< 2 Nyakati 29 >

1 Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
Ezechiáš kralovati počal, když byl v pětmecítma letech, a dvadceti devět let kraloval v Jeruzalémě. Jméno matky jeho bylo Abia dcera Zachariášova.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.
A činil to, což pravého bylo před očima Hospodinovýma, podlé všech věcí, kteréž činil David otec jeho.
3 Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati.
On prvního léta kralování svého měsíce prvního otevřel dvéře domu Hospodinova, a opravil je.
4 Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki
Uvedl také kněží a Levíty, shromáždiv je do ulice východní,
5 na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu.
A řekl jim: Slyšte mne, Levítové. Nyní posvěťte se, posvěťte také i domu Hospodina Boha otců vašich, a vyneste nečistotu z svatyně.
6 Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao.
Neboť zhřešili otcové naši, a činili zlé věci před očima Hospodina Boha našeho, opouštějíce jej, a odvracujíce tvář svou od stánku Hospodinova, obracejíce se hřbetem k němu.
7 Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli.
Zavřeli také dvéře síně, a zhasili lampy, a kadidlem nekadili, aniž zápalu obětovali v svatyni Bohu Izraelskému.
8 Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe.
Protož rozhněval se Hospodin na Judu a na Jeruzalém, a vydal je v posmýkání, zpuštění a ku podivení, jakož sami očima svýma vidíte.
9 Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka.
A aj, padli otcové naši od meče, a synové naši i dcery naše a manželky naše zajaty jsou pro tu příčinu.
10 Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi.
Nyní tedy umínil jsem učiniti smlouvu s Hospodinem Bohem Izraelským, aby odvrátil od nás hněv prchlivosti své.
11 Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”
Synové moji, nebluďtež již. Vásť jest zajisté vyvolil Hospodin, abyste stojíce před ním, sloužili jemu, a byli služebníci jeho, a kadili.
12 Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi: Kutoka kwa Wakohathi, Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria; kutoka kwa Wamerari, Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli; kutoka kwa Wagershoni, Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;
Tedy povstali Levítové tito: Machat syn Amazai, a Joel syn Azariášův z synů Kahat; z synů pak Merari: Cis syn Abdi, a Azariáš syn Jehalleelův; a z Gersonitských: Joach syn Zimma, a Eden syn Joachův;
13 kutoka kwa wana wa Elisafani, Shimri na Yeieli; kutoka kwa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
Též z synů Elizafanových: Simri a Jehiel; z synů pak Azafových: Zachariáš a Mataniáš;
14 kutoka kwa wana wa Hemani, Yehieli na Shimei; kutoka kwa wana wa Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
A z synů Hémanových: Jechiel a Simei; z synů pak Jedutunových: Semaiáš a Uziel.
15 Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana.
I shromáždili bratří své, kteříž posvětivše se, přišli podlé rozkázaní králova a slov Hospodinových, aby vyčistili dům Hospodinův.
16 Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni.
A všedše kněží do domu Hospodinova, aby jej vyčistili, vynesli všelikou nečistotu, kterouž našli v chrámě Hospodinově, do síně domu Hospodinova. Levítové pak probravše to, vynesli ven ku potoku Cedron.
17 Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.
Začali pak prvního dne měsíce prvního posvěcovati, a dne osmého téhož měsíce vešli do síně Hospodinovy, a posvěcovali domu Hospodinova za osm dní, a dne šestnáctého měsíce prvního dokonali.
18 Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.
Tedy vešli k Ezechiášovi králi, a řekli: Vyčistili jsme všecken dům Hospodinův, i oltář zápalu, i všecky nádoby jeho, i stůl předložení a všecky nádoby jeho.
19 Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”
Všecky také nádoby, kteréž byl zavrhl král Achas za kralování svého, když převráceně činil, připravili jsme a posvětili, a aj, jsou před oltářem Hospodinovým.
20 Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana.
Potom vstav ráno Ezechiáš král, shromáždil úředníky města, a vstoupil do domu Hospodinova.
21 Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana.
A přivedli volků sedm, a skopců sedm, a beránků sedm, a kozlů sedm za hřích, za království, a za svatyni, a za Judu; a rozkázal synům Aronovým kněžím, aby obětovali na oltáři Hospodinovu.
22 Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu.
Takž zbili voly ty, a kněží berouce krev jejich, kropili na oltář. Zbili též i skopce a pokropovali krví jejich oltáře; zbili také i beránky, a krví jejich kropili na oltář.
23 Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu.
Přivedli i kozly k oběti za hřích před krále i shromáždění, kteřížto vložili ruce své na ně.
24 Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.
I zbili je kněží a vyčistili krví jejich oltář k očištění všeho Izraele; nebo za všecken lid Izraelský rozkázal král obětovati zápal a oběti za hřích.
25 Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake.
Postavil zase i Levíty v domě Hospodinově s cymbály, loutnami a harfami podlé rozkázaní Davidova, a Gáda proroka královského, a Nátana proroka; nebo od Hospodina bylo to přikázáno skrze proroky jeho.
26 Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.
A tak stáli Levítové s nástroji Davidovými a kněží s trubami.
27 Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli.
I rozkázal Ezechiáš, aby obětovali zápal na oltáři. A když se začala obět zápalná, začal se zpěv Hospodinův a troubení i zpěvové na nástroje Davida, krále Izraelského.
28 Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.
Všecko pak shromáždění klanělo se, když zpěváci zpívali, a trubači troubili, a to vše, až se dokonal zápal.
29 Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu.
A když dokonali obětování zápalu, sklonili se král a všickni, kteříž byli s ním, a poklonu učinili.
30 Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.
Tedy přikázal Ezechiáš král i knížata Levítům, aby chválili Hospodina slovy Davidovými a Azafa proroka. I chválili s velikým veselím, a sklánějíce se, poklonu činili.
31 Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.
Potom mluvil Ezechiáš, řka: Nyní jste posvětili rukou svých Hospodinu. Přistupte, a přiveďte oběti vítězné a oběti chvály do domu Hospodinova. Protož přivodilo shromáždění to oběti vítězné a oběti chvály, ano i každý z srdce ochotného k zápalným obětem,
32 Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana.
Tak že počet obětí zápalných, kteréž přivedlo shromáždění to, byl volů sedmdesáte, skopců sto, beránků dvě stě, všecko to na obět zápalnou Hospodinu.
33 Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000.
Jiných pak věcí posvěcených bylo volů šest set, a ovec tři tisíce.
34 Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani.
Kněží však bylo málo, tak že nemohli postačiti vytahovati z koží všech obětí zápalných. Pročež pomáhali jim bratří jejich Levítové, až i dokonali dílo to, a dokudž se neposvětili jiní kněží; nebo Levítové byli hotovější ku posvěcení se, nežli kněží.
35 Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa. Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya.
K tomu k zápalům bylo množství veliké tuků z obětí pokojných a obětí mokrých, kromě jiných zápalů. A tak vykonána byla služba domu Hospodinova.
36 Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.
A veselil se Ezechiáš i všecken lid, že Bůh byl nastrojil lid, tak aby se ta věc rychle spravila.

< 2 Nyakati 29 >