< 2 Nyakati 29 >

1 Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
A Ezechyjasz gdy począł królować, miał dwadzieścia i pięć lat; a dwadzieścia i dziewięć lat królował w Jeruzalemie. Imię matki jego Abi, córka Zacharyjaszowa.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.
A czynił co było dobrego przed oczami Pańskiemi, według wszystkiego, jako czynił Dawid ojciec jego.
3 Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati.
Ten roku pierwszego królowania swego, miesiąca pierwszego, otworzył drzwi domu Pańskiego, i poprawił je.
4 Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki
I przywiódł kapłanów i Lewitów, a zgromadził ich na ulicę wschodnią.
5 na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu.
I rzekł do nich: Słuchajcie mię Lewitowie: Teraz się poświęćcie: poświęćcie też i dom Pana, Boga ojców waszych, i wyrzućcie plugastwa z świątnicy:
6 Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao.
Albowiem zgrzeszyli ojcowie nasi, i czynili złe przed oczyma Pana, Boga naszego, opuszczając go, i odwracając oblicza swoje od przybytku Pańskiego, a obracając się tyłem do niego.
7 Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli.
Zamknęli też drzwi u przysionka, i pogasili lampy, a kadzidłem nie kadzili, ani całopalenia nie ofiarowali w świątnicy Bogu Izraelskiemu.
8 Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe.
Przetoż był gniew Pański nad Judą, i nad Jeruzalemem, a podał ich na rozproszenie, na spustoszenie, i na pośmiech, jako sami widzicie oczyma waszemi.
9 Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka.
Bo oto polegli ojcowie nasi od miecza, a synowie nasi, i córki nasze, i żony nasze zawiedzione są w niewolę dla tego.
10 Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi.
Teraz tedy umyśliłem uczynić przymierze z Panem, Bogiem Izraelskim, aby odwrócił od nas gniew popędliwości swojej.
11 Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”
Synowie moi! nie bądźcież już niedbałymi; bo was Pan obrał, abyście stojąc przed nim służyli mu, a byli sługami jego, i kadzili mu.
12 Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi: Kutoka kwa Wakohathi, Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria; kutoka kwa Wamerari, Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli; kutoka kwa Wagershoni, Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;
Tedy powstali Lewitowie: Machat, syn Amasajowy, i Joel, syn Azaryjaszowy, z synów Kaatowych, a z synów Merarego: Cys, syn Abdy, i Azaryjasz, syn Jehaleelowy; a z Giersończyków: Joach, syn Zamy, i Eden, syn Joachowy:
13 kutoka kwa wana wa Elisafani, Shimri na Yeieli; kutoka kwa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
A z synów Elisafanowych: Symry i Jehijel: a z synów Asafowych: Zacharyjasz i Matanijasz;
14 kutoka kwa wana wa Hemani, Yehieli na Shimei; kutoka kwa wana wa Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
A z synów Hemanowych: Jehijel i Symchy; a z synów Jedytunowych: Semejasz i Uzyjel.
15 Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana.
I zgromadzili braci swych, którzy poświęciwszy się przyszli według rozkazania królewskiego, i rozkazania Pańskiego, aby wyczyścili dom Pański.
16 Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni.
A wszedłszy kapłani do domu Pańskiego, aby go oczyścili, wynieśli wszystkie plugastwa, które znaleźli w kościele Pańskim, do sieni domu Pańskiego; a Lewitowie zabrawszy to wynieśli precz do potoku Cedron.
17 Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.
I poczęli pierwszego dnia miesiąca pierwszego poświęcać, a dnia ósmego tego miesiąca weszli do przysionku Pańskiego i poświęcali dom Pański przez ośm dni, a dnia szesnastego, miesiąca pierwszego, dokończyli.
18 Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.
Potem weszli do króla Ezechyjasza, i rzekli: Oczyściliśmy wszystek dom Pański, i ołtarz całopalenia, i wszystkie naczynia jego, i stół pokładny i wszystkie naczynia jego;
19 Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”
Także wszystko naczynie, które był odrzucił król Achaz za królowania swego, gdy grzeszył, zgotowaliśmy i poświęcili; a oto są przed ołtarzem Pańskim.
20 Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana.
A tak wstawszy rano król Ezechyjasz zgromadził przedniejszych miasta, i szedł do domu Pańskiego.
21 Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana.
I przywiedziono mu cielców siedm, i baranów siedm, i baranków siedm, i kozłów siedm, na ofiarę za grzech, za królestwo, i za świątnicę, i za Judę, a rozkazał synom Aaronowym, kapłanom, aby ofiarowali na ołtarzu Pańskim.
22 Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu.
A tak pobili one woły, a kapłani wziąwszy krew ich kropili po ołtarzu; pobili też i barany, a kropili krwią ich po ołtarzu; pobili też i baranki, a kropili krwią ich po ołtarzu.
23 Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu.
Przywiedli kozły też na ofiarę za grzech przed króla i przed zgromadzenie, którzy włożyli ręce swoje na nie.
24 Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.
I pobili je kapłani, i oczyścili krwią ich ołtarz na oczyszczenie wszystkiego Izraela; albowiem za wszystkiego Izraela rozkazał król ofiarować całopalenie i ofiarę za grzech.
25 Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake.
Postanowił też i Lewitów w domu Pańskim z cymbałami, i z cytrami, i z harfami, według rozkazania Dawidowego, i Gada, widzącego królewskiego, i Natana proroka; bo to było rozkazanie Pańskie przez proroków jego.
26 Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.
A tak stali Lewitowie z instrumentami Dawidowemi, i kapłani z trąbami.
27 Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli.
I rozkazał Ezechyjasz, aby ofiarowali całopalenia na ołtarzu; a gdy się zaczęło całopalenie, poczęło się śpiewanie Panu, i trąbienie, i granie na instrumentach Dawida, króla Izraelskiego.
28 Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.
Tedy wszystko zgromadzenie kłaniało się, a śpiewacy śpiewali, i trębacze trąbili; co wszystko trwało, póki się nie dokończyło całopalenie.
29 Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu.
A gdy się skończyło całopalenie, poklęknęli król i wszyscy, którzy z nim byli, i modlili się.
30 Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.
Tedy rozkazał król Ezechyjasz i książęta Lewitom, aby chwalili Pana słowy Dawidowemi, i Asafa, widzącego; chwalili z weselem wielkiem, a kłaniając się modlili się.
31 Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.
Zatem rzekł Ezechyjasz, mówiąc: Terazeście poświęcili ręce wasze Panu; przystąpcież, a przywiedźcie ofiary spokojne, i ofiary chwały do domu Pańskiego. Przetoż przywiodło ono zgromadzenie ofiary spokojne i ofiary chwały, i każdy ochotnego serca przywiódł ofiary na całopalenie.
32 Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana.
I była liczba ofiar na całopalenie, które przywiodło zgromadzenie, wołów siedmdziesiąt, baranów sto, baranków dwieście, wszystko to na całopalenie Panu.
33 Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000.
Innych też rzeczy poświęconych było: wołów sześć set, i owiec trzy tysiące,
34 Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani.
Lecz kapłanów mało było, tak, iż nie mogli nadążyć odzierać ze skóry wszystkich ofiar na całopalenie: przetoż im pomagali Lewitowie, bracia ich, póki nie dokończyli onej pracy, i póki się nie poświęcili drudzy kapłani; albowiem Lewitowie byli och otniejsi, aby się poświęcili, niż kapłani.
35 Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa. Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya.
Nadto i całopalenia było bardzo wiele z tłustościami spokojnych ofiar, i z mokremi ofiarami na całopalenie. A tak wygotowana była służba domu Pańskiego.
36 Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.
I weselił się Ezechyjasz i wszystek lud z tego, co Bóg ludowi przygotował; bo się ta rzecz była z prędka stała.

< 2 Nyakati 29 >