< 2 Nyakati 30 >

1 Hezekia akatuma ujumbe kuwaita Israeli wote na Yuda, pia akaandika barua kwa Efraimu na Manase, kuwakaribisha ili waje hekaluni mwa Bwana huko Yerusalemu kuadhimisha Pasaka kwa Bwana, Mungu wa Israeli.
And Hezekiah sends to all Israel and Judah, and he has also written letters to Ephraim and Manasseh, [to cause them] to come to the house of YHWH in Jerusalem, to make a Passover to YHWH, God of Israel.
2 Mfalme na maafisa wake pamoja na kusanyiko lote katika Yerusalemu waliamua kuadhimisha Pasaka katika mwezi wa pili.
And the king takes counsel, and his heads, and all the assembly in Jerusalem, to make the Passover in the second month,
3 Kwa sababu makuhani hawakuwa wamejitakasa idadi ya kutosha na watu wakawa hawajakusanyika huko Yerusalemu, hawakuwa wameweza kuadhimisha Pasaka kwa wakati wake wa kawaida.
for they have not been able to make it at that time, for the priests have not sanctified themselves sufficiently, and the people have not been gathered to Jerusalem.
4 Mpango huu ukaonekana wafaa kwa mfalme na kusanyiko lote.
And the thing is right in the eyes of the king, and in the eyes of all the assembly,
5 Wakaamua kupeleka tangazo Israeli kote, kuanzia Beer-Sheba hadi Dani, wakiwaita watu waje Yerusalemu kuadhimisha Pasaka ya Bwana, Mungu wa Israeli. Ilikuwa haijaadhimishwa na idadi kubwa ya watu kama hiyo kufuatana na yale yaliyokuwa yameandikwa.
and they establish the thing, to cause an intimation to pass over into all Israel, from Beer-Sheba even to Dan, to come to make a Passover to YHWH, God of Israel, in Jerusalem; for they had not done as it is written for a long time.
6 Kwa amri ya mfalme, matarishi wakapita katika Israeli na Yuda kote wakiwa na barua kutoka kwa mfalme na kutoka kwa maafisa wake zikisema: “Watu wa Israeli, mrudieni Bwana, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Israeli, ili naye awarudie ninyi mliosalia, mlionusurika kutoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru.
And the runners go with letters from the hand of the king and his heads into all Israel and Judah, even according to the command of the king, saying, “O sons of Israel, turn back to YHWH, God of Abraham, Isaac, and Israel, and He turns back to the escaped part that is left of you from the hand of the kings of Asshur;
7 Msiwe kama baba zenu na ndugu zenu, ambao hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Mungu wa baba zao, hivyo akawafanya kitu cha kushangaza kama mnavyoona.
and do not be like your fathers and like your brothers, who trespassed against YHWH, God of their fathers, and He gives them to desolation, as you see.
8 Msiwe na shingo ngumu, kama baba zenu walivyokuwa, bali nyenyekeeni kwa Bwana. Njooni mahali patakatifu, alipopatakasa milele. Mtumikieni Bwana Mungu wenu, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nanyi.
Now do not harden your neck like your fathers, give a hand to YHWH, and come into His sanctuary that He has sanctified for all time, and serve your God YHWH, and the fierceness of His anger turns back from you;
9 Kama mkimrudia Bwana ndipo wale ndugu zenu waliotekwa pamoja na watoto wenu watakapoonewa huruma na wale waliowateka na kuwaachia warudi katika nchi hii, kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni mwenye neema na huruma, hatageuzia uso wake mbali nanyi kama ninyi mkimrudia yeye.”
for in your turning back to YHWH, your brothers and your sons have mercies before their captors, even to return to this land, for your God YHWH [is] gracious and merciful, and He does not turn aside the face from you if you turn back to Him.”
10 Matarishi wakaenda mji hadi mji katika Efraimu na Manase, wakafika mpaka Zabuloni, lakini watu wakawadharau na kuwadhihaki.
And the runners are passing over from city to city in the land of Ephraim and Manasseh, even to Zebulun, but they are laughing at them and mocking at them,
11 Lakini, baadhi ya watu wa Asheri, Manase na Zabuloni, wakajinyenyekeza wakaja Yerusalemu.
only, certain from Asher, and Manasseh, and from Zebulun, have been humbled, and come to Jerusalem.
12 Pia katika Yuda mkono wa Mungu ulikuwa juu ya watu kuwapa umoja katika kutenda yale ambayo mfalme na maafisa wake waliwaamuru, kulingana na neno la Bwana.
Also, in Judah the hand of God has been to give one heart to them to do the command of the king and of the heads in the matter of YHWH;
13 Basi umati mkubwa wa watu ukakusanyika huko Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu katika mwezi wa pili.
and many people are gathered to Jerusalem to make the Celebration of Unleavened Things in the second month—a mighty assembly for multitude.
14 Wakajitia kazini kuyaondoa yale madhabahu yaliyokuwa huko Yerusalemu, wakayaondoa pia yale madhabahu ya kufukizia uvumba kwa miungu na kuyatupa Bonde la Kidroni.
And they arise and turn aside the altars that [are] in Jerusalem, and they have turned aside all the incense altars, and cast [them] into the Brook of Kidron;
15 Kisha wakamchinja mwana-kondoo wa Pasaka katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Makuhani na Walawi waliona aibu, wakajitakasa na kuleta sadaka za kuteketezwa katika Hekalu la Bwana.
and they slaughter the Passover-offering on the fourteenth of the second month, and the priests and the Levites have been ashamed, and sanctify themselves, and bring in burnt-offerings to the house of YHWH.
16 Kisha wakachukua nafasi zao za kawaida kama ilivyoelezwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu. Makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa na Walawi.
And they stand on their station according to their ordinance, according to the Law of Moses the man of God; the priests are sprinkling the blood out of the hand of the Levites,
17 Kwa kuwa wengi waliokuwa katika lile kusanyiko walikuwa hawajajitakasa, iliwapasa Walawi wachinje wana-kondoo wengine wa Pasaka kwa ajili ya wale watu ambao hawakuwa safi, kwa kufuata taratibu za ibada ili kuwatakasa kwa Bwana.
for many [are] in the assembly who have not sanctified themselves, and the Levites [are] over the slaughtering of the Passover-offerings for everyone not clean, to sanctify [him] to YHWH:
18 Ingawa watu wengi miongoni mwa wale waliotoka Efraimu, Manase, Isakari na Zabuloni walikuwa hawajajitakasa, hata hivyo walikula Pasaka kinyume na ilivyoandikwa. Lakini Hezekia akawaombea, akisema, “Bwana, ambaye ni mwema na amsamehe kila mmoja
for a multitude of the people, many from Ephraim, and Manasseh, Issachar, and Zebulun, have not been cleansed, but have eaten the Passover otherwise than it is written; but Hezekiah prayed for them, saying, “YHWH, who [is] good, receives atonement for everyone
19 ambaye anauelekeza moyo wake kumtafuta Mungu, Bwana, Mungu wa baba zake, hata kama yeye si safi kulingana na sheria za mahali patakatifu.”
who has prepared his heart to seek God—YHWH, God of his fathers—yet not according to the cleansing of the holy place”;
20 Naye Bwana akamsikia Hezekia akawaponya watu.
and YHWH listens to Hezekiah and heals the people.
21 Waisraeli waliokuwa Yerusalemu wakaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa muda wa siku saba, nao Walawi na makuhani walikuwa wakiimba kila siku, wakiwa na ala za uimbaji za kumsifu Bwana.
And the sons of Israel, those found in Jerusalem, make the Celebration of Unleavened Things [for] seven days with great joy; and the Levites and the priests are giving praise to YHWH day by day with instruments of praise before YHWH.
22 Hezekia akazungumza akiwatia moyo Walawi wote, ambao walionyesha ustadi katika kumtumikia Bwana. Hivyo watu wakala chakula cha sikukuu kwa siku saba, wakitoa sadaka za amani na kumshukuru Bwana, Mungu wa baba zao.
And Hezekiah speaks to the heart of all the Levites, those giving good understanding concerning YHWH, and they eat the appointed thing [for] seven days; sacrificing sacrifices of peace-offerings, and making confession to YHWH, God of their fathers.
23 Kisha kusanyiko lote likakubali kuendelea na sikukuu kwa siku saba zaidi, kwa hiyo kwa siku saba nyingine wakaendelea kuiadhimisha kwa furaha.
And all the assembly take counsel to keep [it] another seven days, and they keep [it for] seven days [with] joy;
24 Hezekia, mfalme wa Yuda akatoa mafahali 1,000, kondoo na mbuzi 7,000 kwa ajili ya kusanyiko, nao maafisa wakatoa mafahali 1,000 pamoja na kondoo na mbuzi 10,000. Idadi kubwa ya makuhani wakajiweka wakfu.
for Hezekiah king of Judah has presented one thousand bullocks and seven thousand sheep to the assembly; and the heads have presented one thousand bullocks and ten thousand sheep to the assembly; and priests sanctify themselves in abundance.
25 Kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi na lile kusanyiko lote lililotoka Israeli, pamoja na wale wageni waliotoka Israeli na wale walioishi katika Yuda wakafurahi.
And all the assembly of Judah rejoices, and the priests, and the Levites, and all the assembly, those coming in from Israel, and the sojourners—those coming in from the land of Israel and those dwelling in Judah,
26 Kulikuwa na furaha kubwa katika Yerusalemu, kwa sababu tangu siku za Mfalme Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli halijakuwepo jambo kama hili katika Yerusalemu.
and there is great joy in Jerusalem; for from the days of Solomon son of David, king of Israel, there is not like this in Jerusalem,
27 Ndipo makuhani na Walawi wakasimama wakawabariki watu, naye Mungu akawasikia, kwa sababu maombi yao yalifika mbinguni, makao yake matakatifu.
and the priests, the Levites, rise and bless the people, and their voice is heard, and their prayer comes into His holy habitation in the heavens.

< 2 Nyakati 30 >