< 2 Nyakati 3 >

1 Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu la Bwana katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapo Bwana alikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi.
Then Solomon began to build the house of the LORD at Jerusalem in mount Moriah, where the LORD appeared unto David his father; for which provision had been made in the Place of David, in the threshingfloor of Ornan the Jebusite.
2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa utawala wake.
And he began to build in the second day of the second month, in the fourth year of his reign.
3 Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitini na upana dhiraa ishirini.
Now these are the foundations which Solomon laid for the building of the house of God. The length by cubits after the ancient measure was threescore cubits, and the breadth twenty cubits.
4 Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini. Akaufunika ndani kwa dhahabu safi.
And the porch that was before the house, the length of it, according to the breadth of the house, was twenty cubits, and the height a hundred and twenty; and he overlaid it within with pure gold.
5 Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo.
And the greater house he covered with cypress-wood, which he overlaid with fine gold, and wrought thereon palm-trees and chains.
6 Alilipamba Hekalu kwa vito vya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu.
And he garnished the house with precious stones for beauty; and the gold was gold of Parvaim.
7 Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.
He overlaid also the house, the beams, the thresholds, and the walls thereof, and the doors thereof, with gold; and graved cherubim on the walls.
8 Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 120 za dhahabu safi.
And he made the most holy place; the length thereof, according to the breadth of the house, was twenty cubits, and the breadth thereof twenty cubits; and he overlaid it with fine gold, amounting to six hundred talents.
9 Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.
And the weight of the nails was fifty shekels of gold. And he overlaid the upper chambers with gold.
10 Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu.
And in the most holy place he made two cherubim of image work; and they overlaid them with gold.
11 Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano, nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine.
And the wings of the cherubim were twenty cubits long: the wing of the one cherub was five cubits, reaching to the wall of the house; and the other wing was likewise five cubits, reaching to the wing of the other cherub.
12 Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza.
And the wing of the other cherub was five cubits, reaching to the wall of the house; and the other wing was five cubits also, joining to the wing of the other cherub.
13 Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.
The wings of these cherubim spread themselves forth twenty cubits; and they stood on their feet, and their faces were inward.
14 Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na za kitani safi, na kutarizi makerubi juu yake.
And he made the veil of blue, and purple, and crimson, and fine linen, and wrought cherubim thereon.
15 Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake, na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano.
Also he made before the house two pillars of thirty and five cubits high, and the capital that was on the top of each of them was five cubits.
16 Akatengeneza minyororo iliyosokotwa, na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100, na kuyashikamanisha kwenye minyororo.
And he made chains in the Sanctuary, and put them on the tops of the pillars; and he made a hundred pomegranates, and put them on the chains.
17 Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakini, na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.
And he set up the pillars before the temple, one on the right hand, and the other on the left; and called the name of that on the right hand Jachin, and the name of that on the left Boaz.

< 2 Nyakati 3 >