< 2 Nyakati 22 >
1 Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
Et les habitants de Jérusalem établirent Roi en sa place Achazia, le plus jeune de ses fils, parce que les troupes, qui étaient venues avec les Arabes en forme de camp, avaient tué tous ceux qui étaient plus âgés que lui; ainsi Achazia, fils de Joram Roi de Juda, régna.
2 Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.
Achazia était âgé de quarante-deux ans quand il commença à régner, et il régna un an à Jérusalem; sa mère avait nom Hathalie, et elle était fille de Homri.
3 Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu.
Et il suivit le train de la maison d'Achab; car sa mère était sa conseillère à mal faire.
4 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake.
Il fit donc ce qui déplaît à l'Eternel, comme ceux de la maison d'Achab; parce qu'ils furent ses conseillers après la mort de son père, pour son malheur.
5 Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
Même se gouvernant selon leurs conseils, il alla avec Joram fils d'Achab, Roi d'Israël, à la guerre à Ramoth de Galaad, contre Hazaël Roi de Syrie, là où les Syriens frappèrent Joram;
6 Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.
Qui s'en retourna pour se faire panser à Jizréhel, à cause des blessures qu'il avait reçues à Rama, quand il faisait la guerre contre Hazaël Roi de Syrie; et Hazaria fils de Joram, Roi de Juda, descendit à Jizréhel pour voir Joram le fils d'Achab, parce qu il était malade.
7 Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu.
Et ce fut là l'entière ruine d'Achazia, laquelle procédait de Dieu, d'être allé vers Joram; parce qu'après y être arrivé, il sortit avec Joram contre Jéhu fils de Nimsi, que l'Eternel avait oint pour retrancher la maison d'Achab.
8 Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua.
Car quand Jéhu prenait vengeance de la maison d'Achab, il trouva les principaux de Juda, et les fils des frères d'Achazia, qui servaient Achazia, et les tua.
9 Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.
Et ayant cherché Achazia qui s'était caché en Samarie, on le prit, et on l'amena vers Jéhu, et on le fit mourir, puis on l'ensevelit; car on dit: C'est le fils de Josaphat, qui a recherché l'Eternel de tout son cœur. Ainsi la maison d'Achazia ne put point se conserver le Royaume.
10 Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda.
Et Hathalie mère d'Achazia ayant vu que son fils était mort, s'éleva, et extermina tout le sang Royal de la maison de Juda.
11 Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue.
Mais Jéhosabhath fille du Roi [Joram] prit Joas fils d'Achazia, et le déroba d'entre les fils du Roi qu'on faisait mourir, et le mit avec sa nourrice dans la chambre aux lits. Ainsi Jéhosabhath fille du Roi Joram, et femme de Jéhojadah le Sacrificateur, le cacha de devant Hathalie, à cause qu'elle [était] sœur d'Achazia, de sorte qu'[Hathalie] ne le fit point mourir.
12 Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.
Et il fut caché avec eux dans la maison de Dieu l'espace de six ans; cependant Hathalie régnait sur le pays.