< 2 Nyakati 21 >

1 Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
Josaphat se coucha avec ses pères et fut enterré avec ses pères dans la ville de David; et Joram, son fils, régna à sa place.
2 Ndugu zake Yehoramu, wana wa Yehoshafati walikuwa: Azaria, Yehieli, Zekaria, Azaria, Mikaeli na Shefatia. Hawa wote walikuwa wana wa Yehoshafati mfalme wa Israeli
Il avait des frères, les fils de Josaphat: Azaria, Jehiel, Zacharie, Azaria, Michel et Schephatia. Tous ceux-là étaient les fils de Josaphat, roi d'Israël.
3 Baba yao alikuwa amewapa zawadi nyingi za fedha na dhahabu na vitu vya thamani, pamoja na miji yenye ngome huko Yuda, bali ufalme akampa Yehoramu kwa sababu alikuwa mwanawe mzaliwa wa kwanza.
Leur père leur fit de grands dons en argent, en or et en objets précieux, ainsi que des villes fortifiées en Juda; mais il donna la royauté à Joram, parce qu'il était le premier-né.
4 Baada ya Yehoramu kujiimarisha katika ufalme wa baba yake, akawaua kwa upanga ndugu zake wote pamoja na baadhi ya wakuu wa Israeli.
Or, lorsque Joram s'éleva sur le royaume de son père et qu'il se fortifia, il tua par l'épée tous ses frères, et aussi quelques-uns des princes d'Israël.
5 Yehoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane.
Joram avait trente-deux ans lorsqu'il devint roi, et il régna huit ans à Jérusalem.
6 Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana.
Il marcha dans la voie des rois d'Israël, comme la maison d'Achab, car il avait pour femme la fille d'Achab. Il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel.
7 Hata hivyo, kwa sababu ya Agano ambalo Bwana alikuwa amefanya na Daudi, Bwana hakuwa radhi kuangamiza nyumba ya Daudi. Mungu alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili yake na wazao wake milele.
Mais Yahvé ne voulut pas détruire la maison de David, à cause de l'alliance qu'il avait conclue avec lui, et parce qu'il avait promis de lui donner une lampe, à lui et à ses enfants, pour toujours.
8 Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe.
De son temps, Édom se révolta de dessous la main de Juda, et se fit un roi.
9 Basi Yehoramu akaenda huko pamoja na maafisa wake na magari yake ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu.
Et Joram s'y rendit avec ses chefs et tous ses chars avec lui. Il se leva de nuit et frappa les Edomites qui l'entouraient, ainsi que les chefs des chars.
10 Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo kwa sababu Yehoramu alikuwa amemwacha Bwana, Mungu wa baba zake.
Ainsi, jusqu'à ce jour, Édom s'est révolté sous la main de Juda. En même temps, Libna se révolta de sous sa main, parce qu'il avait abandonné Yahvé, le Dieu de ses pères.
11 Alikuwa pia ametengeneza mahali pa juu pa kuabudia miungu katika vilima vya Yuda na akawa amewasababisha watu wa Yerusalemu kufanya uzinzi na akawa amewapotosha watu wa Yuda.
Il fit aussi des hauts lieux dans les montagnes de Juda, il poussa les habitants de Jérusalem à se prostituer, et il égara Juda.
12 Yehoramu akapokea barua kutoka kwa nabii Eliya iliyosema: “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Daudi baba yako, asemalo: ‘Hukuenenda katika njia za Yehoshafati baba yako au za Asa mfalme wa Yuda.
Une lettre lui fut adressée par le prophète Élie, en ces termes: « Yahvé, le Dieu de David, ton père, dit: 'Parce que tu n'as pas suivi la voie de Josaphat, ton père, ni celle d'Asa, roi de Juda,
13 Lakini umeenenda katika njia za wafalme wa Israeli, nawe umewaongoza Yuda na watu wa Yerusalemu kuzini, kama vile nyumba ya Ahabu ilivyofanya. Pia umewaua ndugu zako mwenyewe, watu wa nyumbani mwa baba yako, watu waliokuwa bora kuliko wewe.
mais que tu as suivi la voie des rois d'Israël, tu as fait de Juda et des habitants de Jérusalem des prostitués comme la maison d'Achab, et tu as tué tes frères de la maison de ton père, qui étaient meilleurs que toi,
14 Hivyo basi Bwana yu karibu kuwapiga watu wako, wanao, wake zako na kila kitu kilicho chako, kwa pigo zito.
voici, Yahvé frappera ton peuple d'une grande plaie, avec tes enfants, tes femmes et tous tes biens;
15 Wewe mwenyewe utaugua sana kwa ugonjwa wa tumbo kwa muda mrefu, hadi ugonjwa utakaposababisha matumbo yako kutoka nje.’”
et vous serez atteints d'une grande maladie des entrailles, jusqu'à ce que vos entrailles tombent de jour en jour à cause de la maladie.'"
16 Bwana akaamsha chuki ya Wafilisti na ya Waarabu walioishi karibu na Wakushi dhidi ya Yehoramu.
Yahvé excita contre Joram l'esprit des Philistins et des Arabes qui sont à côté des Éthiopiens,
17 Wakaishambulia Yuda, wakaivamia na kuchukua mali zote zilizopatikana katika jumba la mfalme pamoja na wanawe na wake zake. Hakubakiziwa mwana yeyote isipokuwa Ahazia aliyekuwa mdogo wa wote.
et ils montèrent contre Juda, y firent irruption et emportèrent tous les biens qui se trouvaient dans la maison du roi, y compris ses fils et ses femmes, de sorte qu'il ne lui resta plus d'autre fils que Joachaz, le plus jeune de ses fils.
18 Baada ya mambo haya yote, Bwana akampiga Yehoramu kwa ugonjwa usioponyeka wa matumbo.
Après tout cela, Yahvé le frappa aux entrailles d'une maladie incurable.
19 Ikawa baada ya muda, mwisho wa mwaka wa pili, matumbo yake yakatoka nje kwa sababu ya ugonjwa, naye akafa katika maumivu makali sana. Watu wake hawakuwasha moto kwa heshima yake, kama walivyokuwa wamewafanyia baba zake.
Avec le temps, au bout de deux ans, ses entrailles tombèrent à cause de sa maladie, et il mourut de maladies graves. Son peuple ne fit pas pour lui de brûlure, comme celle de ses pères.
20 Yehoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipokuwa mfalme, naye akatawala huko Yerusalemu miaka minane. Akafa, bila kusikitikiwa na mtu yeyote, naye akazikwa katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
Il avait trente-deux ans lorsqu'il devint roi, et il régna huit ans à Jérusalem. Il s'en alla sans que personne ne le regrette. On l'enterra dans la ville de David, mais pas dans les tombeaux des rois.

< 2 Nyakati 21 >