< 2 Nyakati 29 >
1 Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
Ni-roapolo taoñe lim’ amby t’Iekizkia te niorotse nifehe, le nifehe roapolo taoñe sive amby e Ierosalaime ao: i Abiià ana’ i Zekarià ty tahinan-drene’e.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.
Le nanao ty fahiti’e am-pihaino’ Iehovà, manahake ze he’e nanoe’ i Davide rae’e.
3 Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati.
Ie amy taom-baloham-pifehea’ey, amy volam-baloha’ey, le sinoka’e o lalambein’ anjomba’ Iehovào vaho nisomontie’e.
4 Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki
Nampiheove’e ao o mpisoroñeo naho o nte-Levio, le natonto’e ho raik’ amy toetse mangadagadañe atiñanañey,
5 na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu.
vaho nanoa’e ty hoe, Mijanjiña ahy ry nte-Levio, mampiavaha vatañe henaneo, le ampiavaho ty anjomba’ Iehovà Andrianañaharen-droae’ areo vaho ondroho boak’ an-toetse miavake ao ze atao leotse.
6 Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao.
Fa nikitro-karatiañe naho nanao haloloañe am-pihaino’ Iehovà Andrianañaharentikañe o roaentikañeo naho naforintse’ iereo naho nitoli-daharañe vaho tsinambolitio’ iereo ty fimoneña’ Iehovà.
7 Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli.
Mbore narindri’ iareo o lalambein-davarangañeo naho nakipeke o failoo naho tsy nañemboke, tsy nañenga soroñe aman’ Añahare’ Israele amy toetse masiñey.
8 Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe.
Toly ndra nifetsak’ am’ Iehoda naho am’ Ierosalaime ty haviñera’ Iehovà, le natolo’e ho fangebahebahañe naho halatsañe naho fikosihañe, manahake o isam-pihaino’ areoo.
9 Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka.
Hehe te nakoròvom-pibara o roaen-tikañeo naho am-pandrohizañe añe o ana-dahintikañeo naho o anak’ ampelan-tikañeo vaho o tañanjomban-tikañeo, ty amy zay.
10 Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi.
Aa le an-troko ao henaneo ty hifañina am’ Iehovà Andrianañahare’ Israele, hampihankañe aman-tika i haviñera’e miforoforoy.
11 Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”
O ry anako, ko mihenekeneke henaneo; fa jinobo’ Iehovà nahareo hijohañe añatrefa’e, hiatrak’ aze naho ho mpitoro’e vaho hañembok’ ama’e.
12 Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi: Kutoka kwa Wakohathi, Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria; kutoka kwa Wamerari, Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli; kutoka kwa Wagershoni, Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;
Niongak’ amy zao o nte-Levio, i Makate, ana’ i Amasay naho Ioele ana’ i Azarià amo ana’ o nte-Kehàteo; le amo ana’ i Merario: i Kise, ana’ i Abdý naho i Azarià ana’ Iehalelale; le amo nte-Gersoneo, Ioak’ ana’ i Zimà naho i Edene ana’ Ioake;
13 kutoka kwa wana wa Elisafani, Shimri na Yeieli; kutoka kwa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
le amo ana’ i Elitsafaneo; i Simrý naho Ieiele; le amo ana’ i Asafeo; i Zekarià naho i Matanià;
14 kutoka kwa wana wa Hemani, Yehieli na Shimei; kutoka kwa wana wa Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
le amo ana’ i Hemaneo; Iehiele naho i Simey; vaho amo ana’ Iedotoneo, i Semaià naho i Oziele.
15 Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana.
Le navori’ iareo o roahalai’eo, le nañamasim-batañe vaho nimoak’ ao, ty amy lili’ i mpanjakay ty amo tsara’ Iehovào, hañalio ty anjomba’ Iehovà.
16 Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni.
Nizilik’ amy toetse añate’ i anjomba’ Iehovày o mpisoroñeo, hañalio aze, le nakareñe ze fonga leotse nizoe’ iereo an-kiboho’ Iehovà ao mb’ an-kiririsan’ anjomba’ Iehovà ey, le rinambe’ o nte-Levio naho nandese’e mb’ an-torahan-Kidrone añe.
17 Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.
Aa ie niorotse nampiavake amy androm-baloha’ i volam-baloha’eiy, le pok’ amy lavaranga’ Iehovày iereo amy androm-pahavalo’ i volañeiy; le valo andro ty nampiavahe’ iereo ty anjomba’ Iehovà; vaho nifonire’ iareo amy andro faha folo-eneñ’ ambi’ i volam-baloha’eiy.
18 Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.
Aa le niheo mb’am’ Iekizkia mpanjaka mb’eo iereo, nanao ty hoe: Fa niliove’ay iaby ty anjomba’ Iehovà naho i kitrelim-pisoroñañey naho o fana’e iabio naho i lataba’ o mofo-piatrekeoy vaho o fana’e iabio.
19 Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”
Mbore nivaoe’ay naho navahe’ay o fanake iaby nahifi’ i Ahkazeo, ie nanao haloloañe amy fifehea’ey; le oniño t’ie fa aolo’ i kitreli’ Iehovày.
20 Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana.
Nañaleñaleñe t’Iekizkia, mpanjaka nanontoñe o roandria’ i rovaio vaho nionjomb’ amy anjomba’ Iehovà mb’eo,
21 Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana.
le ninday bania fito naho añondrilahy fito naho vik’ añondry fito vaho oselahy fito ho fañeferan-kakeo’ i fifeheañey naho i toetse masiñey vaho Iehodà. Le linili’e o mpisoroñeo, o ana’ i Aharoneo, t’ie hengaeñe amy kitreli’ Iehovày.
22 Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu.
Aa le linenta’ iareo i bania rey naho rinambe’ o mpisoroñeo ty lio’e, le nadasi’ iereo amy kitreliy; le linenta’ iereo i añondrilahy rey naho nadasi’ iereo amy kitrelio ty lio’e; linenta’ iareo ka i vik’añondry rey vaho nadasi’ iareo amy kitreliy ty lio’e.
23 Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu.
Le nañarivoe’ iereo i oselahy rey ho ami’ty fañeferan-kakeo, añatrefa’ i mpanjakay naho i fivoriy, le nanampeza’ iareo fitañe;
24 Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.
naho linenta’ o mpisoroñeo le nanao fañeferan-kakeo ambone’ i kitreliy amy lio’ey, hijebañañe Israele iaby; fa linili’ i mpanjakay te hanoeñe ho a Israele iaby i soroñey naho i fañeferan-kakeoy.
25 Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake.
Le nampijohañe’e añ’ anjomba’ Iehovà ao o nte-Levio reketse fikontsañañe naho jejo-bory vaho marovany ty amy lili’ i Davidey naho i Gade mpioni’ i mpanjakay naho i Natane mpitokiy vaho toe lili’ Iehovà añamo mpitoki’eo.
26 Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.
Aa le nijohañe eo o nte-Levio rekets’ o fititiha’ i Davideo naho o mpisoroñeo reketse trompetra.
27 Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli.
Le linili’ Iekizkia te hengaeñe ambone’ i kitreliy i soroñey. Aa ie namototse i fisoroñañey, le niorotse ka ty fisaboañe Iehovà an-trompetra mitraoke amo fititiha’ i Davide mpanjaka’ Israeleo.
28 Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.
Le nibaboke i fivory iabiy naho nitakasy o mpisaboo naho nitioke o mpampipopò trompetrao; vaho nitolom-panao izay ampara’ te niheneke i fisoroñañey.
29 Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu.
Ie nifonitse i fañengañey, le nidròdreke vaho niambane i mpanjakay naho o mpiama’e iabio.
30 Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.
Mbore linili’ Iekizkia mpanjaka naho o roandriañeo o nte-Levio ty hitakasy am’ Iehovà amo onin-tsabo’ i Davide naho i Asafe mpioniñeo. Le nisabo fandrengeañe an-kaehake naho niandaly vaho nitalaho.
31 Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.
Nampigadoñe’ Iekizkia, ami’ty hoe: Fa navahañe am’ Iehovà nahareo henaneo; mañarinea le mibanabanà soroñe naho engam-pañandriañañe mb’añ’anjomba’ Iehovà. Aa le nanese soroñe naho engam-pañandriañañe i fivoriy; vaho ninday engan-koroañe o matarikeo.
32 Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana.
Aa ty ia’ o soroñe nendese’ o fivorio mb’eoo, le bania fitompolo naho añondrilahy zato vaho vik’ añondry roanjato; hene hisoroñañe am’ Iehovà.
33 Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000.
Le o enga navaheñeo: añombe enen-jato naho añondry telo-arivo.
34 Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani.
Fe tsy niampe ty mpisoroñe hañolitse o hisoroñañeo, aa le nimbae’ o nte-Levy roahalahi’ iareoo, ampara’ te niheneke i fitoloñañey, ampara’ te nañamasim-batañe o mpisoroñe ila’eo; amy te nilombolombo’ o mpisoroñeo o nte-Levio ami’ty havañonan’ arofo nampiavahem-batañe.
35 Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa. Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya.
Nimaro o nisoroñañe reketse i saboran’ engam-panintsiñañeio naho o enga-rano ho amo nisoroñañeo. Aa le nijadoñe soa ty fitoroñañe añ’ anjomba’ Iehovà ao,
36 Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.
naho nandia taroba t’Iekizkia naho ondaty iabio, ty amy nampihentseñan’ Añahare ho a’ondatio; amy te nitojeha i nanoeñey.