< 2 Nyakati 23 >
1 Katika mwaka wa saba, Yehoyada akaonyesha nguvu zake. Alifanya agano na wakuu wa vikosi vya mamia: yaani Azaria mwana wa Yerohamu, Ishmaeli mwana wa Yehohanani, Azaria mwana wa Obedi, Maaseya mwana wa Adaya, na Elishafati mwana wa Zikri.
W roku siódmym Jehojada umocnił się i zawarł przymierze z setnikami: Azariaszem, synem Jerochama, Izmaelem, synem Jochanana, Azariaszem, synem Obeda, Maasejaszem, synem Adajasza, i Elisafatem, synem Zikriego.
2 Wakazunguka katika Yuda yote na kukusanya Walawi na viongozi wa jamaa za Israeli kutoka miji yote. Walipofika Yerusalemu,
Obeszli oni ziemię Judy, zebrali Lewitów ze wszystkich miast Judy oraz naczelników rodów Izraela i przybyli do Jerozolimy.
3 kusanyiko lote likafanya agano na mfalme katika Hekalu la Mungu. Yehoyada akawaambia, “Mwana wa mfalme atatawala, kama Bwana alivyoahidi kuhusu wazao wa Daudi.
Całe to zgromadzenie zawarło z królem przymierze w domu Bożym. I powiedział im: Oto syn króla będzie królował, tak jak PAN zapowiedział o synach Dawida.
4 Basi hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Theluthi yenu makuhani na Walawi ambao mnaingia zamu siku ya Sabato mtalinda milangoni,
Oto co macie uczynić: Trzecia część z was – kapłanów i Lewitów, którzy przychodzicie w szabat – [będzie] odźwiernymi przy bramach.
5 theluthi yenu mtalinda jumba la kifalme, na theluthi nyingine mtalinda Lango la Msingi. Walinzi wengine wote mwe ndani ya nyua za Hekalu la Bwana.
Trzecia część [będzie] w domu królewskim i trzecia część będzie w bramie fundamentu. Cały zaś lud [zostanie] w dziedzińcach domu PANA.
6 Hakuna mtu yeyote ataingia katika Hekalu la Bwana isipokuwa makuhani na Walawi walioko kwenye zamu. Wao wanaweza kuingia kwa sababu ni watakatifu, lakini watu wengine wote itawapasa kulinda kile walichoamriwa na Bwana.
Niech [nikt] nie wchodzi do domu PANA prócz kapłanów i usługujących Lewitów. Oni mogą wchodzić, gdyż są poświęceni. A cały lud niech trzyma straż PANA.
7 Walawi watajipanga kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha zake mkononi. Mtu mwingine yeyote aingiaye Hekaluni lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”
Lewici otoczą króla ze wszystkich stron, każdy z bronią w ręku. Ktokolwiek wejdzie do domu, poniesie śmierć. Bądźcie przy królu, gdy będzie wchodził i gdy będzie wychodził.
8 Walawi na watu wote wa Yuda wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, kwa sababu kuhani Yehoyada hakuruhusu kikosi chochote kiondoke.
I uczynili Lewici oraz cały lud Judy według wszystkiego, co rozkazał kapłan Jehojada. Każdy wziął swoich ludzi, którzy przychodzili w szabat, i tych, którzy odchodzili w szabat, bo kapłan Jehojada nie zwolnił [tych] zmian.
9 Kisha akawapa wakuu wa vikosi vya mamia mikuki na ngao kubwa na ndogo zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu.
I kapłan Jehojada rozdał setnikom włócznie, tarcze i puklerze, które [należały do] króla Dawida, a które [znajdowały się] w domu Bożym.
10 Akawapanga walinzi wote kumzunguka mfalme, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.
Ustawił też cały lud, a każdy miał broń w ręku, od prawej strony domu aż do lewej strony domu, [przy] ołtarzu i domu, dokoła króla.
11 Yehoyada na wanawe wakamtoa Yoashi mwana wa mfalme nje na kumvika taji. Wakampa nakala ya agano na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”
Wtedy wyprowadzili syna króla, włożyli mu koronę, [wręczyli mu] Świadectwo i ustanowili go królem. Jehojada i jego synowie namaścili go i wołali: Niech żyje król!
12 Athalia aliposikia kelele za watu wakikimbia na kumsifu mfalme, akawaendea watu katika Hekalu la Bwana.
Kiedy Atalia usłyszała krzyk zbiegającego się ludu, który chwalił króla, przyszła do ludu do domu PANA.
13 Athalia akaangalia, tazama alikuwepo mfalme akiwa amesimama karibu na nguzo yake kwenye ingilio. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa kando ya mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wanashangilia na kupiga tarumbeta na waimbaji wakiwa na vyombo vya uimbaji, walikuwa wakiongoza nyimbo za sifa. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kupiga kelele, akisema, “Uhaini! Uhaini!”
A gdy spojrzała, oto król stał przy kolumnie u wejścia, a wokół króla książęta i trąby. Cały lud tej ziemi radował się i dął w trąby, także śpiewacy z instrumentami muzycznymi oraz ci, którzy kierowali śpiewem. Wtedy Atalia rozdarła swoje szaty, mówiąc: Zdrada! Zdrada!
14 Kuhani Yehoyada akawatuma majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, na kuwaambia: “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Msimuulie ndani ya Hekalu la Bwana.”
Wówczas kapłan Jehojada rozkazał wystąpić setnikom dowodzącym wojskiem i powiedział do nich: Wyprowadźcie ją poza szeregi, a ktokolwiek pójdzie za nią, niech będzie zabity mieczem. Kapłan bowiem powiedział: Nie zabijajcie jej w domu PANA.
15 Kwa hiyo wakamkamata alipofika kwenye ingilio la Lango la Farasi katika viwanja vya jumba la mfalme wakamuulia hapo.
Pochwycili ją więc, a gdy przyszła do wejścia Bramy Końskiej przy domu królewskim, tam ją zabili.
16 Kisha Yehoyada akafanya agano kwamba yeye na watu wote na mfalme watakuwa watu wa Bwana.
Wtedy Jehojada zawarł przymierze między nim a całym ludem i królem, aby byli ludem PANA.
17 Kisha watu wote wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu pamoja na sanamu na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu.
Potem cały lud wszedł do domu Baala i zburzył go. Pokruszyli jego ołtarze i posągi, a Mattana, kapłana Baala, zabili przed ołtarzami.
18 Kisha Yehoyada akaweka uangalizi wa Hekalu la Bwana mikononi mwa makuhani, waliokuwa Walawi, ambao Mfalme Daudi alikuwa amewagawa ili wahudumu hekaluni kwa ajili ya kutoa sadaka za kuteketezwa za Bwana kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, kwa kushangilia na kuimba kama Daudi alivyokuwa ameagiza.
I Jehojada ustanowił przełożonych nad domem PANA pod władzą kapłanów i Lewitów, których Dawid podzielił w domu PANA, aby z radością i pieśniami składali PANU całopalenia, jak jest napisane w Prawie Mojżesza, według rozporządzenia Dawida.
19 Pia akawaweka mabawabu kwenye malango ya Hekalu la Bwana ili kwamba kwa vyovyote asije akaingia mtu yeyote aliye najisi.
Postawił też odźwiernych przy bramach domu PANA, aby nie wchodził nikt, kto byłby w jakikolwiek sposób nieczysty.
20 Akawachukua majemadari wa mamia, watu waheshimiwa, viongozi wa watu pamoja na watu wote wa nchi na kumteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana. Wakaingia kwenye jumba la mfalme kupitia Lango la Juu na kumkalisha mfalme kwenye kiti cha enzi,
Potem wziął setników, dostojników i przełożonych ludu oraz cały lud ziemi i wyprowadzili króla z domu PANA. Przeszli przez bramę wyższą do domu królewskiego i posadzili króla na tronie królestwa.
21 nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga.
I radował się cały lud ziemi. A miasto zaznało pokoju, gdy Atalię zabito mieczem.