< 2 Nyakati 22 >
1 Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
Поставиша же царем обитающии во Иерусалиме Охозию сына его меншаго вместо его: всех бо старших избиша нашедшии на них разбойницы Арави и Алимазоняне, и воцарися Охозиа сын Иорамов царь Иудин:
2 Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.
двадесяти дву лет сый Охозиа царствовати нача, и едино лето царствова во Иерусалиме. И имя матери его Гофолиа дщи Амвриина.
3 Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu.
И сей ходил есть по пути дому Ахаавля, мати бо его бе советница, да грешит:
4 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake.
и сотвори лукавое пред Господем якоже дом Ахаавов, сии бо быша ему советницы по смерти отца его, в погубление ему,
5 Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
и в советех их хождаше: и пойде со Иорамом сыном Ахаава царя Израилева на брань противу Азаила царя Сирска в Рамоф Галаадский. И поразиша стрелцы Иорама.
6 Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.
И возвратися Иорам изцелитися во Иезраель от ран, имиже раниша его Сиряне в Рамофе, внегда братися ему со Азаилем царем Сирским. Охозиа же сын Иорамль царь Иудин сниде посетити Иорама сына Ахаавля во Иезраель, разболеся бо.
7 Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu.
И от Бога бысть превращение Охозии, да приидет ко Иораму: и внегда приити ему, изыде с ним Иорам противу Ииуа сына Намессиина, егоже помаза Господь на дом Ахаавль.
8 Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua.
И бысть егда отмсти Ииуй дому Ахаавлю, и обрете началники Иудины и братию Охозиину, служащих Охозии, и уби их: и уби Ииуй Иорама, и убежа Охозиа.
9 Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.
И рече Ииуй, еже взыскати Охозию: и яша его врачующася в Самарии и приведоша его ко Ииуеви, и уби его, и погребоша его: реша бо, яко сын Иосафатов есть, иже взыска Господа всем сердцем своим. И не бысть в дому Охозиине восприяти силу о царстве.
10 Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda.
И Гофолиа мати Охозиина виде, яко умре сын ея, и воста и погуби все семя царское в дому Иудине.
11 Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue.
И взя Иосавееф дщи царева Иоаса сына Охозиина, и украде его от среды сынов царевых, егда убиваху их, и даде его и кормилицу его в храмину постельнюю, и скры его Иосавееф дщерь царя Иорама, сестра Охозиина, жена Иодаа архиереа, и скры его от лица Гофолиина, и не уби его.
12 Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.
И бысть с ними в дому Божии сокрыт шесть лет, и царствова Гофолиа на земли.