< 2 Nyakati 27 >

1 Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Jotham [was] twenty and five years old when he began to reign and he reigned sixteen years in Jerusalem. His mother's name also [was] Jerushah, the daughter of Zadok.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
And he did [that which was] right in the sight of the LORD, according to all that his father Uzziah did: yet, he entered not into the temple of the LORD. And the people did yet corruptly.
3 Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
He built the high gate of the house of the LORD, and on the wall of Ophel he built much.
4 Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
Moreover, he built cities in the mountains of Judah, and in the forests he built castles and towers.
5 Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
He fought also with the king of the Ammonites, and prevailed against them. And the children of Ammon gave him the same year a hundred talents of silver, and ten thousand measures of wheat, and ten thousand of barley. So much did the children of Ammon pay to him, both the second year, and the third.
6 Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
So Jotham became mighty, because he prepared his ways before the LORD his God.
7 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
Now the rest of the acts of Jotham, and all his wars, and his ways, see, they [are] written in the book of the kings of Israel and Judah.
8 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
He was five and twenty years old when he began to reign, and reigned sixteen years in Jerusalem.
9 Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Jotham slept with his fathers, and they buried him in the city of David: and Ahaz his son reigned in his stead.

< 2 Nyakati 27 >