< 2 Nyakati 27 >
1 Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Jotham was twenty-five when he became king, and he reigned in for Jerusalem sixteen years. His mother's name was Jerushah, daughter of Zadok.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
He did what was right in the Lord's sight as his father Uzziah had done, and he did not enter the Lord's Temple as his father had. But the people still acted corruptly.
3 Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
Jotham rebuilt the Upper Gate of the Lord's Temple, and did extensive building work on the wall at Ophel.
4 Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
He built towns in the hill country of Judah, and fortresses and towers in the mountains and forests.
5 Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
Jotham fought with the king of the Ammonites and defeated them. The Ammonites gave him every year for three years one hundred talents of silver, and ten thousand cors of wheat and ten thousand of barley.
6 Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
Jotham grew powerful because he made sure what he did followed the ways of the Lord his God.
7 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
The rest of what Jotham did, his wars and other events, were written in the Book of the Kings of Israel and Judah.
8 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
He was twenty-five when he became king, and he reigned in Jerusalem for sixteen years.
9 Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jotham died and was buried in the City of David. His son Ahaz took over as king.