< 2 Nyakati 27 >

1 Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Jotám je bil star petindvajset let, ko je začel kraljevati in v Jeruzalemu je kraljeval šestnajst let. Ime njegove matere je bilo Jerúša, Cadókova hči.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
Delal je to, kar je bilo pravilno v Gospodovih očeh, glede na vse to, kar je delal njegov oče Uzíjah. Vendar ni vstopil v Gospodov tempelj. Ljudstvo pa je še počelo izprijeno.
3 Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
Zgradil je visoka velika vrata Gospodove hiše in na obzidju Ofele je mnogo gradil.
4 Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
Poleg tega je zgradil mesta v Judovih gorah in v gozdovih je zgradil gradove in stolpe.
5 Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
Boril se je tudi s kraljem Amóncev in prevladal zoper njih. Amónovi otroci so mu isto leto dali sto talentov srebra, sto tisoč mer pšenice in deset tisoč [mer] ječmena. Toliko so mu Amónovi otroci plačali tako drugo leto kakor tretje leto.
6 Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
Tako je Jotám postal mogočen, ker je pripravil svoje poti pred Gospodom, svojim Bogom.
7 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
Torej preostala izmed Jotámovih dejanj in vse njegove vojne in njegove poti, glej, zapisane so v knjigi Izraelovih in Judovih kraljev.
8 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
Star je bil petindvajset let, ko je začel kraljevati in v Jeruzalemu je kraljeval šestnajst let.
9 Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jotám je zaspal s svojimi očeti in pokopali so ga v Davidovem mestu in namesto njega je zakraljeval njegov sin Aház.

< 2 Nyakati 27 >