< 2 Nyakati 29 >

1 Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
Therfor Ezechie bigan to regne, whanne he was of fyue and twenti yeer, and he regnede in Jerusalem nyne and twenti yeer; the name of his modir was Abia, the douytir of Zacharie.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.
And he dide that, that was pleasaunt in the siyt of the Lord, bi alle thingis whiche Dauid, his fadir, hadde do.
3 Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati.
In that yeer and the firste monethe of his rewme he openyde the yatis of the hows of the Lord, and restoride tho;
4 Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki
and he brouyte the preestis and dekenes, and gaderide hem in to the eest strete,
5 na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu.
and seide to hem, Sones of Leuy, here ye me, and be ye halewid; clense ye the hows of the Lord God of youre fadris; do ye awei al vnclennesse fro the seyntuarie.
6 Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao.
Oure fadris synneden, and diden yuel in the siyt of `oure Lord God, and forsoken hym; thei turneden awei her faces fro the tabernacle of `oure Lord God, and yauen the bak.
7 Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli.
Thei closiden the doris that weren in the porche, and quenchiden the lanternes; and thei brenten not encense, and thei offriden not brent sacrifices in the seyntuarie of God of Israel.
8 Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe.
Therfor the stronge veniaunce of the Lord was reisid on Juda and Jerusalem; and he yaf hem in to stiryng, and in to perischyng, and in to `hisshing, ether scornyng, as ye seen with youre iyen.
9 Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka.
Lo! oure fadris felden doun bi swerdis; oure sones, and oure douytris, and wyues ben led prisouneris for this greet trespas.
10 Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi.
Now therfor it plesith me, that we make a boond of pees with the Lord God of Israel, and that he turne fro vs the stronge veniaunce of his ire.
11 Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”
My sones, nyle ye be reccheles; the Lord hath chose you, that ye stonde bifor hym, and serue hym, that ye herie hym, and brenne encense to hym.
12 Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi: Kutoka kwa Wakohathi, Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria; kutoka kwa Wamerari, Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli; kutoka kwa Wagershoni, Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;
Therfor the dekenes risiden, Mahat, the sone of Amasie, and Johel, the sone of Azarie, of the sones of Caath; sotheli of the sones of Merarye, Cys, the sone of Abdai, and Azarie, the sone of Jelaleel; forsothe of the sones of Jerson, Joha, the sone of Zemma, and Hedem, the sone of Johaa;
13 kutoka kwa wana wa Elisafani, Shimri na Yeieli; kutoka kwa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
and sotheli of the sones of Elisaphan, Samri, and Jahiel; and of the sones of Asaph, Zacharie, and Mathanye;
14 kutoka kwa wana wa Hemani, Yehieli na Shimei; kutoka kwa wana wa Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
also of the sones of Heman, Jahiel, and Semei; but also of the sones of Iditum, Semei, and Oziel.
15 Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana.
And thei gaderiden to gidere her britheren, and weren halewid; and thei entriden bi comaundement of the kyng, and bi comaundement of the Lord, for to clense the hows of the Lord.
16 Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni.
Also preestis entriden in to the temple of the Lord, for to halewe it, and thei baren out al vnclennesse, which thei founden ther ynne in the porche, `ethir large place, of the hows of the Lord; which vnclennesse the dekenes token, and baren out to the stronde of Cedron with outforth.
17 Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.
Sotheli thei bigunnen to clense in the firste dai of the firste monethe, and in the eiyte dai of the same monethe thei entriden in to the porche of the hows of the Lord, and thei clensiden the temple eiyte daies; and in the sixtenthe dai of the same monethe thei filliden that, that thei hadden bigunne.
18 Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.
And thei entriden to Ezechie, the king, and seiden to hym, We han halewid al the hows of the Lord, and the auter of brent sacrifice therof, and the vessels therof, also and the boord of settyngforth with alle hise vessels,
19 Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”
and al the purtenaunce of the temple, `which purtenaunce king Achaz hadde defoulid in his rewme, aftir that he brak the lawe; and lo! alle thingis ben set forth bifor the auter of the Lord.
20 Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana.
And Ezechie, the kyng, roos in the morwetid, and gaderide togidere alle the princes of the citee, and stiede in to the hows of the Lord;
21 Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana.
and thei offriden togidere seuene bolis, and seuene rammes, seuene lambren, and seuene buckis of geet, for synne, for the rewme, for the seyntuarye, and for Juda. And he seide to preestis, the sones of Aaron, that thei schulden offre on the auter of the Lord.
22 Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu.
Therfor thei killiden bolis, and `the preestis tooken the blood, and schedden it on the auter; also thei killiden rammes, and `the preestis schedden the blood of tho on the auter; thei offriden lambren, and `the preestis schedden the blood on the auter.
23 Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu.
And thei brouyten buckis of geet `for synne bifor the kyng and al the multitude, and thei settiden her hondis on tho;
24 Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.
and the preestis offriden tho, and spreynten the blood of tho bifor the auter, for the clensyng of al Israel. For the king comaundide, that brent sacrifice shulde be made for al Israel, and for synne.
25 Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake.
Also he ordeynede dekenes in the hows of the Lord, with cymbalis, and sawtrees, and harpis, bi the ordenaunce of `Dauid the kyng, and of Gad, the profete, and of Nathan, the profete; for it was the comaundement of the Lord bi the hond of hise prophetis.
26 Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.
And the dekenes stoden, and helden the orguns of Dauid; and preestis helden trumpis.
27 Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli.
And Ezechie comaundide, that thei schulden offre brent sacrifices on the auter; and whanne brent sacrifices weren offrid, thei bigunnen to synge preisyngis to the Lord, and to sowne with trumpis, and in dyuerse orguns, whiche Dauid, the kyng of Israel, hadde maad redi for to sowne.
28 Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.
Forsothe whanne al the cumpenye worschipide, syngeris and thei that helden trumpis weren in her office, til the brent sacrifice was fillid.
29 Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu.
And whanne the offryng was endid, the kyng was bowid, and alle that weren with hym, and thei worschipiden God.
30 Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.
And Ezechie and the princes comaundiden to the dekenes, that thei schulden preise the Lord with the wordis of Dauith, and of Asaph, the profete; whiche preisiden hym with greet gladnesse, and kneliden, and worschipiden.
31 Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.
Sothely Ezechie addide also these thingis, Ye han fillid youre hondis to the Lord; neiye ye, and offre sacrifices and preisyngis in the hows of the Lord.
32 Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana.
Therfor al the multitude offride with deuoute soule sacrifices, and preisyngis, and brent sacrifices. Sotheli this was the noumbre of brent sacrifices, whiche the multitude offride; seuenti bolis, and an hundrid rammes, two hundrid lambren.
33 Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000.
Also thei halewiden to the Lord sixe hundrid oxis, and thre thousynde sheep.
34 Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani.
Forsothe the preestis weren fewe, and myyten not suffice for to `drawe awei the skynnes of brent sacrifices; wherfor and the dekenes her britheren helpiden hem, til the werk was fillid, and the preestis weren halewid; for the dekenes ben halewid bi liytere custom than the preestis.
35 Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa. Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya.
Therfor there weren ful many brent sacrifices, ynnere fatnessis of pesible sacrifices, and the moyste sacrifices of brent sacrifices, and the worschip, `ethir ournyng, of the `Lordis hows was fillid.
36 Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.
And Ezechie was glad, and al the puple, for the seruyce of the Lord was fillid; for it pleside, that this was doon sodeynly.

< 2 Nyakati 29 >