< 2 Nyakati 23 >

1 Katika mwaka wa saba, Yehoyada akaonyesha nguvu zake. Alifanya agano na wakuu wa vikosi vya mamia: yaani Azaria mwana wa Yerohamu, Ishmaeli mwana wa Yehohanani, Azaria mwana wa Obedi, Maaseya mwana wa Adaya, na Elishafati mwana wa Zikri.
Dans la huitième année, Joad se fortifia, il prit avec lui dans le temple du Seigneur les centeniers Azarias, fils de Joram; Ismaël, fils de Johanan; Azarias, fils d'Obed; Maaseas, fils d'Adia, et Elisaphan, fils de Zacharie.
2 Wakazunguka katika Yuda yote na kukusanya Walawi na viongozi wa jamaa za Israeli kutoka miji yote. Walipofika Yerusalemu,
Ceux-ci parcoururent Juda, rassemblèrent les lévites de toutes les villes de Juda et les chefs de familles d'Israël, et rentrèrent à Jérusalem.
3 kusanyiko lote likafanya agano na mfalme katika Hekalu la Mungu. Yehoyada akawaambia, “Mwana wa mfalme atatawala, kama Bwana alivyoahidi kuhusu wazao wa Daudi.
Et dans le temple du Seigneur toute l'Église de Juda fit alliance avec le roi, et Joad leur montra le fils du roi, et il leur dit: Voilà le fils du roi: qu'il règne, selon la parole du Seigneur concernant la maison de David.
4 Basi hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Theluthi yenu makuhani na Walawi ambao mnaingia zamu siku ya Sabato mtalinda milangoni,
Écoutez donc ce que vous avez à faire: Que le tiers des prêtres et des lévites commence son service de semaine et garde les portes d'entrée,
5 theluthi yenu mtalinda jumba la kifalme, na theluthi nyingine mtalinda Lango la Msingi. Walinzi wengine wote mwe ndani ya nyua za Hekalu la Bwana.
Que l'on place un autre tiers au palais du roi, le dernier tiers à la porte du milieu, et tout le peuple dans les parvis du temple.
6 Hakuna mtu yeyote ataingia katika Hekalu la Bwana isipokuwa makuhani na Walawi walioko kwenye zamu. Wao wanaweza kuingia kwa sababu ni watakatifu, lakini watu wengine wote itawapasa kulinda kile walichoamriwa na Bwana.
Que nul ne pénètre dans le temple hormis les prêtres, les lévites et ceux qui les servent. Ceux-là entreront parce qu'ils sont saints, et tout le peuple fera la garde sainte autour du temple du Seigneur.
7 Walawi watajipanga kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha zake mkononi. Mtu mwingine yeyote aingiaye Hekaluni lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”
Et les lévites entoureront la personne du roi, les armes à la main; ils mettront à mort quiconque s'introduira dans le temple, et ils ne quitteront point le roi, soit qu'il entre, soit qu'il sorte.
8 Walawi na watu wote wa Yuda wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, kwa sababu kuhani Yehoyada hakuruhusu kikosi chochote kiondoke.
Les lévites et tout Juda se conformèrent aux ordres de Joad, et ceux qui sortaient de semaine restèrent avec ceux qui entraient en semaine, parce que le grand prêtre ne congédia point ceux dont le service finissait.
9 Kisha akawapa wakuu wa vikosi vya mamia mikuki na ngao kubwa na ndogo zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu.
Et Joad leur délivra les glaives, les boucliers et les armures du roi David, qui étaient dans le temple de Dieu.
10 Akawapanga walinzi wote kumzunguka mfalme, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.
Et il rangea le peuple, chacun sous ses armes, autour du roi, à l'aile droite du temple, et à l'aile gauche.
11 Yehoyada na wanawe wakamtoa Yoashi mwana wa mfalme nje na kumvika taji. Wakampa nakala ya agano na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”
Alors, il amena le fils du roi; il lui donna la couronne et les témoignages; puis, Joad le prêtre et ses fils le proclamèrent roi, et ils le sacrèrent, et le peuple cria: Vive le roi!
12 Athalia aliposikia kelele za watu wakikimbia na kumsifu mfalme, akawaendea watu katika Hekalu la Bwana.
Et Athalie entendit la rumeur du peuple courant, applaudissant, louant le roi, et elle entra auprès du roi dans le temple du Seigneur.
13 Athalia akaangalia, tazama alikuwepo mfalme akiwa amesimama karibu na nguzo yake kwenye ingilio. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa kando ya mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wanashangilia na kupiga tarumbeta na waimbaji wakiwa na vyombo vya uimbaji, walikuwa wakiongoza nyimbo za sifa. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kupiga kelele, akisema, “Uhaini! Uhaini!”
Et elle regarda, et voilà que le roi était sur son siège; et il y avait aux portes les princes, les trompettes, et, autour du roi, des princes et tout le peuple de la terre plein de joie; et les trompettes sonnaient, et les chantres au son des instruments chantaient des cantiques et des louanges; et Athalie déchira sa robe, et elle s'écria: Vous complotez et complotez.
14 Kuhani Yehoyada akawatuma majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, na kuwaambia: “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Msimuulie ndani ya Hekalu la Bwana.”
Et Joad s'avança pour donner ses ordres aux centeniers et aux chefs de l'armée, et il leur dit: Jetez-la hors du temple, suivez-la, qu'elle périsse par le glaive; et le prêtre ajouta: Qu'elle ne meure pas dans le temple du Seigneur.
15 Kwa hiyo wakamkamata alipofika kwenye ingilio la Lango la Farasi katika viwanja vya jumba la mfalme wakamuulia hapo.
Et ils la laissèrent libre de ses mouvements, et elle franchit la porte qui mène aux chevaux de la maison du roi, et là, ils la tuèrent.
16 Kisha Yehoyada akafanya agano kwamba yeye na watu wote na mfalme watakuwa watu wa Bwana.
Et Joad fit alliance avec le roi et avec le peuple, pour que Juda fût le peuple de Dieu.
17 Kisha watu wote wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu pamoja na sanamu na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu.
Et tout le peuple de la terre entra dans le temple de Baal, et ils renversèrent son autel, et ils brisèrent ses idoles, et ils tuèrent devant l'autel Mathan, prêtre de Baal.
18 Kisha Yehoyada akaweka uangalizi wa Hekalu la Bwana mikononi mwa makuhani, waliokuwa Walawi, ambao Mfalme Daudi alikuwa amewagawa ili wahudumu hekaluni kwa ajili ya kutoa sadaka za kuteketezwa za Bwana kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, kwa kushangilia na kuimba kama Daudi alivyokuwa ameagiza.
Et Joad remit aux prêtres et aux lévites le service du temple de Dieu, rétablit l'ordre des temps où ils devaient être employés, comme l'avait prescrit David, tant pour la garde du temple que pour les offrandes d'holocaustes, selon qu'il est écrit en la loi de Moïse, en y ajoutant les réjouissances et les chants institués par David.
19 Pia akawaweka mabawabu kwenye malango ya Hekalu la Bwana ili kwamba kwa vyovyote asije akaingia mtu yeyote aliye najisi.
Et les portiers veillèrent aux portes du temple, pour que nul homme impur n'y pût entrer sous aucun prétexte.
20 Akawachukua majemadari wa mamia, watu waheshimiwa, viongozi wa watu pamoja na watu wote wa nchi na kumteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana. Wakaingia kwenye jumba la mfalme kupitia Lango la Juu na kumkalisha mfalme kwenye kiti cha enzi,
Et il prit les chefs de famille, les vaillants, les chefs du peuple et tout le peuple de la terre, et ils firent monter le roi dans le temple du Seigneur, d'où il alla par la porte intérieure au palais du roi; là, ils assirent le roi sur le trône du royaume.
21 nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga.
Et tout le peuple de la terre fut en joie; la ville resta calme: Athalie avait été mise à mort.

< 2 Nyakati 23 >