< 2 Nyakati 30 >

1 Hezekia akatuma ujumbe kuwaita Israeli wote na Yuda, pia akaandika barua kwa Efraimu na Manase, kuwakaribisha ili waje hekaluni mwa Bwana huko Yerusalemu kuadhimisha Pasaka kwa Bwana, Mungu wa Israeli.
Ézéchias envoya des messages à tout Israël et Juda, et écrivit des lettres à Éphraïm et Manassé, pour qu'ils viennent à la maison de l'Éternel à Jérusalem, afin de célébrer la Pâque en l'honneur de l'Éternel, le Dieu d'Israël.
2 Mfalme na maafisa wake pamoja na kusanyiko lote katika Yerusalemu waliamua kuadhimisha Pasaka katika mwezi wa pili.
Car le roi avait pris l'avis de ses princes et de toute l'assemblée de Jérusalem de célébrer la Pâque au second mois.
3 Kwa sababu makuhani hawakuwa wamejitakasa idadi ya kutosha na watu wakawa hawajakusanyika huko Yerusalemu, hawakuwa wameweza kuadhimisha Pasaka kwa wakati wake wa kawaida.
Car ils ne pouvaient pas la célébrer en ce temps-là, parce que les prêtres ne s'étaient pas sanctifiés en nombre suffisant et que le peuple ne s'était pas rassemblé à Jérusalem.
4 Mpango huu ukaonekana wafaa kwa mfalme na kusanyiko lote.
La chose était juste aux yeux du roi et de toute l'assemblée.
5 Wakaamua kupeleka tangazo Israeli kote, kuanzia Beer-Sheba hadi Dani, wakiwaita watu waje Yerusalemu kuadhimisha Pasaka ya Bwana, Mungu wa Israeli. Ilikuwa haijaadhimishwa na idadi kubwa ya watu kama hiyo kufuatana na yale yaliyokuwa yameandikwa.
Et ils établirent un décret pour proclamer dans tout Israël, depuis Beersheba jusqu'à Dan, qu'il fallait venir célébrer la Pâque en l'honneur de Yahvé, le Dieu d'Israël, à Jérusalem, car ils ne l'avaient pas célébrée en grand nombre comme il est écrit.
6 Kwa amri ya mfalme, matarishi wakapita katika Israeli na Yuda kote wakiwa na barua kutoka kwa mfalme na kutoka kwa maafisa wake zikisema: “Watu wa Israeli, mrudieni Bwana, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Israeli, ili naye awarudie ninyi mliosalia, mlionusurika kutoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru.
Et les courriers portèrent les lettres du roi et de ses princes dans tout Israël et Juda, selon l'ordre du roi: « Enfants d'Israël, revenez à l'Éternel, le Dieu d'Abraham, d'Isaac et d'Israël, afin qu'il revienne au reste d'entre vous qui s'est échappé de la main des rois d'Assyrie.
7 Msiwe kama baba zenu na ndugu zenu, ambao hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Mungu wa baba zao, hivyo akawafanya kitu cha kushangaza kama mnavyoona.
Ne soyez pas comme vos pères et comme vos frères, qui ont péché contre Yahvé, le Dieu de leurs pères, et qui les ont livrés à la désolation, comme vous le voyez.
8 Msiwe na shingo ngumu, kama baba zenu walivyokuwa, bali nyenyekeeni kwa Bwana. Njooni mahali patakatifu, alipopatakasa milele. Mtumikieni Bwana Mungu wenu, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nanyi.
Maintenant, n'ayez pas la nuque raide, comme vos pères, mais soumettez-vous à l'Éternel, entrez dans son sanctuaire, qu'il a sanctifié pour toujours, et servez l'Éternel, votre Dieu, afin que son ardente colère se détourne de vous.
9 Kama mkimrudia Bwana ndipo wale ndugu zenu waliotekwa pamoja na watoto wenu watakapoonewa huruma na wale waliowateka na kuwaachia warudi katika nchi hii, kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni mwenye neema na huruma, hatageuzia uso wake mbali nanyi kama ninyi mkimrudia yeye.”
Car si vous revenez à Yahvé, vos frères et vos enfants auront pitié de ceux qui les ont emmenés en captivité, et ils reviendront dans ce pays, car Yahvé votre Dieu est compatissant et miséricordieux, et il ne détournera pas sa face de vous si vous revenez à lui. »
10 Matarishi wakaenda mji hadi mji katika Efraimu na Manase, wakafika mpaka Zabuloni, lakini watu wakawadharau na kuwadhihaki.
Les coursiers passèrent donc de ville en ville dans le pays d'Ephraïm et de Manassé, jusqu'à Zabulon, mais les gens se moquaient d'eux et les bafouaient.
11 Lakini, baadhi ya watu wa Asheri, Manase na Zabuloni, wakajinyenyekeza wakaja Yerusalemu.
Néanmoins, quelques hommes d'Asher, de Manassé et de Zabulon s'humilièrent et vinrent à Jérusalem.
12 Pia katika Yuda mkono wa Mungu ulikuwa juu ya watu kuwapa umoja katika kutenda yale ambayo mfalme na maafisa wake waliwaamuru, kulingana na neno la Bwana.
Et la main de Dieu vint sur Juda pour leur donner un seul cœur, afin qu'ils mettent en pratique les ordres du roi et des princes, selon la parole de Yahvé.
13 Basi umati mkubwa wa watu ukakusanyika huko Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu katika mwezi wa pili.
Un peuple nombreux s'assembla à Jérusalem pour célébrer la fête des pains sans levain au deuxième mois, une très grande assemblée.
14 Wakajitia kazini kuyaondoa yale madhabahu yaliyokuwa huko Yerusalemu, wakayaondoa pia yale madhabahu ya kufukizia uvumba kwa miungu na kuyatupa Bonde la Kidroni.
Ils se levèrent et enlevèrent les autels qui étaient à Jérusalem, ils enlevèrent tous les autels à encens et les jetèrent dans le torrent de Cédron.
15 Kisha wakamchinja mwana-kondoo wa Pasaka katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Makuhani na Walawi waliona aibu, wakajitakasa na kuleta sadaka za kuteketezwa katika Hekalu la Bwana.
Puis ils immolèrent la Pâque le quatorzième jour du deuxième mois. Les prêtres et les lévites eurent honte, se purifièrent et apportèrent des holocaustes dans la maison de Yahvé.
16 Kisha wakachukua nafasi zao za kawaida kama ilivyoelezwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu. Makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa na Walawi.
Ils se tinrent à leur place selon leur ordre, conformément à la loi de Moïse, homme de Dieu. Les prêtres aspergeaient le sang qu'ils avaient reçu de la main des Lévites.
17 Kwa kuwa wengi waliokuwa katika lile kusanyiko walikuwa hawajajitakasa, iliwapasa Walawi wachinje wana-kondoo wengine wa Pasaka kwa ajili ya wale watu ambao hawakuwa safi, kwa kufuata taratibu za ibada ili kuwatakasa kwa Bwana.
Car il y avait dans l'assemblée beaucoup de gens qui ne s'étaient pas sanctifiés; c'est pourquoi les Lévites étaient chargés d'immoler la Pâque pour tous ceux qui n'étaient pas purs, afin de les sanctifier pour Yahvé.
18 Ingawa watu wengi miongoni mwa wale waliotoka Efraimu, Manase, Isakari na Zabuloni walikuwa hawajajitakasa, hata hivyo walikula Pasaka kinyume na ilivyoandikwa. Lakini Hezekia akawaombea, akisema, “Bwana, ambaye ni mwema na amsamehe kila mmoja
En effet, une grande partie du peuple, beaucoup d'Ephraïm, de Manassé, d'Issacar et de Zabulon ne s'étaient pas purifiés, et ils mangeaient la Pâque autrement qu'il est écrit. Car Ézéchias avait prié pour eux en disant: « Que le bon Yahvé pardonne à tous ceux
19 ambaye anauelekeza moyo wake kumtafuta Mungu, Bwana, Mungu wa baba zake, hata kama yeye si safi kulingana na sheria za mahali patakatifu.”
qui mettent leur cœur à chercher Dieu, Yahvé, le Dieu de leurs pères, même s'ils ne sont pas purs selon la purification du sanctuaire. »
20 Naye Bwana akamsikia Hezekia akawaponya watu.
Yahvé écouta Ézéchias et guérit le peuple.
21 Waisraeli waliokuwa Yerusalemu wakaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa muda wa siku saba, nao Walawi na makuhani walikuwa wakiimba kila siku, wakiwa na ala za uimbaji za kumsifu Bwana.
Les Israélites qui se trouvaient à Jérusalem célébrèrent la fête des pains sans levain pendant sept jours, avec une grande joie. Les lévites et les prêtres louaient Yahvé jour après jour, en chantant à Yahvé avec des instruments puissants.
22 Hezekia akazungumza akiwatia moyo Walawi wote, ambao walionyesha ustadi katika kumtumikia Bwana. Hivyo watu wakala chakula cha sikukuu kwa siku saba, wakitoa sadaka za amani na kumshukuru Bwana, Mungu wa baba zao.
Ézéchias adressa des paroles d'encouragement à tous les Lévites qui avaient de l'intelligence dans le service de Yahvé. Ils mangèrent pendant toute la durée de la fête, pendant les sept jours, en offrant des sacrifices d'actions de grâces et en se confessant à Yahvé, le Dieu de leurs pères.
23 Kisha kusanyiko lote likakubali kuendelea na sikukuu kwa siku saba zaidi, kwa hiyo kwa siku saba nyingine wakaendelea kuiadhimisha kwa furaha.
Toute l'assemblée prit l'avis de célébrer sept autres jours, et ils célébrèrent sept autres jours avec joie.
24 Hezekia, mfalme wa Yuda akatoa mafahali 1,000, kondoo na mbuzi 7,000 kwa ajili ya kusanyiko, nao maafisa wakatoa mafahali 1,000 pamoja na kondoo na mbuzi 10,000. Idadi kubwa ya makuhani wakajiweka wakfu.
Car Ézéchias, roi de Juda, donna à l'assemblée, en offrande, mille taureaux et sept mille brebis; les princes donnèrent à l'assemblée mille taureaux et dix mille brebis, et un grand nombre de prêtres se sanctifièrent.
25 Kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi na lile kusanyiko lote lililotoka Israeli, pamoja na wale wageni waliotoka Israeli na wale walioishi katika Yuda wakafurahi.
Toute l'assemblée de Juda, avec les prêtres et les lévites, toute l'assemblée venue d'Israël, et les étrangers sortis du pays d'Israël et qui habitaient en Juda, se réjouirent.
26 Kulikuwa na furaha kubwa katika Yerusalemu, kwa sababu tangu siku za Mfalme Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli halijakuwepo jambo kama hili katika Yerusalemu.
Il y eut donc une grande joie à Jérusalem, car depuis le temps de Salomon, fils de David, roi d'Israël, il n'y avait rien eu de tel à Jérusalem.
27 Ndipo makuhani na Walawi wakasimama wakawabariki watu, naye Mungu akawasikia, kwa sababu maombi yao yalifika mbinguni, makao yake matakatifu.
Alors les prêtres lévitiques se levèrent et bénirent le peuple. Leur voix a été entendue, et leur prière est montée jusqu'à sa sainte demeure, jusqu'aux cieux.

< 2 Nyakati 30 >