foundementis of the heepis, and in the seuenthe monethe thei filliden tho heepis.
8 Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.
And whanne Ezechie and hise princes hadden entrid, thei siyen the heepis, and blessiden the Lord, and the puple of Israel.
9 Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo,
And Ezechie axide the preestis and dekenes, whi the heepis laien so.
10 naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”
Azarie, the firste preest of the generacioun of Sadoch, answeride to hym, and seide, Sithen the firste fruytis bigunnen to be offrid in the hows of the Lord, we han ete and ben fillid, and ful many thingis ben left; for the Lord hath blessid his puple; sotheli this plentee, which thou seest, is of the relifs.
11 Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika.
Therfor Ezechie comaundide, that thei schulden make redi bernes in the hows of the Lord; and whanne thei hadden do this thing,
12 Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake.
thei brouyten in feithfuly bothe the firste fruytis, and tithis, and what euere thingis thei hadden avowid. Forsothe Chonenye, the dekene, was the souereyn of tho; and Semei his brother was the secounde;
13 Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.
aftir whom Jehiel, and Azarie, and Nabath, and Asahel, and Jerimoth, `and Jozabad, and Helyel, and Jesmahie, and Maath, and Banaie, weren souereyns vndur the hondis of Chonenye and Semei, his brother, bi the comaundement of `Ezechie the kyng, and of Azarie, the bischop of the hows of the Lord, to whiche alle thingis perteyneden.
14 Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu.
But Chore, the sone of Jemnya, dekene and portere of the eest yate, was souereyn of tho thingis that weren offrid bi fre wille to the Lord, and of the firste fruytis, and of thingis halewid in to hooli thingis of the noumbre of hooli thingis;
15 Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.
and vndur his cure weren Eden, and Beniamyn, Jesue, and Semeye, and Amarie, and Sechenye, in the citees of preestis, that thei schulden departe feithfuli to her britheren the partis, to the lesse and the grettere,
16 Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao.
outakun malis fro three yeer and aboue, these thingis to alle that entriden in to the temple of the Lord, and what euer thing bi ech dai was hirid in the seruyce and obseruaunces bi her departyngis.
17 Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao.
To preestis bi meynees, and to dekenes fro `the twentithe yeer and aboue bi her ordris and cumpenyes, and to alle the multitude,
18 Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.
bothe to the wyues and fre children of hem of euer either kynde, metis weren youun feithfuli of these thingis that weren halewid.
19 Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.
But also men of the sones of Aaron weren ordeyned bi the feeldis and subarbis of alle citees, whyche men schulden dele partis to al the male kynde of preestis and dekenes.
20 Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake.
Therfor Ezechie dide alle thingis, whiche we seiden, in al Juda, and he wrouyte that, that was riytful and good and trewe bifor `his Lord God,
21 Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.
in al the religioun of the seruyce of the hows of the Lord, bi the lawe and cerymonyes; and he wolde seke his Lord God in al his herte, and he dide, and hadde prosperite.