< 2 Nyakati 21 >

1 Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
and to lie down: be dead Jehoshaphat with father his and to bury with father his in/on/with city David and to reign Jehoram son: child his underneath: instead him
2 Ndugu zake Yehoramu, wana wa Yehoshafati walikuwa: Azaria, Yehieli, Zekaria, Azaria, Mikaeli na Shefatia. Hawa wote walikuwa wana wa Yehoshafati mfalme wa Israeli
and to/for him brother: male-sibling son: child Jehoshaphat Azariah and Jehiel and Zechariah and Azariah and Michael and Shephatiah all these son: child Jehoshaphat king Israel
3 Baba yao alikuwa amewapa zawadi nyingi za fedha na dhahabu na vitu vya thamani, pamoja na miji yenye ngome huko Yuda, bali ufalme akampa Yehoramu kwa sababu alikuwa mwanawe mzaliwa wa kwanza.
and to give: give to/for them father their gift many to/for silver: money and to/for gold and to/for precious thing with city fortress in/on/with Judah and [obj] [the] kingdom to give: give to/for Jehoram for he/she/it [the] firstborn
4 Baada ya Yehoramu kujiimarisha katika ufalme wa baba yake, akawaua kwa upanga ndugu zake wote pamoja na baadhi ya wakuu wa Israeli.
and to arise: rise Jehoram upon kingdom father his and to strengthen: strengthen and to kill [obj] all brother: male-sibling his in/on/with sword and also from ruler Israel
5 Yehoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane.
son: aged thirty and two year Jehoram in/on/with to reign he and eight year to reign in/on/with Jerusalem
6 Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana.
and to go: walk in/on/with way: conduct king Israel like/as as which to make: do house: household Ahab for daughter Ahab to be to/for him woman: wife and to make: do [the] bad: evil in/on/with eye: seeing LORD
7 Hata hivyo, kwa sababu ya Agano ambalo Bwana alikuwa amefanya na Daudi, Bwana hakuwa radhi kuangamiza nyumba ya Daudi. Mungu alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili yake na wazao wake milele.
and not be willing LORD to/for to ruin [obj] house: household David because [the] covenant which to cut: make(covenant) to/for David and like/as as which to say to/for to give: give to/for him lamp and to/for son: descendant/people his all [the] day: always
8 Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe.
in/on/with day his to transgress Edom from underneath: owning hand: owner Judah and to reign upon them king
9 Basi Yehoramu akaenda huko pamoja na maafisa wake na magari yake ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu.
and to pass Jehoram with ruler his and all [the] chariot with him and to be to arise: rise night and to smite [obj] Edom [the] to turn: surround to(wards) him and [obj] ruler [the] chariot
10 Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo kwa sababu Yehoramu alikuwa amemwacha Bwana, Mungu wa baba zake.
and to transgress Edom from underneath: owning hand: owner Judah till [the] day: today [the] this then to transgress Libnah in/on/with time [the] he/she/it from underneath: owning hand: owner his for to leave: forsake [obj] LORD God father his
11 Alikuwa pia ametengeneza mahali pa juu pa kuabudia miungu katika vilima vya Yuda na akawa amewasababisha watu wa Yerusalemu kufanya uzinzi na akawa amewapotosha watu wa Yuda.
also he/she/it to make high place in/on/with mountain: hill country Judah and to fornicate [obj] to dwell Jerusalem and to banish [obj] Judah
12 Yehoramu akapokea barua kutoka kwa nabii Eliya iliyosema: “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Daudi baba yako, asemalo: ‘Hukuenenda katika njia za Yehoshafati baba yako au za Asa mfalme wa Yuda.
and to come (in): come to(wards) him writing from Elijah [the] prophet to/for to say thus to say LORD God David father your underneath: because of which not to go: walk in/on/with way: conduct Jehoshaphat father your and in/on/with way: conduct Asa king Judah
13 Lakini umeenenda katika njia za wafalme wa Israeli, nawe umewaongoza Yuda na watu wa Yerusalemu kuzini, kama vile nyumba ya Ahabu ilivyofanya. Pia umewaua ndugu zako mwenyewe, watu wa nyumbani mwa baba yako, watu waliokuwa bora kuliko wewe.
and to go: walk in/on/with way: conduct king Israel and to fornicate [obj] Judah and [obj] to dwell Jerusalem like/as to fornicate house: household Ahab and also [obj] brother: male-sibling your house: household father your [the] pleasant from you to kill
14 Hivyo basi Bwana yu karibu kuwapiga watu wako, wanao, wake zako na kila kitu kilicho chako, kwa pigo zito.
behold LORD to strike plague great: large in/on/with people your and in/on/with son: child your and in/on/with woman: wife your and in/on/with all property your
15 Wewe mwenyewe utaugua sana kwa ugonjwa wa tumbo kwa muda mrefu, hadi ugonjwa utakaposababisha matumbo yako kutoka nje.’”
and you(m. s.) in/on/with sickness many in/on/with sickness belly your till to come out: issue belly your from [the] sickness day upon day
16 Bwana akaamsha chuki ya Wafilisti na ya Waarabu walioishi karibu na Wakushi dhidi ya Yehoramu.
and to rouse LORD upon Jehoram [obj] spirit: temper [the] Philistine and [the] Arabian which upon hand: to Ethiopian
17 Wakaishambulia Yuda, wakaivamia na kuchukua mali zote zilizopatikana katika jumba la mfalme pamoja na wanawe na wake zake. Hakubakiziwa mwana yeyote isipokuwa Ahazia aliyekuwa mdogo wa wote.
and to ascend: rise in/on/with Judah and to break up/open her and to take captive [obj] all [the] property [the] to find to/for house: home [the] king and also son: child his and woman: wife his and not to remain to/for him son: child that if: except if: except Ahaziah small: young son: child his
18 Baada ya mambo haya yote, Bwana akampiga Yehoramu kwa ugonjwa usioponyeka wa matumbo.
and after all this to strike him LORD in/on/with belly his to/for sickness to/for nothing healing
19 Ikawa baada ya muda, mwisho wa mwaka wa pili, matumbo yake yakatoka nje kwa sababu ya ugonjwa, naye akafa katika maumivu makali sana. Watu wake hawakuwasha moto kwa heshima yake, kama walivyokuwa wamewafanyia baba zake.
and to be to/for day from day and like/as time to come out: extends [the] end to/for day: year two to come out: come belly his with sickness his and to die in/on/with disease bad: harmful and not to make to/for him people his fire like/as fire father his
20 Yehoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipokuwa mfalme, naye akatawala huko Yerusalemu miaka minane. Akafa, bila kusikitikiwa na mtu yeyote, naye akazikwa katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
son: aged thirty and two to be in/on/with to reign he and eight year to reign in/on/with Jerusalem and to go: went in/on/with not desire and to bury him in/on/with city David and not in/on/with grave [the] king

< 2 Nyakati 21 >