< 2 Nyakati 28 >

1 Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala. Akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana.
آحاز در سن بیست سالگی پادشاه شد و شانزده سال در اورشلیم سلطنت کرد. او مانند جدش داوود مطابق میل خداوند رفتار ننمود.
2 Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na pia akasubu sanamu kwa ajili ya kuabudu Mabaali.
آحاز به پیروی از پادشاهان اسرائیل، بتهای بعل را می‌پرستید.
3 Akatoa sadaka za kuteketezwa katika Bonde la Ben-Hinomu, na kuwatoa wanawe kafara kwa kuwateketeza kwa moto, akifuata njia za machukizo za yale mataifa Bwana aliyoyafukuza humo mbele ya Waisraeli.
او حتی به درهٔ هنوم رفت و نه فقط در آنجا برای بتها بخور سوزاند، بلکه پسران خود را نیز زنده‌زنده سوزانیده و قربانی بتها کرد. این رسم قومهایی بود که خداوند سرزمینشان را از آنها گرفته، به بنی‌اسرائیل داده بود.
4 Akatoa sadaka na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
آحاز در بتخانه‌های روی تپه‌ها و بلندیها و زیر هر درخت سبز قربانی کرد و بخور سوزانید.
5 Kwa hiyo Bwana Mungu wake akamtia mikononi mwa mfalme wa Aramu. Waaramu wakamshinda, wakachukua watu wake wengi mateka na kuwaleta mpaka Dameski. Tena alitiwa mikononi mwa mfalme wa Israeli, ambaye aliwaua watu wake wengi.
به همین علّت خداوند به پادشاه سوریه اجازه داد او را شکست دهد و عده زیادی از قومش را اسیر کرده، به دمشق ببرد. سربازان اسرائیل نیز عدهٔ زیادی از سربازان آحاز را کشتند.
6 Kwa siku moja Peka mwana wa Remalia aliwaua askari 120,000 katika Yuda, kwa kuwa Yuda walikuwa wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao.
فقح (پسر رملیا)، پادشاه اسرائیل در یک روز صد و بیست هزار نفر از سربازان یهودا را کشت زیرا مردم یهودا از خداوند، خدای اجدادشان برگشته بودند.
7 Zikri, askari shujaa Mwefraimu, akamuua Maaseya mwana wa mfalme, Azrikamu mkuu wa jumba la kifalme na Elikana aliyekuwa wa pili kwa mfalme.
سپس یک جنگاور اسرائیلی از اهالی افرایم به نام زکری، معسیا پسر آحاز و عزریقام سرپرست امور دربار و القانه را که شخص دوم مملکت بود به قتل رساند.
8 Waisraeli wakawachukua mateka kutoka ndugu zao, watu wapatao 200,000 hawa wakiwa ni wanawake, watoto wa kiume na wa kike. Wakachukua pia kiasi kikubwa cha nyara, ambazo walirudi nazo Samaria.
سپاهیان اسرائیل نیز دویست هزار زن و بچهٔ یهودی را اسیر کرده، با غنیمت فراوانی که به چنگ آورده بودند به سامره پایتخت اسرائیل بردند.
9 Lakini kulikuwako huko nabii wa Bwana aliyeitwa Odedi, akaondoka ili kukutana na jeshi liliporejea Samaria. Akawaambia, “Kwa kuwa Bwana, Mungu wa baba zenu, aliwakasirikia Yuda, aliwatia mikononi mwenu. Lakini mmewachinja kwa hasira ambayo imefika hadi mbinguni.
ولی عودید، نبی خداوند که در سامره بود به ملاقات سپاهیان اسرائیل که از جنگ بازمی‌گشتند رفت و به آنها گفت: «ببینید! خداوند، خدای اجداد شما بر یهودا خشمگین شد و گذاشت شما بر آنها پیروز شوید، ولی شما آنها را کشتید و نالهٔ آنها تا آسمان رسیده است.
10 Nanyi sasa mnakusudia kuwafanya wanaume na wanawake wa Yuda na Yerusalemu watumwa wenu. Lakini ninyi je, hamna pia hatia ya dhambi mliyotenda dhidi ya Bwana Mungu wenu?
حالا هم می‌خواهید این زنها و بچه‌ها را که از اورشلیم و یهودا آورده‌اید غلام و کنیز خود سازید. آیا فکر می‌کنید که خود شما بی‌تقصیر هستید و بر ضد خداوند، خدای خود گناه نکرده‌اید؟
11 Basi nisikilizeni! Mkawarudishe mateka mliowachukua kutoka kwa ndugu zenu, kwa kuwa hasira kali ya Bwana iko juu yenu.”
به حرف من گوش دهید و این اسیران را که بستگان خود شما هستند به خانه‌هایشان بازگردانید، زیرا هم اکنون آتش خشم خداوند بر شما شعله‌ور شده است.»
12 Ndipo baadhi ya viongozi katika Efraimu, yaani, Azaria mwana wa Yehohanani, Berekia mwana wa Meshilemothi, Yehizkia mwana wa Shalumu na Amasa mwana wa Hadlai, wakakubaliana na huyo nabii, hivyo wakawapinga wale waliokuwa wanawasili kutoka vitani.
بعضی از سران قبیلهٔ افرایم نیز با سپاهیانی که از جنگ بازگشته بودند مخالفت کردند. آنها عبارت بودند از: عزریا پسر یهوحانان، برکیا پسر مشلیموت، یحِزِقیا پسر شلوم و عماسا پسر حدلای.
13 Wakamwambia, “Hamna ruhusa kuwaleta hao wafungwa hapa, ama sivyo tutakuwa na hatia mbele za Bwana. Je, mnataka kuongezea dhambi yetu na hatia yetu? Kwa sababu hatia yetu tayari ni kubwa, nayo hasira kali ya Bwana iko juu ya Israeli.”
ایشان اعتراض‌کنان گفتند: «نباید این اسیران را به اینجا بیاورید. اگر این کار را بکنید ما در نظر خداوند مقصر خواهیم بود. آیا می‌خواهید به بار گناهان ما بیافزایید؟ ما به اندازهٔ کافی برای گناهانمان مورد خشم خدا قرار گرفته‌ایم.»
14 Hivyo wale askari wakawaacha wale mateka pamoja na nyara mbele ya hao maafisa na kusanyiko lote.
پس سپاهیان تمام اسیران و غنایمی را که آورده بودند به قوم خود و رهبرانشان واگذار کردند تا دربارهٔ آنها تصمیم بگیرند.
15 Kisha watu waliotajwa kwa majina wakawachukua wale mateka na kutoka zile nyara, wakachukua mavazi wakawavika wale wafungwa wote waliokuwa uchi. Wakawapatia nguo na viatu, chakula na cha kunywa, wakawapa matibabu, wote waliokuwa dhaifu miongoni mwao wakawapandisha juu ya punda, wakawaleta ndugu zao mpaka Yeriko, ndio Mji wa Mitende, kisha wakarudi Samaria.
آنگاه چهار نفری که قبلاً نامشان برده شد، لباسهای غنیمت گرفته شده را بین اسیران توزیع کردند و به آنها کفش، نان و آب دادند و زخمهای بیماران را بستند. سپس کسانی را که ضعیف بودند بر الاغ سوار کرده، آنها را به شهر اریحا که به شهر نخلستان معروف بود، نزد خانواده‌هایشان بردند و خود به سامره بازگشتند.
16 Wakati ule, Mfalme Ahazi akatuma wajumbe kwa mfalme wa Ashuru kuomba msaada.
در آن زمان، آحاز پادشاه یهودا از پادشاه آشور کمک طلبید.
17 Waedomu walikuwa wamekuja tena na kuwashambulia Yuda na kuchukua mateka.
زیرا لشکر اَدوم دوباره یهودا را تسخیر کرده، عده‌ای را به اسارت برده بود.
18 Pia Wafilisti walikuwa wameshambulia miji iliyokuwa chini ya vilima na katika miji ya Negebu ya Yuda. Nao wakawa wametwaa Beth-Shemeshi, Aiyaloni, Gederothi, Soko pamoja na vijiji vyake, Timna pamoja na vijiji vyake, Gimzo pia pamoja na vijiji vyake na kuishi humo.
در ضمن فلسطینی‌ها نیز به شهرهایی که در دشتهای یهودا و در جنوب این سرزمین بودند هجوم آوردند و بیت‌شمس، ایلون، جدیروت، سوکو، تمنه، جمزو و روستاهای اطراف آنها را گرفتند و در آنها ساکن شدند.
19 Bwana aliishusha Yuda kwa sababu ya Ahazi mfalme wa Israeli, kwa kuwa alikuwa ameongeza uovu katika Yuda na kumkosea Bwana mno.
خداوند به سبب آحاز، یهودا را دچار مصیبت کرد، زیرا آحاز نسبت به خداوند گناه ورزید و یهودا را نیز به گناه کشاند.
20 Hivyo Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru akaja kumtesa badala ya kumsaidia.
اما وقتی تغلت فلاسر، پادشاه آشور آمد، به جای کمک به آحاز پادشاه، موجب ناراحتی و دردسر او شد.
21 Ahazi akachukua baadhi ya vitu kutoka Hekalu la Bwana, jumba la kifalme na kutoka kwa wakuu wake na kumpa mfalme wa Ashuru kama ushuru, lakini hilo halikumsaidia.
هر چند آحاز طلا و نقرهٔ خانهٔ خداوند، خزانه‌های کاخ سلطنتی و خانه‌های سران قوم را به پادشاه آشور داد، ولی فایده‌ای نداشت.
22 Katika wakati wake wa mateso Mfalme Ahazi akazidi kukosa uaminifu kwa Bwana.
آحاز با وجود تمام این مشکلات، بیش از پیش نسبت به خداوند گناه ورزید.
23 Akatoa kafara kwa miungu ya Dameski, waliokuwa wamemshinda, kwa kuwa aliwaza, “Kwa kuwa miungu ya mfalme wa Aramu imewasaidia wao, nitaitolea dhabihu ili inisaidie na mimi.” Lakini haya ndiyo yaliyokuwa maangamizi yake na Israeli wote.
او برای بتهای سوریه قربانی نمود زیرا فکر می‌کرد این بتها سوری‌ها را کمک کرده‌اند تا او را شکست دهند. پس او هم برای آنها قربانی کرد تا او را یاری کنند. ولی همین بتها باعث نابودی آحاز و تمام قوم او شدند.
24 Ahazi akakusanya pamoja vyombo vya nyumba ya Mungu na kuvivunja vipande vipande. Akafunga milango ya Hekalu la Bwana na kusimamisha madhabahu katika kila njia panda ya barabara za Yerusalemu.
آحاز ظروف و لوازم خانهٔ خدا را گرفته، در هم کوبید و درهای خانهٔ خداوند را بست تا دیگر کسی در آنجا عبادت نکند و در هر گوشهٔ اورشلیم برای بتها مذبح بنا کرد.
25 Katika kila mji wa Yuda akajenga mahali pa juu pa kuabudia miungu ili kutolea miungu mingine kafara za kuteketezwa na kuchochea hasira ya Bwana, Mungu wa baba zake.
در هر یک از شهرهای یهودا بتکده‌هایی بر بالای تپه‌ها ساخت و برای بتها بخور سوزانید و به این طریق خشم خداوند، خدای اجدادش را برانگیخت.
26 Matukio mengine ya utawala wake na njia zake nyingine zote, tangu mwanzo hadi mwisho, zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
شرح بقیهٔ رویدادهای دوران سلطنت آحاز و کارهای او، از ابتدا تا انتها، در کتاب «تاریخ پادشاهان یهودا و اسرائیل» نوشته شده است.
27 Ahazi akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Yerusalemu, lakini hawakumleta kwenye makaburi ya wafalme wa Israeli. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.
وقتی آحاز مرد، او را در شهر اورشلیم دفن کردند، اما نه در آرامگاه سلطنتی. سپس پسرش حِزِقیا بر تخت سلطنت نشست.

< 2 Nyakati 28 >