< 2 Nyakati 30 >
1 Hezekia akatuma ujumbe kuwaita Israeli wote na Yuda, pia akaandika barua kwa Efraimu na Manase, kuwakaribisha ili waje hekaluni mwa Bwana huko Yerusalemu kuadhimisha Pasaka kwa Bwana, Mungu wa Israeli.
The king and his officials and all the other people who had gathered in Jerusalem wanted to celebrate the Passover Festival. But they were not able to celebrate it at the usual time, because many of the priests had still not performed the rituals to purify themselves; therefore they were not allowed to do serve in the festival. Also, everyone had still not come to Jerusalem [to celebrate the Passover]. So they decided to celebrate it one month later than usual.
2 Mfalme na maafisa wake pamoja na kusanyiko lote katika Yerusalemu waliamua kuadhimisha Pasaka katika mwezi wa pili.
3 Kwa sababu makuhani hawakuwa wamejitakasa idadi ya kutosha na watu wakawa hawajakusanyika huko Yerusalemu, hawakuwa wameweza kuadhimisha Pasaka kwa wakati wake wa kawaida.
4 Mpango huu ukaonekana wafaa kwa mfalme na kusanyiko lote.
The king and all the other people who had gathered thought that was a good plan.
5 Wakaamua kupeleka tangazo Israeli kote, kuanzia Beer-Sheba hadi Dani, wakiwaita watu waje Yerusalemu kuadhimisha Pasaka ya Bwana, Mungu wa Israeli. Ilikuwa haijaadhimishwa na idadi kubwa ya watu kama hiyo kufuatana na yale yaliyokuwa yameandikwa.
So they decided to send messages to all the towns in Judah and in Israel, from Beersheba [in the far south] to Dan [in the far north], including towns in the tribes of Ephraim and Manasseh, to invite people to come to the temple in Jerusalem to celebrate the Passover [Festival] to [honor] Yahweh, the God whom the Israeli people [worshiped/belonged to]. Many of the people had not previously celebrated that festival, even though it had been written [in the laws of Moses that they should do that].
6 Kwa amri ya mfalme, matarishi wakapita katika Israeli na Yuda kote wakiwa na barua kutoka kwa mfalme na kutoka kwa maafisa wake zikisema: “Watu wa Israeli, mrudieni Bwana, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Israeli, ili naye awarudie ninyi mliosalia, mlionusurika kutoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru.
Obeying what the king commanded, messengers went throughout Judah and Israel, taking messages that had been written by the king and his officials. This is what they wrote: “You Israeli people, you who survived after being slaves of the kings of Assyria, return to Yahweh, the God whom [our great ancestors] Abraham, Isaac, and Jacob [worshiped/belonged to], in order that he may return to you. Your fathers and brothers did not faithfully obey Yahweh, the God whom our ancestors [worshiped].
7 Msiwe kama baba zenu na ndugu zenu, ambao hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Mungu wa baba zao, hivyo akawafanya kitu cha kushangaza kama mnavyoona.
Do not act like they did, because what they did caused other people to become disgusted with them.
8 Msiwe na shingo ngumu, kama baba zenu walivyokuwa, bali nyenyekeeni kwa Bwana. Njooni mahali patakatifu, alipopatakasa milele. Mtumikieni Bwana Mungu wenu, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nanyi.
Do not be stubborn as our ancestors were. Do what Yahweh desires. Come [to Jerusalem] to the temple, which he has set apart forever. Do what pleases Yahweh our God, in order that he will no longer be angry with you.
9 Kama mkimrudia Bwana ndipo wale ndugu zenu waliotekwa pamoja na watoto wenu watakapoonewa huruma na wale waliowateka na kuwaachia warudi katika nchi hii, kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni mwenye neema na huruma, hatageuzia uso wake mbali nanyi kama ninyi mkimrudia yeye.”
If you return to Yahweh, the people who have captured our brothers [and sisters] and our children will be kind to them, and allow them to return to this land. Do not forget that Yahweh our God is kind and merciful. If you return to him, he will no longer reject you.”
10 Matarishi wakaenda mji hadi mji katika Efraimu na Manase, wakafika mpaka Zabuloni, lakini watu wakawadharau na kuwadhihaki.
The messengers went to all the towns in the tribes of Ephraim and Manasseh, as far [north] as the tribe of Zebulun, [and gave them this message, ] but most of the people there scorned them and ridiculed them.
11 Lakini, baadhi ya watu wa Asheri, Manase na Zabuloni, wakajinyenyekeza wakaja Yerusalemu.
But some of the people of [the tribes of] Asher, Manasseh, and Zebulun humbled themselves and went to Jerusalem.
12 Pia katika Yuda mkono wa Mungu ulikuwa juu ya watu kuwapa umoja katika kutenda yale ambayo mfalme na maafisa wake waliwaamuru, kulingana na neno la Bwana.
Also in Judah God motivated the people to be united in wanting to do what Yahweh wanted them to do, which is what the king and his officials had told them to do in the message that they sent.
13 Basi umati mkubwa wa watu ukakusanyika huko Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu katika mwezi wa pili.
So a huge crowd of people gathered in Jerusalem in May, to celebrate the Festival of Eating Unleavened Bread.
14 Wakajitia kazini kuyaondoa yale madhabahu yaliyokuwa huko Yerusalemu, wakayaondoa pia yale madhabahu ya kufukizia uvumba kwa miungu na kuyatupa Bonde la Kidroni.
They removed the altars [of Baal] in Jerusalem and took away the altars for burning incense [to honor other gods, and burned them] in Kidron Valley.
15 Kisha wakamchinja mwana-kondoo wa Pasaka katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Makuhani na Walawi waliona aibu, wakajitakasa na kuleta sadaka za kuteketezwa katika Hekalu la Bwana.
They slaughtered the Passover lambs on the fourteenth day of that month. Some of the priests and the other descendants of Levi were ashamed [because they had not performed the rituals to cause them to be acceptable to work for Yahweh]. So they performed those rituals, and brought to the temple animals to be completely burned [on the altar].
16 Kisha wakachukua nafasi zao za kawaida kama ilivyoelezwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu. Makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa na Walawi.
Then they stood at the places where Moses had written in his laws that they should stand. Then the descendants of Levi gave to the priests [bowls containing blood of the animals that were being sacrificed], and the priests sprinkled [the altar] with some of the blood.
17 Kwa kuwa wengi waliokuwa katika lile kusanyiko walikuwa hawajajitakasa, iliwapasa Walawi wachinje wana-kondoo wengine wa Pasaka kwa ajili ya wale watu ambao hawakuwa safi, kwa kufuata taratibu za ibada ili kuwatakasa kwa Bwana.
Many people in the crowd had not purified themselves, and therefore they were not able to kill the lambs [and dedicate them] to Yahweh. So it was necessary for the descendants of Levi to kill the lambs for them.
18 Ingawa watu wengi miongoni mwa wale waliotoka Efraimu, Manase, Isakari na Zabuloni walikuwa hawajajitakasa, hata hivyo walikula Pasaka kinyume na ilivyoandikwa. Lakini Hezekia akawaombea, akisema, “Bwana, ambaye ni mwema na amsamehe kila mmoja
Although most of the people who had come from [the tribes of] Ephraim, Manasseh, and Issachar had not purified themselves, they ate the food of the Passover Festival anyway, ignoring the rules written [by Moses]. But Hezekiah prayed for them, saying “Yahweh, you always do what is good; I pray that you will forgive everyone
19 ambaye anauelekeza moyo wake kumtafuta Mungu, Bwana, Mungu wa baba zake, hata kama yeye si safi kulingana na sheria za mahali patakatifu.”
who sincerely wants to honor you, the God whom our ancestors [worshiped], even if they have not purified themselves by obeying the sacred laws that you gave to us.”
20 Naye Bwana akamsikia Hezekia akawaponya watu.
And Yahweh heard what Hezekiah prayed; he forgave the people, [and did not punish them].
21 Waisraeli waliokuwa Yerusalemu wakaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa muda wa siku saba, nao Walawi na makuhani walikuwa wakiimba kila siku, wakiwa na ala za uimbaji za kumsifu Bwana.
The Israeli people who were there in Jerusalem celebrated the Festival of Eating Unleavened Bread for seven days. They rejoiced greatly as they celebrated, while the priests and other descendants of Levi sang to Yahweh every day, and played musical instruments to [praise] God.
22 Hezekia akazungumza akiwatia moyo Walawi wote, ambao walionyesha ustadi katika kumtumikia Bwana. Hivyo watu wakala chakula cha sikukuu kwa siku saba, wakitoa sadaka za amani na kumshukuru Bwana, Mungu wa baba zao.
Hezekiah thanked all the descendants of Levi for doing this work for Yahweh, and for very skillfully leading the people who were worshiping. For those seven days the people ate the Passover food and brought offerings to maintain fellowship with Yahweh and praised Yahweh, the God whom their ancestors [belonged to/had worshiped].
23 Kisha kusanyiko lote likakubali kuendelea na sikukuu kwa siku saba zaidi, kwa hiyo kwa siku saba nyingine wakaendelea kuiadhimisha kwa furaha.
Then the whole group decided to celebrate for seven more days, so they did: They celebrated joyfully for seven more days.
24 Hezekia, mfalme wa Yuda akatoa mafahali 1,000, kondoo na mbuzi 7,000 kwa ajili ya kusanyiko, nao maafisa wakatoa mafahali 1,000 pamoja na kondoo na mbuzi 10,000. Idadi kubwa ya makuhani wakajiweka wakfu.
King Hezekiah provided 1,000 bulls and 7,000 sheep to be slaughtered for the people [to eat during the festival], and the officials also gave them 1,000 bulls and 10,000 sheep and goats. Many priests consecrated themselves.
25 Kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi na lile kusanyiko lote lililotoka Israeli, pamoja na wale wageni waliotoka Israeli na wale walioishi katika Yuda wakafurahi.
All the people of Judah rejoiced, including the priests and other descendants of Levi and all the people from Israel who had come, and including some from other countries who were living in Israel and some from other countries who were living in Judah.
26 Kulikuwa na furaha kubwa katika Yerusalemu, kwa sababu tangu siku za Mfalme Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli halijakuwepo jambo kama hili katika Yerusalemu.
Everyone in Jerusalem was very joyful, because nothing like this had happened in Jerusalem since the time when David’s son Solomon was the king of Israel.
27 Ndipo makuhani na Walawi wakasimama wakawabariki watu, naye Mungu akawasikia, kwa sababu maombi yao yalifika mbinguni, makao yake matakatifu.
The priests and the other descendants of Levi stood up to bless the people, and God heard them in heaven, the holy place where he lives.