< 2 Nyakati 26 >
1 Kisha watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya mfalme mahali pa Amazia baba yake.
Wtedy cały lud Judy wziął Uzjasza, który miał szesnaście lat, i ustanowił go królem w miejsce jego ojca Amazjasza.
2 Ndiye alijenga upya Elathi kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
Ten odbudował Elat i przywrócił go do Judy, kiedy król już zasnął ze swoimi ojcami.
3 Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Uzjasz miał szesnaście lat, kiedy zaczął królować, i królował pięćdziesiąt dwa lata w Jerozolimie. Jego matka miała na imię Jekolia, [była] z Jerozolimy.
4 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
Czynił on to, co prawe w oczach PANA, według wszystkiego, co czynił jego ojciec Amazjasz.
5 Akamtafuta Mungu katika siku za Zekaria, aliyemwelekeza kumcha Mungu. Wakati wote alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.
I szukał Boga, dopóki żył Zachariasz, który miał rozeznanie w widzeniach Bożych. A przez te wszystkie dni, kiedy szukał PANA, Bóg darzył go powodzeniem.
6 Alipigana vita dhidi ya Wafilisti na kubomoa kuta za Gathi, Yabne na Ashdodi. Kisha akajenga upya miji karibu na Ashdodi na mahali pengine katikati ya Wafilisti.
Wyruszył do walki z Filistynami, zburzył mury Gat, Jabne i Aszdodu, a odbudował miasta w okolicy Aszdodu i [w ziemi] Filistynów.
7 Mungu akamsaidia dhidi ya Wafilisti na dhidi ya Waarabu walioishi Gur-Baali na dhidi ya Wameuni.
Wspomagał go bowiem Bóg [przeciw] Filistynom i Arabom, którzy mieszkali w Gur-Baal, i przeciw Meunitom.
8 Waamoni wakamletea Uzia ushuru, umaarufu wake ukaenea hadi kwenye mpaka wa Misri, kwa sababu alikuwa amekuwa na nguvu sana.
Ammonici dawali Uzjaszowi daniny, a [sława] jego imienia rozeszła się aż do wejścia do Egiptu, bo wielce się umocnił.
9 Uzia akajenga minara huko Yerusalemu katika Lango la Pembeni, katika Lango la Bondeni na katika pembe, mahali kuta zikutanapo, kisha akaijengea ngome.
I Uzjasz zbudował wieże w Jerozolimie nad Bramą Narożną, nad Bramą Doliny i nad Narożnikiem i umocnił je.
10 Akajenga pia minara jangwani na kuchimba visima vingi vya maji, kwa sababu alikuwa na mifugo mingi chini ya vilimani na kwenye nchi tambarare. Alikuwa na watu wanaofanya kazi katika mashamba yake na kwenye mashamba yake ya mizabibu huko vilimani na katika ardhi zenye rutuba, kwa kuwa aliupenda udongo.
Zbudował też wieże na pustyni i wykopał wiele studni, ponieważ miał bardzo dużo stad, zarówno w dolinach, jak i na równinach, także rolników i uprawiających winnice na górach i na Karmelu. Był bowiem rozmiłowany w uprawie ziemi.
11 Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililofunzwa vizuri, lililokuwa tayari kwenda vitani kwa vikosi kufuatana na idadi yao kama walivyokusanywa na Yeieli mwandishi na Maaseya msimamizi chini ya maelekezo ya Hanania, mmojawapo wa maafisa wa mfalme.
Uzjasz miał też wojsko [gotowe] do bitwy, które wyruszało na wojnę w odliczonych oddziałach, według spisu dokonanego przez pisarza Jejela i urzędnika Maasejasza, pod nadzorem Chananiasza, [jednego] z dowódców króla.
12 Idadi yote ya viongozi wa jamaa waliowaongoza hawa wapiganaji walikuwa 2,600.
Całkowita liczba naczelników rodów [postawionych] nad dzielnymi wojownikami wynosiła dwa tysiące sześciuset.
13 Chini ya uongozi wao kulikuwa na jeshi la askari 307,500 watu waliofundishwa kwa ajili ya vita, jeshi lenye nguvu la kumsaidia mfalme dhidi ya adui zake.
A pod ich rozkazami [stało] wojsko [złożone z] trzystu siedmiu tysięcy pięciuset wojowników gotowych do wojny z wielką siłą, aby wesprzeć króla przeciw wrogowi.
14 Uzia akalipatia jeshi lote ngao, mikuki, chapeo, dirii, pinde na mawe ya kombeo.
Uzjasz przygotował całemu wojsku tarcze, włócznie, hełmy, pancerze, łuki oraz kamienie do proc.
15 Huko Yerusalemu watu wenye utaalamu mkubwa wakatengeneza mitambo iliyotumika katika minara na kwenye pembe za ulinzi ili kurusha mishale na kuvurumisha mawe makubwa. Sifa zake zikaenea mbali sana kwa sababu alisaidiwa mno mpaka akawa na nguvu sana.
Sporządził w Jerozolimie machiny wojenne wymyślone przez zdolnych ludzi, aby stały na wieżach i na narożnikach w celu ciskania strzał i wielkich kamieni. Jego sława rozeszła się daleko, ponieważ doznawał cudownej pomocy, aż stał się potężny.
16 Lakini baada ya Uzia kuwa na nguvu sana, majivuno yake yakamsababishia kuanguka. Alikosa uaminifu kwa Bwana Mungu wake, naye akaingia hekaluni mwa Bwana ili afukize uvumba kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba.
Ale kiedy się umocnił, uniosło się jego serce ku jego własnej zgubie. Zgrzeszył przeciw PANU, swemu Bogu, gdyż wszedł do świątyni PANA, aby palić kadzidło na ołtarzu kadzenia.
17 Azaria kuhani akiwa pamoja na makuhani wengine themanini wa Bwana wenye ujasiri wakamfuata huko ndani.
Wszedł za nim kapłan Azariasz, a z nim osiemdziesięciu kapłanów PANA, odważnych mężczyzn.
18 Wakamkabili na kumwambia, “Siyo sawa kwako, Uzia, kumfukizia Bwana uvumba. Hiyo ni kazi ya makuhani, wazao wa Aroni, ambao wamewekwa wakfu ili kufukiza uvumba. Ondoka mahali patakatifu, kwa kuwa umekosa uaminifu nawe hutaheshimiwa na Bwana.”
I sprzeciwili się królowi Uzjaszowi, i powiedzieli mu: Nie do ciebie, Uzjaszu, należy palenie kadzidła PANU, lecz do kapłanów, synów Aarona, którzy są poświęceni, aby palić kadzidło. Wyjdź ze świątyni. Zgrzeszyłeś bowiem i nie [przynosi ci] to chwały od PANA Boga.
19 Uzia, ambaye alikuwa na chetezo mkononi mwake tayari kufukiza uvumba, akakasirika. Alipokuwa anawaghadhibikia makuhani mbele ya madhabahu ya kufukizia uvumba katika Hekalu la Bwana, ukoma ukamtokea penye kipaji chake cha uso.
Wtedy Uzjasz rozgniewał się, mając w ręku kadzielnicę, by spalić kadzidło. A gdy pałał gniewem na kapłanów, pojawił się trąd na jego czole przed kapłanami w domu PANA, przy ołtarzu kadzenia.
20 Azaria kuhani mkuu pamoja na makuhani wengine wote walipomtazama wakaona kwamba alikuwa na ukoma penye kipaji chake cha uso wakaharakisha kumtoa nje. Naam, hata yeye mwenyewe alikuwa anatamani kuondoka kwa sababu Bwana alikuwa amempiga.
Kiedy najwyższy kapłan Azariasz i wszyscy kapłani spojrzeli na niego, oto miał trąd na czole. Wypchnęli go więc stamtąd, a i on sam spieszył się z wyjściem, bo dotknął go PAN.
21 Mfalme Uzia alikuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Akatengwa katika nyumba ya pekee akiwa mwenye ukoma, naye akawa ametengwa kutoka Hekalu la Bwana. Yothamu mwanawe akawa msimamizi wa jumba la mfalme, pia akawaongoza watu wa nchi.
I tak król Uzjasz był trędowaty aż do dnia swojej śmierci i jako trędowaty mieszkał w domu odosobnienia. Został bowiem wyłączony z domu PANA. W tym czasie jego syn Jotam zarządzał domem królewskim i sądził lud ziemi.
22 Matukio mengine ya utawala wa Uzia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi.
A pozostałe dzieje Uzjasza, od pierwszych do ostatnich, opisał prorok Izajasz, syn Amosa.
23 Uzia akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika shamba la kuzikia lililokuwa mali ya wafalme, kwa kuwa watu walisema, “Alikuwa na ukoma.” Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Zasnął więc Uzjasz ze swoimi ojcami i pogrzebali go z nimi na polu grobów królewskich, gdyż mówili: Trędowaty jest. A jego syn Jotam królował w jego miejsce.