< 2 Nyakati 29 >

1 Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
Језекији беше двадесет и пет година кад поче царовати, и царова двадесет и девет година у Јерусалиму. Матери му беше име Авија, кћи Захаријина.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.
И чињаше што је право пред Господом сасвим како је чинио Давид отац његов.
3 Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati.
Прве године свог царовања, првог месеца, отвори врата на дому Господњем, и оправи их.
4 Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki
И сазва свештенике и Левите, и сабра их на источну улицу,
5 na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu.
И рече им: Чујте ме, Левити, освештајте се сада и осветите дом Господа Бога отаца својих, и изнесите нечистоту из светиње.
6 Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao.
Јер сагрешише оци наши и чинише што је зло пред Господом Богом нашим, и оставише га; и одвратише лице своје од шатора Господњег и окренуше му леђа;
7 Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli.
И затворише врата од трема, и погасише жишке, и кадом не кадише, нити жртава паљеница приносише у светињи Богу Израиљевом.
8 Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe.
Зато се разгневи Господ на Јуду и на Јерусалим, те их даде да се потуцају, и да буду чудо и подсмех, како видите својим очима.
9 Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka.
Јер, ето, падоше оци наши од мача, и синови наши и кћери наше и жене наше заробише се зато.
10 Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi.
Сада дакле наумио сам задати веру Господу Богу Израиљевом, да би се одвратила од нас жестина гнева Његовог.
11 Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”
Синови моји, не оклевајте више, јер је вас изабрао Господ да стојите пред Њим и служите му, и да му будете слуге и да му кадите.
12 Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi: Kutoka kwa Wakohathi, Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria; kutoka kwa Wamerari, Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli; kutoka kwa Wagershoni, Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;
Тада усташе Левити Мат син Амасајев и Јоило син Азаријин од синова Катових; а од синова Мераријевих Кис син Авдијев и Азарија син Јалелеилов; и од синова Гирсонових Јоах син Зимин и Еден син Јоахов;
13 kutoka kwa wana wa Elisafani, Shimri na Yeieli; kutoka kwa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
И од синова Елифасанових Симрије и Јеило, и од синова Асафових Захарија и Матанија;
14 kutoka kwa wana wa Hemani, Yehieli na Shimei; kutoka kwa wana wa Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
И од синова Амонових Јеило и Симеј, и од синова Једутунових Семаја и Озило;
15 Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana.
И скупише браћу своју, и освештавши се дођоше, како беше заповедио цар по речи Господњој, да очисте дом Господњи.
16 Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni.
И ушавши свештеници у дом Господњи да га очисте, износише сву нечистоту што нађоше у цркви Господњој у трем дома Господњег; а Левити купише и износише напоље на поток Кедрон.
17 Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.
А почеше освећивати првог дана првог месеца; а осмог дана тог месеца уђоше у трем Господњи, и освећиваше дом Господњи осам дана, и шеснаестог дана првог месеца свршише.
18 Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.
Потом дођоше к цару Језекији и рекоше: Очистисмо сав дом Господњи и олтар за жртве паљенице и све судове његове и сто за постављање и све судове његове,
19 Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”
И све судове које беше бацио цар Ахаз докле цароваше грешећи, и спремисмо и осветисмо, и ено их пред олтаром Господњим.
20 Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana.
Потом цар Језекија уста рано, и сазва управитеље градске, и отиде у дом Господњи.
21 Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana.
И доведе седам јуница и седам овнова и седам јагањаца и седам јараца за грех, за царство и за светињу и за Јуду; и рече синовима Ароновим свештеницима да принесу на олтару Господњем.
22 Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu.
Тада заклаше говеда, и свештеници узевши крв њихову покропише олтар; заклаше и овнове, и крвљу њиховом покропише олтар; и заклаше јагањце и крвљу њиховом покропише олтар.
23 Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu.
Потом доведоше јарце за грех пред цара и пред збор, и они метнуше руке своје на њих.
24 Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.
И заклаше их свештеници, и очистише крвљу њиховом олтар на очишћење свему Израиљу, јер цар заповеди да се за сав народ Израиљев принесе жртва паљеница и жртва за грех.
25 Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake.
И постави Левите у дому Господњем с кимвалима и псалтирима и гуслама, како беше заповедио Давид и Гад виделац царев и Натан пророк; јер од Господа беше заповест преко пророка Његових.
26 Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.
И тако стајаху Левити са справама Давидовим а свештеници с трубама.
27 Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli.
Тада заповеди Језекија да принесу жртву паљеницу на олтару. И кад се поче жртва паљеница, поче се песма Господња уз трубе и справе Давида, цара Израиљевог.
28 Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.
И сав се збор клањаше, и певачи певаху и трубачи трубљаху, и то све докле се не сврши жртва паљеница.
29 Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu.
А кад свршише жртву, цар и сви који беху с њим падоше и поклонише се.
30 Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.
Потом рече цар и кнезови Левитима да хвале Господа речима Давидовим и Асафа видеоца; и хвалише с великим весељем, и савивши се поклонише се.
31 Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.
Тада Језекија проговори и рече: Сада посветисте руке своје Господу, приступите и донесите приносе и жртве захвалне у дом Господњи. И донесе сав збор приносе и жртве захвалне, и ко год беше вољног срца жртве паљенице.
32 Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana.
И на број беше жртава паљеница што донесе збор, седамдесет волова, сто овнова, двеста јагањаца, све за жртву паљеницу Господу;
33 Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000.
А других ствари посвећених беше шест стотина волова и три хиљаде оваца.
34 Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani.
Али мало беше свештеника, те не могаху драти свих жртава паљеница; зато им помагаху браћа њихова Левити, докле се не сврши посао и докле се не освешташе други свештеници; јер Левити беху радији освештати се него свештеници.
35 Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa. Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya.
И беше врло много жртава паљеница с претилином од жртава захвалних и налива на жртве паљенице. Тако би повраћена служба у дому Господњем.
36 Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.
И радоваше се Језекија и сав народ, што Бог управи народ, јер ово би нагло.

< 2 Nyakati 29 >