< 2 Nyakati 29 >

1 Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
Hezekiah el tokosrala fin acn Judah ke el yac longoul limekosr, ac el leum in Jerusalem ke yac longoul eu. Nina kial pa Abijah, acn natul Zechariah.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.
El fahsr tukun srikasrak lal Tokosra David, papa matu tumal, ac el oru ma LEUM GOD El insewowo kac.
3 Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati.
In malem se meet ke yac se tukun Hezekiah el tokosrala, el sifil ikasla mutunoa lun Tempul, ac sap in akwoyeyukla.
4 Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki
El solani sie un mwet tol ac mwet Levi ke nien tukeni se layen kutulap in Tempul,
5 na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu.
ac kaskas nu selos we. El fahk, “Kowos mwet Levi, akmutalye kowos ac aknasnasyela Tempul lun LEUM GOD lun papa tomowos. Sisla liki Tempul ma nukewa ma akfohkfokye.
6 Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao.
Papa matu tumasr elos tiana pwaye nu sin LEUM GOD lasr, ac elos oru ma El tia insewowo kac. Elos ngetla lukel ac fahsr liki yen El muta we.
7 Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli.
Elos kaliya mutunoa lun Tempul ac fuhlela lam we in kunla. Elos tia akosak mwe keng ku kisakin mwe kisa firir in Tempul lun God lun Israel.
8 Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe.
Ke sripa inge, LEUM GOD El kasrkusrak sin Judah ac Jerusalem, ac ma El oru nu selos arulana mwe lut ac mwe aksangeng nu sin mwet nukewa. Kowos sifacna liye ma inge ke motowos.
9 Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka.
Papa tumasr elos anwuki ke mweun, ac utukla mutan kiasr ac tulik natusr nu in sruoh.
10 Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi.
“Inge nga akola in orala sie wulela yurin LEUM GOD lun Israel, tuh Elan tia sifil kasrkusrak sesr.
11 Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”
Wen nutik, nik kowos sisla pacl. Kowos pa LEUM GOD El sulela in akosak mwe keng nu sel, ac in kol mwet uh in alu nu sel.”
12 Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi: Kutoka kwa Wakohathi, Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria; kutoka kwa Wamerari, Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli; kutoka kwa Wagershoni, Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;
Na mwet Levi inge elos tuyak: Liki sou lulap lal Kohath: Mahath wen natul Amasai, ac Joel wen natul Azariah Liki sou lulap lal Merari: Kish wen natul Abdi, ac Azariah wen natul Jehallelel Liki sou lulap lal Gershon: Joah wen natul Zimmah, ac Eden wen natul Joah
13 kutoka kwa wana wa Elisafani, Shimri na Yeieli; kutoka kwa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
Liki sou lulap lal Elizaphan: Shimri ac Jeuel Liki sou lulap lal Asaph: Zechariah ac Mattaniah
14 kutoka kwa wana wa Hemani, Yehieli na Shimei; kutoka kwa wana wa Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
Liki sou lulap lal Heman: Jehuel ac Shimei Liki sou lulap lal Jeduthun: Shemaiah ac Uzziel
15 Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana.
Mwet inge elos solani mwet Levi wialos, ac elos nukewa aknasnasyalos sifacna. Na elos oru oana ma tokosra el sapkin nu selos, ac elos mutawauk in oru Tempul uh in nasnas, fal nu ke Ma Sap lun LEUM GOD.
16 Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni.
Mwet tol elos utyak nu in Tempul in aknasnasyela, ac ma nukewa we ma tia nasnas elos usla liki Tempul nu ke nien tukeni likinum in Tempul. Na mwet Levi elos us ma inge nukewa we lac nu Infahlfal Kidron likin siti uh.
17 Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.
Orekma se inge mutawauk ke len se meet ke malem se meet, ac ke len akoalkosr elos aksafyela ma nukewa, weang pac infukil in utyak nu in Tempul. Na elos sifil orekma len oalkosr toko, nwe ke len aksingoul onkosr ke malem sac tuh elos in akoo Tempul nu ke alu.
18 Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.
Mwet Levi elos fahkak koanon orekma lalos nu sel Tokosra Hezekiah. Elos fahk, “Kut aknasnasyela tari acn nukewa in Tempul, weang pac loang in orek kisa, tepu neinyen bread mutal, ac kufwen mwe orekma nukewa.
19 Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”
Kut oayapa folokonma kufwa nukewa ma Tokosra Ahaz el usla ke pacl ma el tuh tia pwaye nu sin LEUM GOD, ac kut sifil akmutalyela nufon. Ma inge nukewa oasr mutun loang lun LEUM GOD.”
20 Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana.
Tokosra Hezekiah el sulaklak na pangoneni mwet kol lun siti uh, ac elos tukeni som nu ke Tempul.
21 Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana.
Elos srukak cow mukul itkosr, sheep itkosr, sheep fusr itkosr, ac nani itkosr in mwe kisa in aknasnasye ma koluk lun sou in leum uh ac mwet Judah, ac in aknasnasye Tempul. Na tokosra el fahk nu sin mwet tol, su ma in sou lal Aaron, in orekmakin kosro inge in mwe kisa fin loang uh.
22 Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu.
Mwet tol elos uniya cow mukul uh meet, na sheep uh toko, na fah sheep fusr, ac elos aksroksrokye loang uh ke srahn ma inge ke kais sie pacl ma kisaiyuk kosro inge.
23 Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu.
Tukun ma inge nukewa elos usla nani uh nu yorol tokosra ac mwet ma wi alu uh, ac elos filiya paolos fin nani inge.
24 Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.
Na mwet tol elos uniya nani uh, ac ukuiya srah kac nu fin loang uh tuh in mwe kisa nu ke eela ma koluk lun mwet nukewa, mweyen tokosra el sap tuh mwe kisa firir, ac mwe kisa in eela ma koluk, in orek ke mwet Israel nukewa.
25 Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake.
Tokosra el oru oana ma LEUM GOD El sapkin nu sel Tokosra Davi — ma David el eis sel Gad, mwet liaten lun tokosra, oayapa sel mwet palu Nathan. Tokosra el oakiya acn sin mwet Levi in Tempul, wi harp ac cymbal,
26 Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.
kain mwe on ma Tokosra David el tuh orekmakin. Mwet tol elos oayapa tu we wi mwe ukuk natulos.
27 Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli.
Hezekiah el sap in mutawauk orek mwe kisa firir, ac ke kisa uh mutawauk, mwet uh on ac kaksak nu sin LEUM GOD, ac mwet srital ke mwe on elos mutawauk ukya mwe ukuk ac mwe on nukewa pac saya.
28 Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.
Mwet nukewa su muta we elos wi alu, na pusren on lun mwet uh ac mwe on saya orek nwe ke firirla nukewa mwe kisa uh.
29 Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu.
Na Tokosra Hezekiah ac mwet nukewa sikukmutunte ac alu nu sin God.
30 Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.
Tokosra ac mwet kol lun mutunfacl sac elos fahk nu sin mwet Levi in onkakin on in kaksak ma David el simusla, oayapa ma Asaph mwet palu el simusla. Ouinge mwet nukewa on ke engan lulap ke elos sikukmutunte ac alu nu sin LEUM GOD.
31 Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.
Hezekiah el fahk nu sin mwet uh, “Inge ke kowos nasnasla tari, use mwe kisa tuh in mwe sang kulo nu sin LEUM GOD.” Na elos akos, ac kutu selos sifacna use kosro natulos ke insewowo lalos, tuh in mwe kisa firir.
32 Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana.
Elos use cow mukul itngoul, sheep siofok, ac sheep fusr luofoko, in mwe kisa firir nu sin LEUM GOD.
33 Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000.
Elos oayapa use cow mukul onfoko, ac tolu tausin sheep tuh in mwe kisa ma mwet uh in kang.
34 Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani.
Ke puelac mwet tol in mukena uniya kosro inge kewa, na mwet Levi elos kasrelos nwe ke na tari orekma kac. In pacl sacn oasr pac mwet tol su sifacna aknasnasyalosla. Mwet Levi elos oaru liki mwet tol in oru lumah fal nu ke aknasnas lalos uh.
35 Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa. Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya.
Sayen mwe kisa ma fonna firiryak, ma kunen mwet tol in esukak kiris ke ma kisakinyukla ke ma mwet uh kangla, oayapa in okoala wain ma wi na mwe kisa firir utuku. Ouinge alu in Tempul uh sifilpa mutawauk.
36 Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.
Tokosra Hezekiah ac mwet uh elos engan, mweyen God El kasrelos oru ma inge nukewa ke sie pacl na fototo.

< 2 Nyakati 29 >