< 2 Nyakati 25 >

1 Amazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani kutoka Yerusalemu.
Amatsia avait vingt-cinq ans lorsqu'il devint roi, et il régna vingt-neuf ans à Jérusalem. Le nom de sa mère était Joaddan, de Jérusalem.
2 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kwa moyo wake wote.
Il fit ce qui est droit aux yeux de l'Éternel, mais pas avec un cœur parfait.
3 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
Et lorsque la royauté fut établie en sa faveur, il tua ses serviteurs qui avaient tué le roi son père.
4 Hata hivyo hakuwaua watoto wao, lakini akafanya sawasawa na ilivyoandikwa katika Sheria, katika Kitabu cha Mose, ambako Bwana aliamuru: “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
Mais il ne fit pas mourir leurs enfants, et il agit selon ce qui est écrit dans la loi, dans le livre de Moïse, comme Yahvé l'a ordonné, en disant: « Les pères ne mourront pas pour les enfants, et les enfants ne mourront pas pour les pères; mais chacun mourra pour son propre péché. »
5 Amazia akawaita watu wa Yuda pamoja, akawaweka chini ya majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia kufuatana na jamaa zao katika Yuda yote na Benyamini. Kisha akawahesabu wale wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na akakuta kwamba walikuwa wanaume 300,000 watu walio tayari kwa utumishi wa jeshi, walio na uwezo wa kutumia mkuki na ngao.
Amatsia rassembla Juda et les classa selon les maisons de leurs pères, sous les chefs de milliers et les chefs de centaines, tout Juda et Benjamin. Il les compta depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, et il trouva qu'il y avait trois cent mille hommes d'élite, capables d'aller à la guerre, sachant manier la lance et le bouclier.
6 Akawaajiri pia watu 100,000 wapiganaji kutoka Israeli kwa talanta 100 za fedha.
Il loua aussi cent mille hommes vaillants d'Israël pour cent talents d'argent.
7 Lakini mtu wa Mungu akamjia na kumwambia, “Ee mfalme, haya majeshi kutoka Israeli kamwe usiyaruhusu yaende pamoja na wewe kwa kuwa Bwana hayuko pamoja na Israeli, wala hayupo pamoja na yeyote wa watu wa Efraimu.
Un homme de Dieu vint lui dire: « O roi, ne laisse pas l'armée d'Israël aller avec toi, car Yahvé n'est pas avec Israël, avec tous les enfants d'Ephraïm.
8 Hata kama ukienda na kupigana kwa ujasiri katika vita, Mungu atakufanya ukimbie mbele ya adui, kwa kuwa Mungu anao uwezo wa kusaidia au wa kuangusha.”
Mais si tu veux y aller, agis, et sois fort pour la bataille. Dieu vous renversera devant l'ennemi, car Dieu a le pouvoir de secourir et de renverser. »
9 Amazia akamuuliza yule mtu wa Mungu, “Lakini itakuwaje kwa zile talanta 100 za fedha nilizolipa kwa ajili ya haya majeshi ya Israeli?” Yule mtu wa Mungu akajibu, “Bwana aweza kukupa zaidi sana ya hizo.”
Amatsia dit à l'homme de Dieu: « Mais que ferons-nous pour les cent talents que j'ai donnés à l'armée d'Israël? » L'homme de Dieu répondit: « Yahvé est capable de te donner beaucoup plus que cela. »
10 Hivyo Amazia akayaondoa yale majeshi yaliyokuwa yamekuja kutoka Efraimu na kuyarudisha nyumbani. Waliwakasirikia sana Yuda, nao wakarudi nyumbani wakiwa na hasira kali.
Alors Amatsia sépara l'armée qui était venue à lui d'Ephraïm, pour la renvoyer chez elle. C'est pourquoi leur colère s'enflamma contre Juda, et ils retournèrent chez eux avec fureur.
11 Ndipo Amazia akajitia nguvu na kuliongoza jeshi lake kwenye Bonde la Chumvi, ambako aliua watu 10,000 wa Seiri.
Amatsia prit courage, conduisit son peuple et alla dans la vallée du sel; il frappa dix mille hommes des fils de Séir.
12 Jeshi la Yuda pia likawateka watu 10,000 wakiwa hai, likawapandisha juu ya jabali na kuwatupa chini kwa nguvu hata wote wakavunjika vipande vipande.
Les enfants de Juda en emportèrent dix mille vivants, les amenèrent au sommet du rocher et les jetèrent du haut du rocher, de sorte qu'ils furent tous brisés en morceaux.
13 Wakati huo yale majeshi Amazia aliyoyarudisha na ambayo hakuyaruhusu kushiriki katika vita, yalivamia miji ya Yuda kuanzia Samaria hata Beth-Horoni. Yakawaua watu 3,000 na kuchukua kiasi kikubwa sana cha mateka.
Mais les hommes de l'armée qu'Amatsia avait renvoyés pour ne pas aller avec lui au combat, tombèrent sur les villes de Juda, depuis Samarie jusqu'à Beth Horon, en battirent trois mille et firent un grand pillage.
14 Amazia aliporudi kutoka kuwachinja Waedomu, alileta pia kutoka huko miungu ya watu wa Seiri. Akaisimamisha kama miungu yake mwenyewe, akaisujudia na kuitolea kafara za kuteketezwa.
Après qu'Amatsia fut revenu du massacre des Édomites, il fit venir les dieux des fils de Séir et les érigea en dieux, il se prosterna devant eux et leur offrit des parfums.
15 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Amazia, naye akamtuma nabii kwake, ambaye alisema: “Kwa nini unauliza kwa miungu ya hawa watu, ambayo haikuweza kuwaokoa watu wake wenyewe kutoka mkononi mwako?”
La colère de Yahvé s'enflamma contre Amatsia, et il lui envoya un prophète qui lui dit: « Pourquoi as-tu recherché les dieux de ces peuples qui n'ont pas délivré leur propre peuple de ta main? »
16 Wakati nabii alipokuwa angali anazungumza, mfalme akamwambia, “Je, wewe tumekuchagua kuwa mshauri wa mfalme? Nyamaza, ya nini uuawe?” Hivyo nabii akanyamaza lakini akasema, “Najua kuwa Mungu ameazimia kukuangamiza kwa sababu umefanya jambo hili na hukusikiliza shauri langu.”
Comme il parlait avec lui, le roi lui dit: « T'avons-nous fait un des conseillers du roi? Arrête! Pourquoi devrais-tu être frappé? » Le prophète s'arrêta et dit: « Je sais que Dieu a décidé de te détruire, parce que tu as fait cela et que tu n'as pas écouté mes conseils. »
17 Baada ya Amazia mfalme wa Yuda kushauriana na washauri wake akatuma ujumbe kwa Yehoashi, mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli kusema: “Njoo tukabiliane uso kwa uso.”
Alors Amatsia, roi de Juda, consulta ses conseillers et envoya dire à Joas, fils de Joachaz, fils de Jéhu, roi d'Israël: « Viens! Regardons-nous en face. »
18 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda, “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
Joas, roi d'Israël, envoya dire à Amatsia, roi de Juda: « Le chardon du Liban envoya dire au cèdre du Liban: « Donne ta fille pour femme à mon fils. Alors une bête sauvage qui était au Liban passa et piétina le chardon.
19 Wewe unasema moyoni mwako kwamba umemshinda Edomu, nawe sasa unajigamba na kujivuna. Lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini utafute matatizo na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
Tu te dis que tu as frappé Édom, et ton cœur te pousse à te glorifier. Maintenant, reste chez toi. Pourquoi te mêler à la détresse, pour que tu tombes, toi et Juda avec toi? ».
20 Hata hivyo, Amazia hakutaka kusikia, kwa kuwa Mungu alifanya hivyo ili awatie mikononi mwa Yehoashi, kwa sababu waliitafuta miungu ya Edomu.
Mais Amatsia ne voulut pas écouter, car c'était Dieu qui voulait les livrer entre les mains de leurs ennemis, parce qu'ils avaient recherché les dieux d'Édom.
21 Hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea kuwashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakabiliana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
Joas, roi d'Israël, monta, et lui et Amatsia, roi de Juda, se regardèrent en face à Beth Shemesh, qui appartient à Juda.
22 Yuda ikashindwa na Israeli na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
Juda fut vaincu par Israël, et chacun s'enfuit dans sa tente.
23 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akamleta Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
Joas, roi d'Israël, prit à Beth Shemesh Amatsia, roi de Juda, fils de Joas, fils de Joachaz, et l'amena à Jérusalem. Il abattit la muraille de Jérusalem depuis la porte d'Ephraïm jusqu'à la porte de l'angle, soit quatre cents coudées.
24 Akachukua dhahabu yote, fedha na vyombo vyote vilivyopatikana katika Hekalu la Mungu, ambavyo vilikuwa chini ya uangalizi wa Obed-Edomu, pamoja na hazina za jumba la mfalme na mateka, kisha akarudi Samaria.
Il prit tout l'or et l'argent, tous les objets qui se trouvaient dans la maison de Dieu avec Obed-Edom, les trésors de la maison du roi et les otages, et il retourna à Samarie.
25 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
Amatsia, fils de Joas, roi de Juda, vécut quinze ans après la mort de Joas, fils de Joachaz, roi d'Israël.
26 Kwa habari ya matukio mengine katika utawala wa Amazia, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na wa Israeli?
Le reste des actes d'Amatsia, les premiers et les derniers, ne sont-ils pas écrits dans le livre des rois de Juda et d'Israël?
27 Kuanzia wakati ule Amazia alipogeuka na kuacha kumfuata Bwana walifanya shauri baya dhidi yake huko Yerusalemu naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi nao wakamuulia huko.
Depuis qu'Amatsia s'est détourné de Yahvé, on a formé une conspiration contre lui à Jérusalem. Il s'enfuit à Lakis, mais ils le poursuivirent à Lakis et l'y tuèrent.
28 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Yuda.
On le fit monter sur des chevaux et on l'enterra avec ses pères dans la ville de Juda.

< 2 Nyakati 25 >