< 2 Nyakati 24 >

1 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka arobaini. Mama yake aliitwa Sibia aliyekuwa ametoka Beer-Sheba.
son: aged seven year Joash in/on/with to reign he and forty year to reign in/on/with Jerusalem and name mother his Zibiah from Beersheba Beersheba
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ya Yehoyada kuhani.
and to make: do Joash [the] upright in/on/with eye: appearance LORD all day Jehoiada [the] priest
3 Yehoyada akamwoza wake wawili, akazaa watoto wa kiume na wa kike.
and to lift: marry to/for him Jehoiada woman: wife two and to beget son: child and daughter
4 Baada ya muda, Yoashi akaamua kukarabati Hekalu la Bwana.
and to be after so to be with heart Joash to/for to renew [obj] house: temple LORD
5 Akawaita pamoja makuhani na Walawi akawaambia, “Nendeni katika miji ya Yuda mkakusanye fedha wanazopaswa kulipa kila mwaka kutoka kwa Israeli wote, ili kukarabati Hekalu la Mungu wenu. Fanyeni hivyo sasa.” Lakini Walawi hawakufanya upesi.
and to gather [obj] [the] priest and [the] Levi and to say to/for them to come out: come to/for city Judah and to gather from all Israel silver: money to/for to strengthen: strengthen [obj] house: temple God your from sufficiency year in/on/with year and you(m. p.) to hasten to/for word: thing and not to hasten [the] Levi
6 Kwa hiyo mfalme akamwita Yehoyada kuhani mkuu na kumwambia, “Kwa nini hukuwaambia Walawi walete kutoka Yuda na Yerusalemu kodi iliyowekwa na Mose mtumishi wa Bwana pamoja na kusanyiko la Israeli kwa ajili ya Hema ya Ushuhuda?”
and to call: call to [the] king to/for Jehoiada [the] head: leader and to say to/for him why? not to seek upon [the] Levi to/for to come (in): bring from Judah and from Jerusalem [obj] tribute Moses servant/slave LORD and [the] assembly to/for Israel to/for tent [the] testimony
7 Kwa kuwa wana wa yule mwanamke mwovu Athalia, walikuwa wamevunja na kuingia katika Hekalu la Mungu, nao wakawa wamevitumia hata vile vitu vilivyowekwa wakfu kwa Bwana kwa mabaali.
for Athaliah [the] wickedness son: child her to break through [obj] house: temple [the] God and also all holiness house: temple LORD to make to/for Baal
8 Kwa amri ya mfalme, likatengenezwa kasha, nalo likawekwa nje kwenye lango la Hekalu la Bwana.
and to say [the] king and to make ark one and to give: put him in/on/with gate house: temple LORD outside [to]
9 Tangazo likatolewa katika Yuda na Yerusalemu kwamba inapasa wamletee Bwana kodi ile ambayo Mose, mtumishi wa Bwana alikuwa amewaagiza Israeli huko jangwani.
and to give: make voice: message in/on/with Judah and in/on/with Jerusalem to/for to come (in): bring to/for LORD tribute Moses servant/slave [the] God upon Israel in/on/with wilderness
10 Maafisa wote na watu wote wakaleta michango yao kwa furaha, wakaweka kwenye kasha mpaka likajaa.
and to rejoice all [the] ruler and all [the] people and to come (in): bring and to throw to/for ark till to/for to end: finish
11 Ikawa kila wakati kasha lilipoletwa ndani na Walawi kwa maafisa wa mfalme na kuona kwamba kuna kiasi kikubwa cha fedha, mwandishi wa mfalme na afisa wa kuhani mkuu walikuwa wanakuja na kumimina, kisha kulirudisha mahali pake. Walifanya hivi mara kwa mara, nao wakakusanya fedha nyingi sana.
and to be in/on/with time to come (in): bring [obj] [the] ark to(wards) punishment [the] king in/on/with hand: by [the] Levi and like/as to see: see they for many [the] silver: money and to come (in): come secretary [the] king and overseer priest [the] head: leader and to uncover [obj] [the] ark and to lift: raise him and to return: return him to(wards) place his thus to make: do to/for day: daily in/on/with day: daily and to gather silver: money to/for abundance
12 Mfalme na Yehoyada wakawapa wale watu waliofanya kazi iliyotakiwa katika Hekalu la Bwana. Wakawaajiri waashi na maseremala ili kutengeneza Hekalu la Bwana, pia wafanyakazi za chuma na shaba ili kukarabati Hekalu la Bwana.
and to give: give him [the] king and Jehoiada to(wards) to make: do work service: ministry house: temple LORD and to be to hire to hew and artificer to/for to renew house: temple LORD and also to/for artificer iron and bronze to/for to strengthen: strengthen [obj] house: temple LORD
13 Watu walioshughulika na kazi walikuwa wenye bidii, nayo kazi ya kukarabati ikaendelea vizuri mikononi mwao. Wakalitengeneza upya Hekalu la Bwana likarudi katika hali yake ya awali na kuliimarisha.
and to make: do to make: do [the] work and to ascend: rise health to/for work in/on/with hand their and to stand: stand [obj] house: temple [the] God upon tally his and to strengthen him
14 Walipokamilisha kazi hiyo ya kukarabati, wakaleta fedha zilizobaki wakampa mfalme na Yehoyada, nao kwa hizo wakatengeneza vyombo kwa ajili ya Hekalu la Bwana: Vyombo kwa ajili ya huduma na kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia mabakuli na vitu vingine vya dhahabu na fedha. Wakati wote Yehoyada alipokuwa hai, sadaka za kuteketezwa zilitolewa wakati wote katika Hekalu la Bwana.
and like/as to end: finish they to come (in): bring to/for face: before [the] king and Jehoiada [obj] remnant [the] silver: money and to make him article/utensil to/for house: temple LORD article/utensil ministry and to ascend: offer up and palm: dish and article/utensil gold and silver: money and to be to ascend: offer up burnt offering in/on/with house: temple LORD continually all day Jehoiada
15 Basi Yehoyada alikuwa mzee aliyeshiba siku wakati alipofariki. Alikufa akiwa na umri wa miaka 130.
and be old Jehoiada and to satisfy day and to die son: aged hundred and thirty year in/on/with death his
16 Wakamzika pamoja na wafalme katika Mji wa Daudi, kwa sababu ya mema aliyokuwa ametenda katika Israeli kwa ajili ya Mungu na Hekalu lake.
and to bury him in/on/with city David with [the] king for to make: do welfare in/on/with Israel and with [the] God and house: home his
17 Baada ya kifo cha Yehoyada, wakuu wa Yuda walikuja kumpa mfalme heshima, naye akawasikiliza.
and after death Jehoiada to come (in): come ruler Judah and to bow to/for king then to hear: hear [the] king to(wards) them
18 Wakaacha Hekalu la Bwana, Mungu wa baba zao, wakaabudu nguzo za maashera na sanamu. Kwa sababu ya hatia yao, hasira ya Mungu ikawajia Yuda na Yerusalemu.
and to leave: forsake [obj] house: temple LORD God father their and to serve [obj] [the] Asherah and [obj] [the] idol and to be wrath upon Judah and Jerusalem in/on/with guiltiness their this
19 Ingawa Bwana aliwatuma manabii wawarudishe watu kwake na ingawa waliwaonya, hawakuwasikiliza.
and to send: depart in/on/with them prophet to/for to return: return them to(wards) LORD and to testify in/on/with them and not to listen
20 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya Zekaria mwana wa Yehoyada kuhani. Akasimama mbele ya watu akasema, “Hili ndilo asemalo Mungu, ‘Kwa nini mnakataa kuzitii amri za Bwana? Hamtafanikiwa kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi.’”
and spirit God to clothe [obj] Zechariah son: child Jehoiada [the] priest and to stand: stand from upon to/for people and to say to/for them thus to say [the] God to/for what? you(m. p.) to pass: trespass [obj] commandment LORD and not to prosper for to leave: forsake [obj] LORD and to leave: forsake [obj] you
21 Lakini wakafanya shauri baya juu yake na kwa amri ya mfalme wakampiga kwa mawe mpaka akafa katika ukumbi wa Hekalu la Bwana.
and to conspire upon him and to stone him stone in/on/with commandment [the] king in/on/with court house: temple LORD
22 Mfalme Yoashi hakukumbuka wema aliotendewa na Yehoyada baba yake Zekaria ila alimuua mwanawe, ambaye alisema wakati akiwa amelala akingojea kufa, “Bwana na alione hili na alipize kisasi.”
and not to remember Joash [the] king [the] kindness which to make: do Jehoiada father his with him and to kill [obj] son: child his and like/as to die he to say to see: see LORD and to seek
23 Mwishoni mwa ule mwaka, jeshi la Waaramu likaja dhidi ya Yoashi, likavamia Yuda na Yerusalemu na kuwaua viongozi wote wa watu. Wakapeleka nyara zao zote kwa mfalme wao huko Dameski.
and to be to/for circuit [the] year to ascend: rise upon him strength: soldiers Syria and to come (in): come to(wards) Judah and Jerusalem and to ruin [obj] all ruler [the] people from people and all spoil their to send: depart to/for king Damascus
24 Ingawa jeshi la Waaramu lilikuwa limekuja na watu wachache tu, Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa kuliko lao. Kwa sababu Yuda walikuwa wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, hukumu ilitekelezwa juu ya Yoashi.
for in/on/with little human to come (in): come strength: soldiers Syria and LORD to give: give in/on/with hand: power their strength: soldiers to/for abundance much for to leave: forsake [obj] LORD God father their and with Joash to make: do judgment
25 Waaramu walipoondoka, walimwacha Yoashi akiwa mgonjwa sana. Maafisa wake wakafanya hila dhidi yake kwa sababu alikuwa amemuua mwana wa Kuhani Yehoyada, nao wakamuulia kitandani mwake. Hivyo akafa na wakamzika katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
and in/on/with to go: went they from him for to leave: forsake [obj] him (in/on/with suffering *Q(k)*) many to conspire upon him servant/slave his in/on/with blood son: child Jehoiada [the] priest and to kill him upon bed his and to die and to bury him in/on/with city David and not to bury him in/on/with grave [the] king
26 Wale waliofanya hila mbaya dhidi yake walikuwa Zabadi, mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni, Yehozabadi, mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabu.
and these [the] to conspire upon him Zabad son: child Shimeath [the] Ammon and Jehozabad son: child Shimrith [the] Moabite
27 Kwa habari za wanawe, unabii mwingi kumhusu na kumbukumbu za kutengenezwa upya kwa Hekalu la Mungu, zimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme. Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
and son: child his (to multiply *Q(K)*) [the] oracle upon him and to found house: temple [the] God look! they to write upon story scroll: book [the] king and to reign Amaziah son: child his underneath: instead him

< 2 Nyakati 24 >