< 2 Nyakati 30 >
1 Hezekia akatuma ujumbe kuwaita Israeli wote na Yuda, pia akaandika barua kwa Efraimu na Manase, kuwakaribisha ili waje hekaluni mwa Bwana huko Yerusalemu kuadhimisha Pasaka kwa Bwana, Mungu wa Israeli.
Then sent Hezekiah unto all Israel and Judah, moreover also, letters, wrote he unto Ephraim and Manasseh, that they should come unto the house of Yahweh, in Jerusalem, —to keep a passover unto Yahweh, God of Israel.
2 Mfalme na maafisa wake pamoja na kusanyiko lote katika Yerusalemu waliamua kuadhimisha Pasaka katika mwezi wa pili.
Yea, the king and his rulers and all the convocation in Jerusalem, had taken counsel, —to keep the passover in the second month.
3 Kwa sababu makuhani hawakuwa wamejitakasa idadi ya kutosha na watu wakawa hawajakusanyika huko Yerusalemu, hawakuwa wameweza kuadhimisha Pasaka kwa wakati wake wa kawaida.
For they were unable to keep it at that time, —because, the priests, had not hallowed themselves in sufficient numbers, and, the people, had not gathered themselves unto Jerusalem.
4 Mpango huu ukaonekana wafaa kwa mfalme na kusanyiko lote.
And the thing was right, in the eyes of the king, —and in the eyes of all the convocation.
5 Wakaamua kupeleka tangazo Israeli kote, kuanzia Beer-Sheba hadi Dani, wakiwaita watu waje Yerusalemu kuadhimisha Pasaka ya Bwana, Mungu wa Israeli. Ilikuwa haijaadhimishwa na idadi kubwa ya watu kama hiyo kufuatana na yale yaliyokuwa yameandikwa.
So they established a decree, to make proclamation throughout all Israel, from Beer-sheba even unto Dan, that they should come in to keep a passover unto Yahweh the God of Israel, in Jerusalem, —for, not for a long time, had they kept it as written.
6 Kwa amri ya mfalme, matarishi wakapita katika Israeli na Yuda kote wakiwa na barua kutoka kwa mfalme na kutoka kwa maafisa wake zikisema: “Watu wa Israeli, mrudieni Bwana, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Israeli, ili naye awarudie ninyi mliosalia, mlionusurika kutoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru.
The runners, therefore, went with letters from the hand of the king and his rulers, throughout all Israel and Judah, and according to the commandment of the king, saying, —Ye sons of Israel, return ye unto Yahweh, God of Abraham, Isaac and Israel, and he will return unto the remnant, that which is left to you, out of the hand of the kings of Assyria.
7 Msiwe kama baba zenu na ndugu zenu, ambao hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Mungu wa baba zao, hivyo akawafanya kitu cha kushangaza kama mnavyoona.
And be not ye like your fathers, or like your brethren, who acted unfaithfully with Yahweh, God of your fathers, —who therefore delivered them up for an astonishment, as, ye yourselves, can see.
8 Msiwe na shingo ngumu, kama baba zenu walivyokuwa, bali nyenyekeeni kwa Bwana. Njooni mahali patakatifu, alipopatakasa milele. Mtumikieni Bwana Mungu wenu, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nanyi.
Now, do not stiffen your neck, like your fathers, —stretch forth the hand unto Yahweh, and enter into his sanctuary which he hath hallowed unto times age-abiding, and serve Yahweh your God, that he may turn from you the glow of his anger.
9 Kama mkimrudia Bwana ndipo wale ndugu zenu waliotekwa pamoja na watoto wenu watakapoonewa huruma na wale waliowateka na kuwaachia warudi katika nchi hii, kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni mwenye neema na huruma, hatageuzia uso wake mbali nanyi kama ninyi mkimrudia yeye.”
For, by your returning unto Yahweh, your brethren and your children, shall find compassion before their captors, so as to return unto this land. For, gracious and compassionate, is Yahweh your God, and will not turn away his face from you, if ye will return unto him.
10 Matarishi wakaenda mji hadi mji katika Efraimu na Manase, wakafika mpaka Zabuloni, lakini watu wakawadharau na kuwadhihaki.
So the runners were passing from city to city throughout the land of Ephraim and Manasseh, even unto Zebulun, —but they were laughing them to scorn, and mocking them.
11 Lakini, baadhi ya watu wa Asheri, Manase na Zabuloni, wakajinyenyekeza wakaja Yerusalemu.
Howbeit, some, out of Asher and Manasseh and out of Zebulun, humbled themselves, and came to Jerusalem.
12 Pia katika Yuda mkono wa Mungu ulikuwa juu ya watu kuwapa umoja katika kutenda yale ambayo mfalme na maafisa wake waliwaamuru, kulingana na neno la Bwana.
Also, upon Judah, came the hand of God, to give them one heart, —to keep the commandment of the king and the rulers, as the word of Yahweh.
13 Basi umati mkubwa wa watu ukakusanyika huko Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu katika mwezi wa pili.
And there gathered themselves unto Jerusalem much people, to keep the festival of unleavened cakes, in the second month, —an exceeding large convocation.
14 Wakajitia kazini kuyaondoa yale madhabahu yaliyokuwa huko Yerusalemu, wakayaondoa pia yale madhabahu ya kufukizia uvumba kwa miungu na kuyatupa Bonde la Kidroni.
Then rose they up, and removed the altars, which were in Jerusalem, -and, all the censers, removed they, and cast them into the Kidron ravine.
15 Kisha wakamchinja mwana-kondoo wa Pasaka katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Makuhani na Walawi waliona aibu, wakajitakasa na kuleta sadaka za kuteketezwa katika Hekalu la Bwana.
Then slaughtered they the passover, on the fourteenth of the second month, —and, the priests and the Levites, were put to shame, and hallowed themselves, and brought in the ascending-sacrifices of the house of Yahweh.
16 Kisha wakachukua nafasi zao za kawaida kama ilivyoelezwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu. Makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa na Walawi.
And they stood in their place, according to their regulation, according to the law of Moses the man of God, —the priests, dashing the blood, [which they received] at the hand of the Levites.
17 Kwa kuwa wengi waliokuwa katika lile kusanyiko walikuwa hawajajitakasa, iliwapasa Walawi wachinje wana-kondoo wengine wa Pasaka kwa ajili ya wale watu ambao hawakuwa safi, kwa kufuata taratibu za ibada ili kuwatakasa kwa Bwana.
For there were many in the convocation, who had not hallowed themselves, —but, the Levites, were over the slaughtering of the passover-lambs, for every one who was, not pure, to hallow him unto Yahweh.
18 Ingawa watu wengi miongoni mwa wale waliotoka Efraimu, Manase, Isakari na Zabuloni walikuwa hawajajitakasa, hata hivyo walikula Pasaka kinyume na ilivyoandikwa. Lakini Hezekia akawaombea, akisema, “Bwana, ambaye ni mwema na amsamehe kila mmoja
For, the multitude of the people, many out of Ephraim and Manasseh, Issachar and Zebulun, had not purified themselves, for they did eat the passover, otherwise than as was written, —for Hezekiah prayed for them, saying, May Yahweh the Good, put a propitiatory-covering about
19 ambaye anauelekeza moyo wake kumtafuta Mungu, Bwana, Mungu wa baba zake, hata kama yeye si safi kulingana na sheria za mahali patakatifu.”
every one who hath prepared, his heart, to seek God, even Yahweh, God of his fathers, —though not according to the purification of the sanctuary!
20 Naye Bwana akamsikia Hezekia akawaponya watu.
And Yahweh hearkened unto Hezekiah, and healed the people.
21 Waisraeli waliokuwa Yerusalemu wakaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa muda wa siku saba, nao Walawi na makuhani walikuwa wakiimba kila siku, wakiwa na ala za uimbaji za kumsifu Bwana.
And so the sons of Israel who were found in Jerusalem kept the festival of unleavened cakes seven days, with great rejoicing, —and the Levites and the priests, were offering praise unto Yahweh day by day, with loud instruments, unto Yahweh.
22 Hezekia akazungumza akiwatia moyo Walawi wote, ambao walionyesha ustadi katika kumtumikia Bwana. Hivyo watu wakala chakula cha sikukuu kwa siku saba, wakitoa sadaka za amani na kumshukuru Bwana, Mungu wa baba zao.
And Hezekiah spake unto the heart of all the Levites who were giving good instruction respecting Yahweh, —and they did eat the appointed feast seven days, sacrificing the peace-offerings, and offering praise unto Yahweh, God of their fathers.
23 Kisha kusanyiko lote likakubali kuendelea na sikukuu kwa siku saba zaidi, kwa hiyo kwa siku saba nyingine wakaendelea kuiadhimisha kwa furaha.
Then all the convocation took counsel, to keep seven days more, —and they kept seven days, with rejoicing.
24 Hezekia, mfalme wa Yuda akatoa mafahali 1,000, kondoo na mbuzi 7,000 kwa ajili ya kusanyiko, nao maafisa wakatoa mafahali 1,000 pamoja na kondoo na mbuzi 10,000. Idadi kubwa ya makuhani wakajiweka wakfu.
For, Hezekiah king of Judah, presented to the convocation, a thousand bullocks and seven thousand sheep, and, the rulers, presented to the convocation, a thousand bullocks and ten thousand sheep, -and, priests in great numbers, hallowed themselves.
25 Kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi na lile kusanyiko lote lililotoka Israeli, pamoja na wale wageni waliotoka Israeli na wale walioishi katika Yuda wakafurahi.
So all the convocation of Judah, and the priests and the Levites, and all the convocation that came in out of Israel, rejoiced, —also the sojourners who were coming in out of the land of Israel, and the dwellers in Judah.
26 Kulikuwa na furaha kubwa katika Yerusalemu, kwa sababu tangu siku za Mfalme Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli halijakuwepo jambo kama hili katika Yerusalemu.
Thus was there great rejoicing, in Jerusalem, —for, since the days of Solomon son of David king of Israel, there had not been the like of this, in Jerusalem.
27 Ndipo makuhani na Walawi wakasimama wakawabariki watu, naye Mungu akawasikia, kwa sababu maombi yao yalifika mbinguni, makao yake matakatifu.
Then rose up the priests the Levites, and blessed the people, and there was a hearkening unto their voice, —and their prayer entered into his holy dwelling-place, even into the heavens.