< 2 Nyakati 25 >
1 Amazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani kutoka Yerusalemu.
Amaziah was twenty-five years old when he began to reign; he reigned twenty-nine years in Jerusalem. His mother's name was Jehoaddan, of Jerusalem.
2 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kwa moyo wake wote.
He did what was right in the eyes of Yahweh, but not with a whole heart.
3 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
It came about that as soon as his rule was well established, he killed the servants who had murdered his father, the king.
4 Hata hivyo hakuwaua watoto wao, lakini akafanya sawasawa na ilivyoandikwa katika Sheria, katika Kitabu cha Mose, ambako Bwana aliamuru: “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
But he did not put the children of the murderers to death, but acted according to what was written in the law, in the Book of Moses, as Yahweh had commanded, “The fathers must not die for the children, nor must the children die for the fathers. Instead, every person must die for his own sin.”
5 Amazia akawaita watu wa Yuda pamoja, akawaweka chini ya majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia kufuatana na jamaa zao katika Yuda yote na Benyamini. Kisha akawahesabu wale wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na akakuta kwamba walikuwa wanaume 300,000 watu walio tayari kwa utumishi wa jeshi, walio na uwezo wa kutumia mkuki na ngao.
Moreover, Amaziah gathered Judah together, and registered them by their ancestors' houses, under commanders of thousands and commanders of hundreds—all of Judah and Benjamin. He numbered them from twenty years old and upward, and found them to be 300,000 chosen men, able to go to war, who could handle spear and shield.
6 Akawaajiri pia watu 100,000 wapiganaji kutoka Israeli kwa talanta 100 za fedha.
He hired also 100,000 fighting men from Israel for one hundred talents of silver.
7 Lakini mtu wa Mungu akamjia na kumwambia, “Ee mfalme, haya majeshi kutoka Israeli kamwe usiyaruhusu yaende pamoja na wewe kwa kuwa Bwana hayuko pamoja na Israeli, wala hayupo pamoja na yeyote wa watu wa Efraimu.
But a man of God came to him and said, “King, do not let the army of Israel go with you, for Yahweh is not with Israel—none of the people of Ephraim.
8 Hata kama ukienda na kupigana kwa ujasiri katika vita, Mungu atakufanya ukimbie mbele ya adui, kwa kuwa Mungu anao uwezo wa kusaidia au wa kuangusha.”
But even if you do go and are courageous and strong in battle, God will throw you down before the enemy, for God has power to help, and power to throw down.”
9 Amazia akamuuliza yule mtu wa Mungu, “Lakini itakuwaje kwa zile talanta 100 za fedha nilizolipa kwa ajili ya haya majeshi ya Israeli?” Yule mtu wa Mungu akajibu, “Bwana aweza kukupa zaidi sana ya hizo.”
Amaziah said to the man of God, “But what will we do about the one hundred talents that I have given to the army of Israel?” The man of God answered, “Yahweh is able to give you much more than that.”
10 Hivyo Amazia akayaondoa yale majeshi yaliyokuwa yamekuja kutoka Efraimu na kuyarudisha nyumbani. Waliwakasirikia sana Yuda, nao wakarudi nyumbani wakiwa na hasira kali.
So Amaziah separated the army that had come to him from Ephraim; he sent them home again. So their anger was greatly kindled against Judah, and they returned home in fierce anger.
11 Ndipo Amazia akajitia nguvu na kuliongoza jeshi lake kwenye Bonde la Chumvi, ambako aliua watu 10,000 wa Seiri.
Amaziah took courage and led his people to go out to the Valley of Salt; there he defeated ten thousand men of Seir.
12 Jeshi la Yuda pia likawateka watu 10,000 wakiwa hai, likawapandisha juu ya jabali na kuwatupa chini kwa nguvu hata wote wakavunjika vipande vipande.
The army of Judah carried away alive another ten thousand. They took them to the top of the cliff and threw them down from there, so that they were all broken in pieces.
13 Wakati huo yale majeshi Amazia aliyoyarudisha na ambayo hakuyaruhusu kushiriki katika vita, yalivamia miji ya Yuda kuanzia Samaria hata Beth-Horoni. Yakawaua watu 3,000 na kuchukua kiasi kikubwa sana cha mateka.
But the men of the army which Amaziah sent back, so that they should not go with him to battle, attacked the cities of Judah from Samaria to Beth Horon. They struck down three thousand of the people and took much plunder.
14 Amazia aliporudi kutoka kuwachinja Waedomu, alileta pia kutoka huko miungu ya watu wa Seiri. Akaisimamisha kama miungu yake mwenyewe, akaisujudia na kuitolea kafara za kuteketezwa.
Now it came about, after that Amaziah had returned from the slaughter of the Edomites, that he brought the gods of the people of Seir, and set them up to be his own gods. He bowed down before them and burned incense to them.
15 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Amazia, naye akamtuma nabii kwake, ambaye alisema: “Kwa nini unauliza kwa miungu ya hawa watu, ambayo haikuweza kuwaokoa watu wake wenyewe kutoka mkononi mwako?”
So Yahweh's anger was kindled against Amaziah. He sent a prophet to him, who said, “Why have you sought after the gods of a people who did not even save their own people from your hand?”
16 Wakati nabii alipokuwa angali anazungumza, mfalme akamwambia, “Je, wewe tumekuchagua kuwa mshauri wa mfalme? Nyamaza, ya nini uuawe?” Hivyo nabii akanyamaza lakini akasema, “Najua kuwa Mungu ameazimia kukuangamiza kwa sababu umefanya jambo hili na hukusikiliza shauri langu.”
It came about that as the prophet was speaking with him, the king said to him, “Have we made you an advisor to the king? Stop! Why should you be killed?” Then the prophet stopped and said, “I know that God has decided to destroy you because you have done this deed and have not listened to my advice.”
17 Baada ya Amazia mfalme wa Yuda kushauriana na washauri wake akatuma ujumbe kwa Yehoashi, mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli kusema: “Njoo tukabiliane uso kwa uso.”
Then Amaziah king of Judah consulted with advisors and sent messengers to Jehoash son of Jehoahaz son of Jehu, king of Israel, saying, “Come, let us meet each other face to face in battle.”
18 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda, “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
But Jehoash the king of Israel sent messengers back to Amaziah king of Judah, saying, “A thistle that was in Lebanon sent a message to a cedar in Lebanon, saying, 'Give your daughter to my son for a wife,' but a wild beast in Lebanon walked by and trampled down the thistle.
19 Wewe unasema moyoni mwako kwamba umemshinda Edomu, nawe sasa unajigamba na kujivuna. Lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini utafute matatizo na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
You have said, 'See, I have struck down Edom,' and your heart has lifted you up. Take pride in your victory, but stay at home, for why should you cause yourself trouble and fall, both you and Judah with you?”
20 Hata hivyo, Amazia hakutaka kusikia, kwa kuwa Mungu alifanya hivyo ili awatie mikononi mwa Yehoashi, kwa sababu waliitafuta miungu ya Edomu.
But Amaziah would not listen, because this event was from God, so he might put the people of Judah into the hand of their enemies, because they had sought advice from the gods of Edom.
21 Hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea kuwashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakabiliana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
So Jehoash, king of Israel, attacked; he and Amaziah, king of Judah, met each other face to face at Beth Shemesh, which belongs to Judah.
22 Yuda ikashindwa na Israeli na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
Judah was struck down before Israel, and every man fled home.
23 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akamleta Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
Jehoash, king of Israel, captured Amaziah son of Jehoash son of Ahaziah, king of Judah, at Beth Shemesh. He brought him to Jerusalem and tore down the wall of Jerusalem from the Ephraim Gate to the Corner Gate, four hundred cubits in distance.
24 Akachukua dhahabu yote, fedha na vyombo vyote vilivyopatikana katika Hekalu la Mungu, ambavyo vilikuwa chini ya uangalizi wa Obed-Edomu, pamoja na hazina za jumba la mfalme na mateka, kisha akarudi Samaria.
He took all the gold and silver, all the objects that were found in the house of God with Obed Edom, and the valuable things in the king's house, with hostages also, and returned to Samaria.
25 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
Amaziah son of Joash, king of Judah, lived fifteen years after the death of Jehoash, son of Jehoahaz, king of Israel.
26 Kwa habari ya matukio mengine katika utawala wa Amazia, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na wa Israeli?
As for the other matters concerning Amaziah, first and last, behold, are they not written in the book of the kings of Judah and Israel?
27 Kuanzia wakati ule Amazia alipogeuka na kuacha kumfuata Bwana walifanya shauri baya dhidi yake huko Yerusalemu naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi nao wakamuulia huko.
Now from the time that Amaziah turned away from following Yahweh, they began to make a conspiracy against him in Jerusalem. He fled to Lachish, but they sent men after him to Lachish and killed him there.
28 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Yuda.
They brought him back on horses and buried him with his ancestors in the city of Judah.