< 2 Nyakati 26 >
1 Kisha watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya mfalme mahali pa Amazia baba yake.
Tout le peuple de la terre prit alors Ozias, qui avait seize ans, et ils le proclamèrent roi à la place d'Amasias, son père.
2 Ndiye alijenga upya Elathi kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
Il rebâtit Elath, et la rendit à Juda lorsque le roi se fut endormi avec ses pères.
3 Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Ozias avait seize ans quand il monta sur le trône, et il régna cinquante- deux ans à Jérusalem; sa mère s'appelait Jéchélie de Jérusalem.
4 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
Et il fit ce qui est droit devant le Seigneur, comme avait fait d'abord Amasias, son père.
5 Akamtafuta Mungu katika siku za Zekaria, aliyemwelekeza kumcha Mungu. Wakati wote alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.
Il chercha le Seigneur tant que vécut Zacharie, homme sage et craignant Dieu; tant qu'il vécut, Ozias chercha le Seigneur, et le Seigneur le fit prospérer.
6 Alipigana vita dhidi ya Wafilisti na kubomoa kuta za Gathi, Yabne na Ashdodi. Kisha akajenga upya miji karibu na Ashdodi na mahali pengine katikati ya Wafilisti.
Il se mit en campagne, combattit les Philistins, renversa les murs de Geth, les murs de Jabner, les murs d'Azot, et bâtit des villes, près d'Azot, sur la terre des étrangers.
7 Mungu akamsaidia dhidi ya Wafilisti na dhidi ya Waarabu walioishi Gur-Baali na dhidi ya Wameuni.
Et le Seigneur le fortifia contre les Philistins, contre les Arabes qui habitent au milieu des rochers, et contre les Minéens.
8 Waamoni wakamletea Uzia ushuru, umaarufu wake ukaenea hadi kwenye mpaka wa Misri, kwa sababu alikuwa amekuwa na nguvu sana.
Alors, les Minéens lui firent des présents, et son nom se répandit jusqu'à l'entrée de l'Égypte; car il se fortifia extrêmement.
9 Uzia akajenga minara huko Yerusalemu katika Lango la Pembeni, katika Lango la Bondeni na katika pembe, mahali kuta zikutanapo, kisha akaijengea ngome.
Ozias bâtit aussi des tours dans Jérusalem: sur la porte de l'Angle, sur la porte de la Vallée, sur les angles, et il les fortifia.
10 Akajenga pia minara jangwani na kuchimba visima vingi vya maji, kwa sababu alikuwa na mifugo mingi chini ya vilimani na kwenye nchi tambarare. Alikuwa na watu wanaofanya kazi katika mashamba yake na kwenye mashamba yake ya mizabibu huko vilimani na katika ardhi zenye rutuba, kwa kuwa aliupenda udongo.
Et il bâtit des tours dans le désert, et il fit, en pierres de taille, une multitude de citernes, parce qu'il possédait de nombreux troupeaux dans les basses terres et dans la plaine, et il employait beaucoup de vignerons sur la montagne et sur le Carmel, car il était cultivateur.
11 Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililofunzwa vizuri, lililokuwa tayari kwenda vitani kwa vikosi kufuatana na idadi yao kama walivyokusanywa na Yeieli mwandishi na Maaseya msimamizi chini ya maelekezo ya Hanania, mmojawapo wa maafisa wa mfalme.
Son armée était aguerrie; au dehors, elle se rangeait en bataille; à l'intérieur, elle se déployait pour qu'on en fit la revue; ceux qui la dénombraient étaient le scribe Jehiel, le juge Maasias, et Ananias le lieutenant du roi.
12 Idadi yote ya viongozi wa jamaa waliowaongoza hawa wapiganaji walikuwa 2,600.
Le nombre des vaillants, chefs de familles, qui allaient en guerre, s'élevait à deux mille deux cents.
13 Chini ya uongozi wao kulikuwa na jeshi la askari 307,500 watu waliofundishwa kwa ajili ya vita, jeshi lenye nguvu la kumsaidia mfalme dhidi ya adui zake.
Et ils commandaient une armée aguerrie de trois cent soixante-dix mille cinq cents hommes, qui marchaient au combat, pleins de force et de vaillance, pour défendre le roi contre ses ennemis.
14 Uzia akalipatia jeshi lote ngao, mikuki, chapeo, dirii, pinde na mawe ya kombeo.
Ozias les avait tous armés de longs boucliers, de javelines, de casques, d'arcs et de frondes.
15 Huko Yerusalemu watu wenye utaalamu mkubwa wakatengeneza mitambo iliyotumika katika minara na kwenye pembe za ulinzi ili kurusha mishale na kuvurumisha mawe makubwa. Sifa zake zikaenea mbali sana kwa sababu alisaidiwa mno mpaka akawa na nguvu sana.
Et il fit exécuter à Jérusalem des machines, œuvres d'un habile calculateur, pour être sur les tours et sur les angles, ou pour lancer des traits ou de grosses pierres; partout, même au loin, on parla beaucoup de ses engins; car il en était merveilleusement secouru, et en tirait une grande force.
16 Lakini baada ya Uzia kuwa na nguvu sana, majivuno yake yakamsababishia kuanguka. Alikosa uaminifu kwa Bwana Mungu wake, naye akaingia hekaluni mwa Bwana ili afukize uvumba kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba.
Mais, comme il se fortifiait, son cœur s'enorgueillit pour sa perte; et il pécha contre le Seigneur son Dieu, et il entra dans le temple du Seigneur pour brûler de l'encens sur l'autel des parfums.
17 Azaria kuhani akiwa pamoja na makuhani wengine themanini wa Bwana wenye ujasiri wakamfuata huko ndani.
Et Azarias le prêtre y entra sur ses pas, accompagné de quatre-vingts prêtres du Seigneur, hommes intrépides.
18 Wakamkabili na kumwambia, “Siyo sawa kwako, Uzia, kumfukizia Bwana uvumba. Hiyo ni kazi ya makuhani, wazao wa Aroni, ambao wamewekwa wakfu ili kufukiza uvumba. Ondoka mahali patakatifu, kwa kuwa umekosa uaminifu nawe hutaheshimiwa na Bwana.”
Et ils s'arrêtèrent devant le roi Ozias, et ils lui dirent: Ce n'est pas à toi, Ozias, d'encenser le Seigneur, mais aux prêtres, fils d'Aaron, qui sont consacrés pour faire les sacrifices. Sors du Saint des saints, car tu t'es séparé du Seigneur, et cela ne tournera pas à ta gloire auprès de Dieu.
19 Uzia, ambaye alikuwa na chetezo mkononi mwake tayari kufukiza uvumba, akakasirika. Alipokuwa anawaghadhibikia makuhani mbele ya madhabahu ya kufukizia uvumba katika Hekalu la Bwana, ukoma ukamtokea penye kipaji chake cha uso.
Mais Ozias s'irrita; or, il avait à la main l'encensoir pour brûler de l'encens dans le temple, et, pendant qu'il s'irritait contre les prêtres, la lèpre parut sur son front, devant les prêtres dans le temple du Seigneur, au pied de l'autel des parfums.
20 Azaria kuhani mkuu pamoja na makuhani wengine wote walipomtazama wakaona kwamba alikuwa na ukoma penye kipaji chake cha uso wakaharakisha kumtoa nje. Naam, hata yeye mwenyewe alikuwa anatamani kuondoka kwa sababu Bwana alikuwa amempiga.
Et le grand prêtre Azarias et les prêtres, en se retournant vers lui, virent la lèpre sur son front; ils eurent hâte de le faire sortir, et lui-même n'était pas moins empressé, car le Seigneur l'avait châtié.
21 Mfalme Uzia alikuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Akatengwa katika nyumba ya pekee akiwa mwenye ukoma, naye akawa ametengwa kutoka Hekalu la Bwana. Yothamu mwanawe akawa msimamizi wa jumba la mfalme, pia akawaongoza watu wa nchi.
Le roi Ozias resta lépreux jusqu'au jour de sa mort; et lépreux, il demeura dans une maison isolée, parce qu'il avait été retranché du temple du Seigneur. Et Joatham, son fils, fut mis à la tête du royaume, jugeant le peuple de la terre.
22 Matukio mengine ya utawala wa Uzia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi.
Le reste des actes d'Ozias, les premiers et les derniers, ont été écrits par le prophète Jessé (Isaïe).
23 Uzia akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika shamba la kuzikia lililokuwa mali ya wafalme, kwa kuwa watu walisema, “Alikuwa na ukoma.” Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Ozias s'endormit avec ses pères, et on l'ensevelit auprès d'eux, dans le champ où est le sépulcre des rois, parce que, dirent-ils, il était lépreux. Et Joatham, son fils, régna à sa place.