< 2 Nyakati 27 >

1 Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Tinha Jothão vinte e cinco anos de idade, quando começou a reinar, e dezeseis anos reinou em Jerusalém: e era o nome de sua mãe Jerusa, filha de Zadok.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
E fez o que era reto aos olhos do Senhor, conforme a tudo o que fizera Uzias, seu pai, exceto que não entrou no templo do Senhor. E ainda o povo se corrompia.
3 Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
Este edificou a porta alta da casa do Senhor, e também edificou muito sobre o muro d'Ophel.
4 Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
Também edificou cidades nas montanhas de Judá, e edificou nos bosques castelos e torres.
5 Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
Ele também guerreou contra o rei dos filhos de Ammon, e prevaleceu sobre eles, de modo que os filhos de Ammon naquele ano lhe deram cem talentos de prata, e dez mil coros de trigo, e dez mil de cevada: isto lhe trouxeram os filhos de Ammon também o segundo e o terceiro ano.
6 Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
Assim se fortificou Jothão, porque dirigiu os seus caminhos na presença do Senhor seu Deus.
7 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
O resto pois dos sucessos de Jothão, e todas as suas guerras e os seus caminhos eis que está escrito no livro dos reis de Israel e de Judá.
8 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
Tinha vinte e cinco anos de idade, quando começou a reinar, e dezeseis anos reinou em Jerusalém.
9 Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
E dormiu Jothão com seus pais, e o sepultaram na cidade de David: e Achaz, seu filho, reinou em seu lugar.

< 2 Nyakati 27 >