< 2 Nyakati 26 >

1 Kisha watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya mfalme mahali pa Amazia baba yake.
Forsothe al the puple of Juda made kyng, Ozie, his sone, `of sixtene yeer, for his fader Amasie.
2 Ndiye alijenga upya Elathi kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
He bildide Hailath, and restoride it to the lordschipe of Juda, after that the kyng slepte with hise fadris.
3 Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Ozie was of sixtene yeer, whanne he bigan to regne; and he regnede two and fifti yeer in Jerusalem; the name of his modir was Hiechelia, of Jerusalem.
4 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
And he dide that, that was riytful in the siyt of the Lord, bi alle thingis whiche Amasie, his fadir, hadde do.
5 Akamtafuta Mungu katika siku za Zekaria, aliyemwelekeza kumcha Mungu. Wakati wote alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.
And he souyte the Lord in the daies of Zacarie, vndurstondynge and seynge God; and whanne he souyte God, God reulide hym in alle thingis.
6 Alipigana vita dhidi ya Wafilisti na kubomoa kuta za Gathi, Yabne na Ashdodi. Kisha akajenga upya miji karibu na Ashdodi na mahali pengine katikati ya Wafilisti.
Forsothe he yede out, and fauyt ayens Filisteis, and distriede the wal of Geth, and the wal of Jabyne, and the wal of Azotus; and he bildide stronge places in Azotus and in Filistiym.
7 Mungu akamsaidia dhidi ya Wafilisti na dhidi ya Waarabu walioishi Gur-Baali na dhidi ya Wameuni.
And the Lord helpide hym bothe ayens Filisteis, and ayens Arabeis that dwelliden in Garbahal, and ayenus Amonytis.
8 Waamoni wakamletea Uzia ushuru, umaarufu wake ukaenea hadi kwenye mpaka wa Misri, kwa sababu alikuwa amekuwa na nguvu sana.
Amonytis paieden yiftis to Ozie, and his name was pupplischid `til to the entryng of Egipt for ofte victories.
9 Uzia akajenga minara huko Yerusalemu katika Lango la Pembeni, katika Lango la Bondeni na katika pembe, mahali kuta zikutanapo, kisha akaijengea ngome.
And Ozie bildide touris in Jerusalem ouer the yate of the corner, and ouer the yate of the valey, and othere touris in the same side of the wal; and made tho stidefast.
10 Akajenga pia minara jangwani na kuchimba visima vingi vya maji, kwa sababu alikuwa na mifugo mingi chini ya vilimani na kwenye nchi tambarare. Alikuwa na watu wanaofanya kazi katika mashamba yake na kwenye mashamba yake ya mizabibu huko vilimani na katika ardhi zenye rutuba, kwa kuwa aliupenda udongo.
Also he bildide touris in the wildirnesse, and he diggide ful many cisternes; for he hadde many beestis as wel in the feeldi places as in the wastnesse of deseert. Also he hadde vyneris and tiliers of vynes in the hilles, and in Carmele; for he was a man youun to erthetilthe.
11 Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililofunzwa vizuri, lililokuwa tayari kwenda vitani kwa vikosi kufuatana na idadi yao kama walivyokusanywa na Yeieli mwandishi na Maaseya msimamizi chini ya maelekezo ya Hanania, mmojawapo wa maafisa wa mfalme.
Forsothe the oost of hise werriours, that yeden forth to batels, vndur the hond of Heiel, scribe, and of Masie, techere, and vndur the hond of Ananye that was of the duykis of the kyng;
12 Idadi yote ya viongozi wa jamaa waliowaongoza hawa wapiganaji walikuwa 2,600.
and al the noumbre of princes, by her meynees, was of stronge men two thousynde and sixe hundrid.
13 Chini ya uongozi wao kulikuwa na jeshi la askari 307,500 watu waliofundishwa kwa ajili ya vita, jeshi lenye nguvu la kumsaidia mfalme dhidi ya adui zake.
And vndur hem was al the oost, thre hundrid thousynde and seuen thousynde and fyue hundrid, that weren able to batel, and fouyten for the king ayens aduersaries.
14 Uzia akalipatia jeshi lote ngao, mikuki, chapeo, dirii, pinde na mawe ya kombeo.
And Ozie made redi to hem, that is, to al the oost, scheldis, and speris, and basynetis, and haburiouns, and bouwis, and slyngis to caste stonys.
15 Huko Yerusalemu watu wenye utaalamu mkubwa wakatengeneza mitambo iliyotumika katika minara na kwenye pembe za ulinzi ili kurusha mishale na kuvurumisha mawe makubwa. Sifa zake zikaenea mbali sana kwa sababu alisaidiwa mno mpaka akawa na nguvu sana.
And he made in Jerusalem engynes of dyuerse kynde, which he settide in touris, and in the corneris of wallis, that tho schulden caste arowis and grete stoonys; and his name yede out fer, for the Lord helpide hym, and hadde maad him strong.
16 Lakini baada ya Uzia kuwa na nguvu sana, majivuno yake yakamsababishia kuanguka. Alikosa uaminifu kwa Bwana Mungu wake, naye akaingia hekaluni mwa Bwana ili afukize uvumba kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba.
But whanne he was maad strong, his herte was reisid in to his perischyng; and he dispiside `his Lord God; and he entride in to the temple of the Lord, and wolde brenne encense on the auter of encense.
17 Azaria kuhani akiwa pamoja na makuhani wengine themanini wa Bwana wenye ujasiri wakamfuata huko ndani.
And anoon Azarie, the preest, entride after hym, and with hym the preestis of the Lord, seuenti `men ful noble;
18 Wakamkabili na kumwambia, “Siyo sawa kwako, Uzia, kumfukizia Bwana uvumba. Hiyo ni kazi ya makuhani, wazao wa Aroni, ambao wamewekwa wakfu ili kufukiza uvumba. Ondoka mahali patakatifu, kwa kuwa umekosa uaminifu nawe hutaheshimiwa na Bwana.”
whiche ayenstoden the kyng, and seiden, Ozie, it is not of thin office, that thou brenne encense to the Lord, but of the preestis of the Lord, that is, of the sones of Aaron, that ben halewid to siche seruyce; go thou out of the seyntuarye; dispise thou not; for this thing schal not be arettid of the Lord God to thee in to glorie.
19 Uzia, ambaye alikuwa na chetezo mkononi mwake tayari kufukiza uvumba, akakasirika. Alipokuwa anawaghadhibikia makuhani mbele ya madhabahu ya kufukizia uvumba katika Hekalu la Bwana, ukoma ukamtokea penye kipaji chake cha uso.
And Ozie was wrooth, and he helde in the hond the censere for to offre encence, and manaasside the preestis; and anoon lepre was sprungun forth in his forheed, bifor the preestis in the hows of the Lord on the auter of encense.
20 Azaria kuhani mkuu pamoja na makuhani wengine wote walipomtazama wakaona kwamba alikuwa na ukoma penye kipaji chake cha uso wakaharakisha kumtoa nje. Naam, hata yeye mwenyewe alikuwa anatamani kuondoka kwa sababu Bwana alikuwa amempiga.
And whanne Azarie, the bischop, hadde biholde hym, and alle othere preestis `hadden biholde him, thei sien lepre in his forheed, and hiyngli thei puttiden hym out; but also he was aferd, and hastide to go out; for he feelide anoon the veniaunce of the Lord.
21 Mfalme Uzia alikuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Akatengwa katika nyumba ya pekee akiwa mwenye ukoma, naye akawa ametengwa kutoka Hekalu la Bwana. Yothamu mwanawe akawa msimamizi wa jumba la mfalme, pia akawaongoza watu wa nchi.
Therfor kyng Ozie was leprouse `til to the dai of his deeth, and dwellide in an hows bi it silf, and he was ful of lepre; `for which he was cast out of the hows of the Lord. Forsothe Joathan, his sone, gouernyde the hows of the kyng, and demyde the puple of the lond.
22 Matukio mengine ya utawala wa Uzia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi.
Sotheli Ysaie, the prophete, the sone of Amos, wroot the residue `of the formere and of the laste wordis of Ozie.
23 Uzia akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika shamba la kuzikia lililokuwa mali ya wafalme, kwa kuwa watu walisema, “Alikuwa na ukoma.” Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Ozie slepte with hise fadris, and thei birieden not hym in the feeld of the kyngis sepulcris, for he was leprouse; and Joathan, his sone, regnyde for hym.

< 2 Nyakati 26 >