< 2 Nyakati 3 >

1 Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu la Bwana katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapo Bwana alikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi.
E começou Salomão a edificar a casa do Senhor em Jerusalém, no monte de Moria, onde o Senhor se tinha mostrado a David seu pai, no lugar que David tinha preparado na eira d'Ornan, jebuseu.
2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa utawala wake.
E começou a edificar no segundo mes, no dia segundo, no ano quarto do seu reinado.
3 Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitini na upana dhiraa ishirini.
E estes foram os fundamentos que Salomão pôs para edificar a casa de Deus: o comprimento em côvados, segundo a medida primeira, de sessenta côvados, e a largura de vinte côvados.
4 Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini. Akaufunika ndani kwa dhahabu safi.
E o alpendre, que estava na frente, de comprimento segundo a largura da casa, era de vinte côvados, e a altura de cento e vinte: o que dentro cobriu com ouro puro.
5 Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo.
E a casa grande cobriu com madeira de faia; e então a cobriu com ouro fino: e fez sobre ela palmas e cadeias.
6 Alilipamba Hekalu kwa vito vya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu.
Também a casa adornou de pedras preciosas para ornamento: e o ouro era ouro de Parvaim.
7 Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.
Também na casa cobriu as traves, os umbrais, e as suas paredes, e as suas portas, com ouro: e lavrou cherubins nas paredes.
8 Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 120 za dhahabu safi.
Fez mais a casa da santidade das santidades, cujo comprimento, segundo a largura da casa, era de vinte côvados, e a sua largura de vinte côvados: e cobriu-a de ouro fino, do peso de seiscentos talentos.
9 Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.
O peso dos pregos era de cincoênta siclos de ouro: e os cenáculos cobriu de ouro.
10 Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu.
Também fez na casa da santidade das santidades dois cherubins de feição de andantes, e cobriu-os de ouro.
11 Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano, nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine.
E, quanto às asas dos cherubins, o seu comprimento era de vinte côvados; a aza dum deles de cinco côvados, e tocava na parede da casa; e a outra aza de cinco côvados, e tocava na aza do outro cherubim.
12 Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza.
Também a aza do outro cherubim era de cinco côvados, e tocava na parede da casa: era também a outra aza de cinco côvados, e estava pegada à aza do outro cherubim.
13 Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.
E as asas destes cherubins se estendiam vinte côvados: e estavam postos em pé, e os seus rostos virados para a casa.
14 Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na za kitani safi, na kutarizi makerubi juu yake.
Também fez o véu de azul, e púrpura, e carmezim, e linho fino: e pôs sobre ele cherubins.
15 Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake, na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano.
Fez também diante da casa duas colunas de trinta e cinco côvados de altura: e o capitel, que estava sobre cada uma, era de cinco côvados.
16 Akatengeneza minyororo iliyosokotwa, na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100, na kuyashikamanisha kwenye minyororo.
Também fez as cadeias, como no oráculo, e as pôs sobre as cabeças das colunas: fez também cem romãs, as quais pôs entre as cadeias.
17 Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakini, na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.
E levantou as colunas diante do templo, uma à direita, e outra à esquerda; e chamou o nome da que estava à direita Jachin, e o nome da que estava à esquerda Boaz.

< 2 Nyakati 3 >