< 2 Nyakati 3 >

1 Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu la Bwana katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapo Bwana alikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi.
Et Salomon commença à bâtir le temple du Seigneur à Jérusalem, sur le mont Moria, où le Seigneur était apparu à David, son père, au lieu que David avait préparé, dans l'aire d'Orna le Jébuséen.
2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa utawala wake.
Il commença à bâtir le second mois de la quatrième année de son règne.
3 Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitini na upana dhiraa ishirini.
Et voici comme Salomon commença à bâtir le temple du Seigneur: il lui donna soixante coudées de longueur (ce fut la première mesure), et vingt coudées de largeur.
4 Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini. Akaufunika ndani kwa dhahabu safi.
Le portique de la façade du temple eut vingt coudées de long; c'était la largeur même de l'édifice; sa hauteur fut de cent vingt coudées; Hiram le dora avec de l'or pur, intérieurement.
5 Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo.
Et il revêtit de lambris de cèdre le corps de l'édifice, et il le dora d'or pur, sur lequel il grava des palmiers et des chaînes.
6 Alilipamba Hekalu kwa vito vya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu.
Et il orna le temple de pierres précieuses d'un vif éclat, et il le couvrit de lames d'or, et il y employa de l'or de Pharaïm.
7 Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.
Et il dora le temple, ses murs, ses portes, ses plafonds, les battants des portes, et il fit sur les parois des chérubins ciselés.
8 Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 120 za dhahabu safi.
Et il fit le Saint des saints, dont la façade avait vingt coudées de long, largeur du temple et dont les côtés étaient pareillement de vingt coudées; il le dora d'or pur du poids de six cents talents; pour les chérubins ciselés,
9 Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.
Les clous pesaient chacun cinquante sicles d'or; il revêtit aussi d'or l'étage supérieur.
10 Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu.
Puis, il fit, dans le Saint des saints, deux chérubins de bois qu'il revêtit de lames d'or pur.
11 Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano, nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine.
Les ailes des chérubins avaient un déploiement de vingt coudées; chaque aile était de cinq coudées, de sorte que l'aile droite de l'un des chérubins touchait un mur, et l'aile gauche de l'autre chérubin touchait le mur opposé; [et son autre aile de cinq coudées touchait l'aile de l'autre chérubin.]
12 Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza.
[Et l'aile d'un chérubin était de cinq coudées atteignant le mur du temple, et son autre aile était aussi de cinq coudées, joignant l'aile de l'autre chérubin.]
13 Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.
Les ailes des deux chérubins étaient donc déployées, et il y avait entre les deux ailes extrêmes une distance de vingt coudées. Ils étaient en pied, le visage tourné vers l'intérieur du temple.
14 Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na za kitani safi, na kutarizi makerubi juu yake.
Il fit aussi un voile d'hyacinthe, de pourpre, d'écarlate et de lin, dans lequel étaient tissus des chérubins.
15 Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake, na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano.
Et il fit, devant le temple, deux colonnes, hautes de trente-cinq coudées, avec des chapiteaux de cinq coudées.
16 Akatengeneza minyororo iliyosokotwa, na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100, na kuyashikamanisha kwenye minyororo.
Et il fit des chaînes dans l'oracle, et il les plaça sur les chapiteaux des colonnes, et il fit cent petites grenades qu'il posa sur les chaînes.
17 Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakini, na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.
Et il plaça les colonnes sur la façade du temple, l'une à droite, l'autre à gauche, et il appela celle de droite Rectitude, et celle de gauche Force.

< 2 Nyakati 3 >