< 2 Nyakati 20 >

1 Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati.
Depois disso, as crianças de Moab, as crianças de Ammon, e com elas alguns dos amonitas, vieram contra Jehoshaphat para lutar.
2 Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako kutoka Edomu tokea ngʼambo ile nyingine ya Bahari. Tayari liko Hasason-Tamari” (yaani En-Gedi).
Depois vieram alguns que disseram a Jehoshaphat, dizendo: “Uma grande multidão está vindo contra vocês de além-mar da Síria”. Eis que eles estão em Hazazon Tamar” (ou seja, En Gedi).
3 Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafuta Bwana, na akatangaza kwa Yuda wote kufunga.
Jehoshaphat ficou alarmado, e se propôs a buscar a Yahweh. Ele proclamou um jejum em todo o Judá.
4 Watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kutafuta msaada kutoka kwa Bwana. Wakaja kutoka kila mji wa Yuda ili kumtafuta.
Judah se reuniu para buscar a ajuda de Iavé. Eles saíram de todas as cidades de Judá para buscar a Iavé.
5 Kisha Yehoshafati akasimama katika kusanyiko la Yuda na Yerusalemu katika Hekalu la Bwana, mbele ya ua mpya,
Jehoshaphat esteve na assembléia de Judá e Jerusalém, na casa de Iavé, diante do novo tribunal;
6 akasema: “Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe ndiwe uliye Mungu mbinguni? Si wewe ndiwe utawalaye juu ya falme zote za mataifa? Uweza na nguvu viko mkononi mwako, wala hakuna yeyote awezaye kushindana nawe.
e disse: “Iavé, o Deus de nossos pais, você não é Deus no céu? Não sois vós o governante de todos os reinos das nações? Poder e poder estão em suas mãos, para que ninguém seja capaz de resistir a você.
7 Je, si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu, rafiki yako, hata milele?
Você, nosso Deus, não expulsou os habitantes desta terra diante de seu povo Israel, e não a entregou para sempre à descendência de Abraão, seu amigo?
8 Wameishi ndani yake na humo wamekujengea mahali patakatifu kwa ajili ya Jina lako, wakisema:
Eles viveram nela, e nela construíram um santuário para seu nome, dizendo:
9 ‘Kama maafa yakitujia, ikiwa ni upanga, hukumu, tauni, au njaa, tutasimama mbele zako, mbele ya Hekalu hili ambalo limeitwa kwa Jina lako na kukulilia katika shida yetu, nawe utatusikia na kutuokoa.’
'Se o mal vier sobre nós - a espada, o julgamento, a peste ou a fome - estaremos diante desta casa, e diante de você (pois seu nome está nesta casa), e lhe choraremos em nossa aflição, e você ouvirá e salvará'.
10 “Lakini sasa hawa watu wa kutoka Amoni, Moabu na Mlima Seiri, ambao hukuwaruhusu Israeli wazivamie nchi zao wakati walitoka Misri, hivyo wakageukia mbali nao na hawakuwaangamiza,
Agora, eis que os filhos de Amom e Moabe e do Monte Seir, que não deixastes Israel invadir quando saíram da terra do Egito, mas se afastaram deles, e não os destruíram;
11 tazama jinsi wanavyotulipa kwa kuja kututupa nje ya milki uliyotupa sisi kuwa urithi.
eis como eles nos recompensam, para vir nos expulsar de vossa posse, que vós nos destes para herdar.
12 Ee Mungu wetu, je, wewe hutawahukumu? Kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kukabiliana na jeshi hili kubwa linalokuja kutushambulia. Sisi hatujui la kufanya, bali macho yetu yanakutazama wewe.”
Nosso Deus, você não os julgará? Pois não temos poder contra esta grande empresa que vem contra nós. Não sabemos o que fazer, mas nossos olhos estão em você”.
13 Watu wote wa Yuda pamoja na wake zao, watoto wao na wadogo wao wakasimama pale mbele za Bwana.
Todos os Judá estavam diante de Iavé, com seus pequenos, suas esposas e seus filhos.
14 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya mtu mmoja jina lake Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, Mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi mzao wa Asafu alipokuwa amesimama katika kusanyiko.
Então o Espírito de Javé veio sobre Jaaziel, filho de Zacarias, filho de Benaías, filho de Jeiel, filho de Matanias, o Levita, dos filhos de Asafe, no meio da assembléia;
15 Akasema: “Sikilizeni, enyi Yuda wote nanyi nyote mkaao Yerusalemu, nawe Mfalme Yehoshafati! Hili ndilo Bwana asemalo kwenu, ‘Msiogope wala msifadhaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Kwa maana vita hivi si vyenu, bali ni vya Mungu.
e ele disse: “Escutai, todo Judá, e vós, habitantes de Jerusalém, e vós, rei Jeosafá. Javé vos diz: “Não tenhais medo e não vos assusteis por causa desta grande multidão, pois a batalha não é vossa, mas de Deus”.
16 Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakwea kwa kupandia Genge la Sisi, nanyi mtawakuta mwisho wa bonde, kabla ya Jangwa la Yerueli.
Amanhã, desça contra eles. Eis que eles estão subindo pela ascensão de Ziz. Você os encontrará no final do vale, diante do deserto de Jeruel.
17 Hamtahitaji kupigana vita hivi. Kaeni kwenye nafasi zenu, simameni imara na mkaone wokovu Bwana atakaowapatia, enyi Yuda na Yerusalemu. Msiogope, wala msifadhaike. Kesho tokeni mwende mkawakabili, naye Bwana atakuwa pamoja nanyi.’”
Você não precisará travar esta batalha. Coloquem-se, parados, e vejam a salvação de Javé com vocês, ó Judá e Jerusalém. Não tenham medo, nem se desanimem. Saiam contra eles amanhã, pois Yahweh está com vocês”.
18 Yehoshafati akainamisha uso wake chini, nao watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakaanguka chini ili kuabudu mbele za Bwana.
Jehoshaphat abaixou a cabeça com o rosto no chão; e todo Judá e os habitantes de Jerusalém se prostraram diante de Javé, adorando a Javé.
19 Ndipo baadhi ya Walawi kutoka kwa Wakohathi na kwa wana wa Kora wakasimama na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.
Os levitas, dos filhos dos coatitas e dos filhos dos coraítas, levantaram-se para louvar a Iavé, o Deus de Israel, com uma voz extremamente alta.
20 Asubuhi na mapema wakaondoka kuelekea Jangwa la Tekoa. Walipoanza safari, Yehoshafati akasimama akasema, “Nisikilizeni, enyi Yuda, na watu wa Yerusalemu! Mwaminini Bwana Mungu wenu, hivyo mtathibitika, wasadikini manabii wake nanyi mtafanikiwa.
Eles se levantaram cedo pela manhã e saíram para o deserto de Tekoa. Ao saírem, Jeosafá levantou-se e disse: “Escutem-me, Judá e vocês, habitantes de Jerusalém! Acreditem em Yahweh, vosso Deus, assim vocês serão estabelecidos! Acreditem em seus profetas, assim vocês prosperarão”.
21 Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema: “Mshukuruni Bwana kwa kuwa upendo wake wadumu milele.”
Quando ele tinha tomado conselho com o povo, ele nomeou aqueles que deveriam cantar para Yahweh e fazer elogios em ordem sagrada ao saírem diante do exército, e dizer: “Dê graças a Yahweh, pois sua bondade amorosa perdura para sempre”.
22 Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.
Quando começaram a cantar e a louvar, Javé colocou emboscadas contra as crianças de Amon, Moab e Mount Seir, que tinham vindo contra Judá; e elas foram atingidas.
23 Watu wa Amoni na Moabu wakawainukia watu wa Mlima Seiri ili kuwaua na kuwaangamiza kabisa. Baada ya kumaliza kuwachinja watu wa Seiri, wakaangamizana wao kwa wao.
Pois as crianças de Ammon e Moab se levantaram contra os habitantes do Monte Seir para matá-los e destruí-los completamente. Quando terminaram de matar os habitantes de Seir, todos ajudaram a destruir uns aos outros.
24 Yuda walipofika katika mnara wa ulinzi wa jangwani, wakaliangalia lile jeshi kubwa, wakaona ni maiti tupu zimetapakaa ardhini, wala hakuna yeyote aliyenusurika.
Quando Judah chegou ao lugar com vista para o deserto, eles olharam para a multidão; e eis que eram cadáveres caídos na terra, e não houve quem escapasse.
25 Hivyo Yehoshafati na watu wake wakaenda kujitwalia nyara kutoka kwao, nao wakakuta humo wingi wa mifugo, mali, nguo na vitu vya thamani, ambavyo vilikuwa vingi zaidi ya vile walivyoweza kuchukua. Wakakusanya nyara kwa siku tatu kwa sababu zilikuwa nyingi mno.
Quando Jehoshaphat e seu povo vieram para levar seu saque, encontraram entre eles em abundância tanto riquezas como cadáveres com jóias preciosas, que eles despojaram para si mesmos, mais do que podiam levar. Eles saquearam durante três dias, foi muito.
26 Siku ya nne wakakusanyika katika Bonde la Beraka kwa maana huko ndiko walikomsifu Bwana. Ndiyo sababu linaitwa Bonde la Beraka mpaka leo.
No quarto dia, eles se reuniram no Vale de Beracah, pois lá eles abençoaram Yahweh. Portanto, o nome daquele lugar foi chamado “Vale Beracah” até hoje.
27 Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kwa kuwa Bwana alikuwa amewasababisha wafurahi juu ya adui zao.
Então voltaram, cada homem de Judá e Jerusalém, com Jeosafá à sua frente, para ir novamente a Jerusalém com alegria; pois Javé os tinha feito regozijar-se com seus inimigos.
28 Wakaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni mwa Bwana wakiwa na vinubi, zeze na tarumbeta.
Eles vieram a Jerusalém com instrumentos de cordas, harpas e trombetas para a casa de Iavé.
29 Hofu ya Mungu ikazipata falme zote za nchi waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa amepigana dhidi ya adui za Israeli.
O temor de Deus estava em todos os reinos dos países quando ouviram que Iavé lutou contra os inimigos de Israel.
30 Ufalme wa Yehoshafati ukawa na amani, kwa kuwa Mungu wake alikuwa amemstarehesha pande zote.
So o reino de Jehoshaphat estava calmo, pois seu Deus lhe deu descanso a todos os lados.
31 Hivyo Yehoshafati akatawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala katika Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
Então Jehoshaphat reinou sobre Judá. Ele tinha trinta e cinco anos de idade quando começou a reinar. Ele reinou vinte e cinco anos em Jerusalém. O nome de sua mãe era Azuba, filha de Shilhi.
32 Alienenda katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana.
Ele andou no caminho de Asa, seu pai, e não se desviou dele, fazendo o que estava certo aos olhos de Iavé.
33 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa, na watu wakawa bado hawajaelekeza mioyo yao kwa Mungu wa baba zao.
Entretanto, os lugares altos não foram tirados, e o povo ainda não havia colocado o coração no Deus de seus pais.
34 Matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Yehu mwana wa Hanani, ambazo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.
Agora o resto dos atos de Jeosafá, primeiro e último, eis que estão escritos na história de Jehu, o filho de Hanani, que está incluído no livro dos reis de Israel.
35 Hatimaye Yehoshafati mfalme wa Yuda akafanya urafiki na Ahazia mfalme wa Israeli ambaye alifanya maovu sana.
Depois disso, Jeosafá, rei de Judá, juntou-se a Acazias, rei de Israel. O mesmo fez de forma muito perversa.
36 Akaungana naye kutengeneza meli nyingi za kwenda Tarshishi, nazo zilitengenezwa huko Esion-Geberi.
Ele se uniu a ele para fazer navios para ir a Társis. Eles fizeram os navios em Ezion Geber.
37 Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akasema, “Kwa kuwa umeungana na Ahazia, Bwana ataangamiza vile mlivyotengeneza.” Zile meli zikavunjika na hazikuweza kungʼoa nanga ili kwenda Tarshishi.
Então Eliezer, filho de Dodavahu de Maresafá, profetizou contra Jeosafá, dizendo: “Porque te uniste a Acazias, Javé destruiu tuas obras”. Os navios foram naufragados, de modo que não puderam ir para Tarshish.

< 2 Nyakati 20 >