< 2 Nyakati 21 >
1 Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
And Jehoshaphat lies with his fathers, and is buried with his fathers in the City of David, and his son Jehoram reigns in his stead.
2 Ndugu zake Yehoramu, wana wa Yehoshafati walikuwa: Azaria, Yehieli, Zekaria, Azaria, Mikaeli na Shefatia. Hawa wote walikuwa wana wa Yehoshafati mfalme wa Israeli
And he has brothers, sons of Jehoshaphat: Azariah, and Jehiel, and Zechariah, and Azariah, and Michael, and Shephatiah; all these [are] sons of Jehoshaphat king of Israel,
3 Baba yao alikuwa amewapa zawadi nyingi za fedha na dhahabu na vitu vya thamani, pamoja na miji yenye ngome huko Yuda, bali ufalme akampa Yehoramu kwa sababu alikuwa mwanawe mzaliwa wa kwanza.
and their father gives to them many gifts of silver and of gold, and of precious things, with fortified cities in Judah, and he has given the kingdom to Jehoram, for he [is] the firstborn.
4 Baada ya Yehoramu kujiimarisha katika ufalme wa baba yake, akawaua kwa upanga ndugu zake wote pamoja na baadhi ya wakuu wa Israeli.
And Jehoram rises up over the kingdom of his father, and strengthens himself, and slays all his brothers with the sword, and also of the heads of Israel.
5 Yehoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane.
Jehoram [is] a son of thirty-two years in his reigning, and he has reigned eight years in Jerusalem,
6 Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana.
and he walks in the way of the kings of Israel, as the house of Ahab did, for a daughter of Ahab has been to him for a wife, and he does evil in the eyes of YHWH,
7 Hata hivyo, kwa sababu ya Agano ambalo Bwana alikuwa amefanya na Daudi, Bwana hakuwa radhi kuangamiza nyumba ya Daudi. Mungu alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili yake na wazao wake milele.
and YHWH has not been willing to destroy the house of David, for the sake of the covenant that He made with David, and as He had said to give a lamp to him and to his sons [for] all the days.
8 Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe.
In his days Edom has revolted from under the hand of Judah, and they cause a king to reign over them;
9 Basi Yehoramu akaenda huko pamoja na maafisa wake na magari yake ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu.
and Jehoram passes over with his heads, and all the chariots with him, and it comes to pass, he has risen by night and strikes the Edomites who are coming around against him, and the princes of the chariots,
10 Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo kwa sababu Yehoramu alikuwa amemwacha Bwana, Mungu wa baba zake.
and Edom revolts from under the hand of Judah to this day; then Libnah revolts at that time from under his hand, because he has forsaken YHWH, God of his fathers;
11 Alikuwa pia ametengeneza mahali pa juu pa kuabudia miungu katika vilima vya Yuda na akawa amewasababisha watu wa Yerusalemu kufanya uzinzi na akawa amewapotosha watu wa Yuda.
also, he has made high places on the mountains of Judah, and causes the inhabitants of Jerusalem to commit whoredom, and compels Judah.
12 Yehoramu akapokea barua kutoka kwa nabii Eliya iliyosema: “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Daudi baba yako, asemalo: ‘Hukuenenda katika njia za Yehoshafati baba yako au za Asa mfalme wa Yuda.
And a writing from Elijah the prophet comes to him, saying, “Thus said YHWH, God of your father David: Because that you have not walked in the ways of your father Jehoshaphat, and in the ways of Asa king of Judah,
13 Lakini umeenenda katika njia za wafalme wa Israeli, nawe umewaongoza Yuda na watu wa Yerusalemu kuzini, kama vile nyumba ya Ahabu ilivyofanya. Pia umewaua ndugu zako mwenyewe, watu wa nyumbani mwa baba yako, watu waliokuwa bora kuliko wewe.
and you walk in the way of the kings of Israel, and cause Judah and the inhabitants of Jerusalem to commit whoredom like the whoredoms of the house of Ahab, and also your brothers, the house of your father, who are better than yourself, you have slain;
14 Hivyo basi Bwana yu karibu kuwapiga watu wako, wanao, wake zako na kila kitu kilicho chako, kwa pigo zito.
behold, YHWH is striking [with] a great striking among your people, and among your sons, and among your wives, and among all your goods—
15 Wewe mwenyewe utaugua sana kwa ugonjwa wa tumbo kwa muda mrefu, hadi ugonjwa utakaposababisha matumbo yako kutoka nje.’”
and you, with many sicknesses, with disease of your bowels, until your bowels come out by the sickness, day by day.”
16 Bwana akaamsha chuki ya Wafilisti na ya Waarabu walioishi karibu na Wakushi dhidi ya Yehoramu.
And YHWH wakes up against Jehoram the spirit of the Philistines and of the Arabians, who [are] beside the Cushim,
17 Wakaishambulia Yuda, wakaivamia na kuchukua mali zote zilizopatikana katika jumba la mfalme pamoja na wanawe na wake zake. Hakubakiziwa mwana yeyote isipokuwa Ahazia aliyekuwa mdogo wa wote.
and they come up into Judah, and break into it, and take captive all the substance that is found at the house of the king, and also his sons, and his wives, and there has not been left to him a son except Jehoahaz the youngest of his sons.
18 Baada ya mambo haya yote, Bwana akampiga Yehoramu kwa ugonjwa usioponyeka wa matumbo.
And after all this YHWH has plagued him in his bowels by a disease for which there is no healing,
19 Ikawa baada ya muda, mwisho wa mwaka wa pili, matumbo yake yakatoka nje kwa sababu ya ugonjwa, naye akafa katika maumivu makali sana. Watu wake hawakuwasha moto kwa heshima yake, kama walivyokuwa wamewafanyia baba zake.
and it comes to pass, from days to days, and at the time of the going out of the end of two years, his bowels have gone out with his sickness, and he dies of severe diseases, and his people have not made for him a burning like the burning of his fathers.
20 Yehoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipokuwa mfalme, naye akatawala huko Yerusalemu miaka minane. Akafa, bila kusikitikiwa na mtu yeyote, naye akazikwa katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
He was a son of thirty-two [years] in his reigning, and he has reigned eight years in Jerusalem, and he goes without desire, and they bury him in the City of David, and not in the graves of the kings.