< 2 Nyakati 31 >

1 Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.
And just as finished all this they went out all Israel who were found to [the] cities of Judah and they broke the sacred pillars and they cut down the Asherah poles and they pulled down the high places and the altars from all Judah and Benjamin and in Ephraim and Manasseh until finished and they returned all [the] people of Israel each to possession his to cities their.
2 Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana.
And he appointed Hezekiah [the] divisions of the priests and the Levites on divisions their each - according to [the] mouth of service his to the priests and to the Levites for burnt offering and for peace offerings to serve and to give thanks and to praise in [the] gates of [the] camps of Yahweh.
3 Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana.
And [the] portion of the king from own property his [was] for the burnt offerings for [the] burnt offerings of the morning and the evening and the burnt offerings for the sabbaths and for the new moons and for the appointed feasts according to [what] is written in [the] law of Yahweh.
4 Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana.
And he said to the people to [the] inhabitants of Jerusalem to give [the] portion of the priests and the Levites so that they may be strong in [the] law of Yahweh.
5 Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu.
And just as spread the word they multiplied [the] people of Israel [the] first of grain new wine and fresh oil and honey and every produce of [the] field and [the] tithe of everything to abundance they brought.
6 Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo.
And [the] people of Israel and Judah who dwelt in [the] cities of Judah also they a tithe of herd[s] and flock[s] and a tithe of holy things which were consecrated to Yahweh God their they brought and they made heaps heaps.
7 Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba.
In the month third they began the heaps to found and in the month seventh they finished.
8 Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.
And they came Hezekiah and the officials and they saw the heaps and they blessed Yahweh and people his Israel.
9 Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo,
And he enquired Hezekiah to the priests and the Levites on the heaps.
10 naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”
And he said to him Azariah the priest the head of [the] house of Zadok and he said from when began the contribution to bring [the] house of Yahweh we have eaten and we have been satisfied and we have had more than enough to to abundance for Yahweh he has blessed people his and [what] remains the abundance this.
11 Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika.
And he said Hezekiah to prepare rooms in [the] house of Yahweh and they prepared [them].
12 Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake.
And they brought the contribution and the tithe and the holy things in faithfulness and [was] over them an officer (Konaniah *Q(k)*) the Levite and Shimei brother his [was] second in command.
13 Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.
And Jehiel and Azaziah and Nahath and Asahel and Jerimoth and Jozabad and Eliel and Ismachiah and Mahath and Benaiah [were] overseers from [the] hand of (Konaniah *Q(k)*) and Shimei brother his by [the] appointment of Hezekiah the king and Azariah [the] ruler of [the] house of God.
14 Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu.
And Kore [the] son of Imnah the Levite the gatekeeper to the east [was] over [the] freewill offerings of God to distribute [the] contribution of Yahweh and [the] holy things of the holy things.
15 Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.
And [were] on hand his Eden and Miniamin and Jeshua and Shemaiah Amariah and Shecaniah in [the] cities of the priests in faithfulness to distribute to brothers their by divisions as the great as the small.
16 Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao.
Besides recording genealogy they to males from a son of three years and upwards to every [one who] went to [the] house of Yahweh for [the] matter of a day in day its for service their by duties their according to divisions their.
17 Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao.
And [the] genealogical enrolment of the priests to [the] house of ancestors their and the Levites from a son of twenty year[s] and upwards by duties their by divisions their.
18 Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.
And to genealogical enrolment with all little one[s] their wives their and sons their and daughters their to all [the] assembly for in faithfulness their they had consecrated themselves holiness.
19 Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.
And to [the] descendants of Aaron the priests in [the] fields of [the] pasture land of cities their [were] in every city and a city men who they had been designated by names to distribute portions to every male among the priests and to all [the] genealogical enrolment among the Levites.
20 Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake.
And he did like this Hezekiah in all Judah and he did the good and the right and faithfulness before Yahweh God his.
21 Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.
And in every work which he began - in [the] service of [the] house of God and in the law and in the commandment to seek God his with all heart his he did [it] and he succeeded.

< 2 Nyakati 31 >