< 2 Nyakati 3 >

1 Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu la Bwana katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapo Bwana alikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi.
Et Salomon commença à construire le Temple de l'Éternel à Jérusalem sur le mont de Moriia qui avait été indiqué à David, son père, au lieu que David avait disposé sur l'aire d'Ornan, le Jébusite.
2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa utawala wake.
Et il commença la construction au second mois, le second [jour], la quatrième année de son règne.
3 Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitini na upana dhiraa ishirini.
Et voici la base que Salomon fixa pour la construction de la Maison de Dieu: la longueur, en coudées ancienne mesure, soixante coudées, et la largeur, vingt coudées,
4 Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini. Akaufunika ndani kwa dhahabu safi.
et le vestibule dont la longueur occupait la largeur de la façade de l'édifice, vingt coudées, et la hauteur cent vingt, et il le revêtit intérieurement d'or pur.
5 Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo.
Et il revêtit le grand bâtiment de bois de cyprès, et le revêtit de bel or et d'un parement de palmiers et de chaînettes.
6 Alilipamba Hekalu kwa vito vya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu.
Et il recouvrit l'édifice de pierres précieuses comme ornement, et l'or était or de Parvaïm.
7 Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.
Et il revêtit d'or l'édifice, les solives, les seuils et ses parois et battants de porte, et cisela des Chérubins aux parois.
8 Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 120 za dhahabu safi.
Et il fit le bâtiment du Lieu Très-Saint, sa longueur égale à la largeur de l'édifice, étant de vingt coudées, et sa largeur de vingt coudées, et le revêtit de bel or qui se montait à six cents talents.
9 Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.
Et le poids pour les clous était de cinquante sicles d'or. Et il revêtit aussi d'or les chambres supérieures.
10 Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu.
Et il fit dans le Lieu Très-Saint deux Chérubins en travail de sculpture, et on les recouvrit d'or.
11 Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano, nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine.
Quant aux ailes des Chérubins, leur longueur était de vingt coudées; l'aile de l'un, longue de cinq coudées, touchait à la paroi de l'édifice, et l'autre aile, longue de cinq coudées, touchait à l'aile de l'autre Chérubin;
12 Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza.
et l'aile de l'autre Chérubin, longue de cinq coudées, touchait à la paroi de l'édifice, et l'autre aile, longue de cinq coudées, joignait l'aile de l'autre Chérubin;
13 Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.
les ailes de ces Chérubins, déployées, avaient vingt coudées de longueur, et ils étaient debout sur leurs pieds et leurs visages regardaient l'édifice.
14 Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na za kitani safi, na kutarizi makerubi juu yake.
Et il fit le voile de pourpre azuré et rouge et de cramoisi et de byssus et y adapta des Chérubins.
15 Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake, na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano.
Et il fit devant l'édifice deux colonnes ayant trente-cinq coudées de hauteur, et le parement de leur faîte avait cinq coudées [de longueur].
16 Akatengeneza minyororo iliyosokotwa, na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100, na kuyashikamanisha kwenye minyororo.
Et il fit des chaînettes dans le Sanctuaire et en mit aux faîtes des colonnes et fit cent grenades qu'il ajusta aux chaînettes.
17 Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakini, na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.
Et il dressa les colonnes à la façade du Temple, une à droite et une à gauche, et donna à celle de droite le nom de Jachin et à celle de gauche le nom de Boaz.

< 2 Nyakati 3 >