< 2 Nyakati 20 >

1 Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati.
Après cela, les fils de Moab et les fils d'Ammon, et avec eux des Ammonites, vinrent contre Josaphat pour lui faire la guerre.
2 Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako kutoka Edomu tokea ngʼambo ile nyingine ya Bahari. Tayari liko Hasason-Tamari” (yaani En-Gedi).
Des messagers vinrent en informer Josaphat en disant: " Une multitude nombreuse marche contre toi d'au delà de la mer Morte, de la Syrie, et voici qu'ils sont à Asason-Thamar, qui est Engaddi ".
3 Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafuta Bwana, na akatangaza kwa Yuda wote kufunga.
Effrayé, Josaphat se détermina à recourir à Yahweh, et il publia un jeûne pour tout Juda.
4 Watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kutafuta msaada kutoka kwa Bwana. Wakaja kutoka kila mji wa Yuda ili kumtafuta.
Juda s'assembla pour invoquer Yahweh; même l'on vint de toutes les villes de Juda pour invoquer Yahweh.
5 Kisha Yehoshafati akasimama katika kusanyiko la Yuda na Yerusalemu katika Hekalu la Bwana, mbele ya ua mpya,
Josaphat se tint au milieu de l'assemblée de Juda et de Jérusalem, dans la maison de Yahweh, devant le nouveau parvis,
6 akasema: “Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe ndiwe uliye Mungu mbinguni? Si wewe ndiwe utawalaye juu ya falme zote za mataifa? Uweza na nguvu viko mkononi mwako, wala hakuna yeyote awezaye kushindana nawe.
et il dit: " Yahweh, Dieu de nos pères, n'êtes-vous pas Dieu dans le ciel, et ne dominez-vous pas sur tous les royaumes des nations, et n'avez-vous pas en main la force et la puissance, sans que l'on puisse vous résister?
7 Je, si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu, rafiki yako, hata milele?
N'est-ce pas vous, ô notre Dieu, qui avez chassé les habitants de ce pays devant votre peuple d'Israël, et qui l'avez donné pour toujours à la postérité d'Abraham, votre ami.
8 Wameishi ndani yake na humo wamekujengea mahali patakatifu kwa ajili ya Jina lako, wakisema:
Ils y ont habité et ils y ont bâti pour vous un sanctuaire à votre nom, en disant:
9 ‘Kama maafa yakitujia, ikiwa ni upanga, hukumu, tauni, au njaa, tutasimama mbele zako, mbele ya Hekalu hili ambalo limeitwa kwa Jina lako na kukulilia katika shida yetu, nawe utatusikia na kutuokoa.’
S'il nous survient une calamité, l'épée du jugement, la peste ou la famine, nous nous tiendrons devant cette maison et devant toi, car ton nom est sur cette maison, nous crierons vers vous du milieu de notre angoisse, et vous écouterez et vous sauverez!
10 “Lakini sasa hawa watu wa kutoka Amoni, Moabu na Mlima Seiri, ambao hukuwaruhusu Israeli wazivamie nchi zao wakati walitoka Misri, hivyo wakageukia mbali nao na hawakuwaangamiza,
Maintenant, voici les fils d'Ammon et de Moab, et ceux de la montagne de Séïr, chez lesquels vous n'avez pas permis à Israël d'entrer quand il venait du pays d'Egypte, mais dont il s'est détourné sans les détruire;
11 tazama jinsi wanavyotulipa kwa kuja kututupa nje ya milki uliyotupa sisi kuwa urithi.
les voici qui nous récompensent en venant nous chasser de votre héritage, dont vous nous avez donné la possession!
12 Ee Mungu wetu, je, wewe hutawahukumu? Kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kukabiliana na jeshi hili kubwa linalokuja kutushambulia. Sisi hatujui la kufanya, bali macho yetu yanakutazama wewe.”
O notre Dieu, ne rendrez-vous pas un jugement contre eux? Car nous sommes sans force devant cette nombreuse multitude qui s'avance contre nous, et nous ne savons que faire, mais nos yeux sont tournés vers vous. "
13 Watu wote wa Yuda pamoja na wake zao, watoto wao na wadogo wao wakasimama pale mbele za Bwana.
Et tout Juda se tenait debout devant Yahweh, avec leurs petits enfants, leurs femmes et leurs fils.
14 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya mtu mmoja jina lake Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, Mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi mzao wa Asafu alipokuwa amesimama katika kusanyiko.
Alors, au milieu de l'assemblée, l'esprit de Yahweh fut sur Jahaziel, fils de Zacharias, fils de Banaïas, fils de Jéhiel, fils de Mathanias, lévite, d'entre les fils d'Asaph.
15 Akasema: “Sikilizeni, enyi Yuda wote nanyi nyote mkaao Yerusalemu, nawe Mfalme Yehoshafati! Hili ndilo Bwana asemalo kwenu, ‘Msiogope wala msifadhaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Kwa maana vita hivi si vyenu, bali ni vya Mungu.
Et Jahaziel dit: " Soyez attentifs, tout Juda et habitants de Jérusalem, et toi, roi Josaphat! Ainsi vous dit Yahweh: Ne craignez point et ne vous effrayez point devant cette nombreuse multitude, car ce n'est pas vous que concerne la guerre, mais Dieu.
16 Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakwea kwa kupandia Genge la Sisi, nanyi mtawakuta mwisho wa bonde, kabla ya Jangwa la Yerueli.
Demain descendez contre eux; voici qu'ils monteront par la colline de Sis, et vous les trouverez à l'extrémité de la vallée, en face du désert de Jéruel.
17 Hamtahitaji kupigana vita hivi. Kaeni kwenye nafasi zenu, simameni imara na mkaone wokovu Bwana atakaowapatia, enyi Yuda na Yerusalemu. Msiogope, wala msifadhaike. Kesho tokeni mwende mkawakabili, naye Bwana atakuwa pamoja nanyi.’”
Vous n'aurez pas à combattre en cette affaire: présentez-vous; tenez-vous là, et vous verrez la délivrance que Yahweh vous accordera, ô Juda et Jérusalem. Ne craignez point et ne vous effrayez point; demain, sortez à leur rencontre, et Yahweh sera avec vous. "
18 Yehoshafati akainamisha uso wake chini, nao watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakaanguka chini ili kuabudu mbele za Bwana.
Josaphat s'inclina le visage contre terre, et tout Juda et les habitants de Jérusalem tombèrent devant Yahweh pour adorer Yahweh.
19 Ndipo baadhi ya Walawi kutoka kwa Wakohathi na kwa wana wa Kora wakasimama na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.
Les lévites d'entre les fils de Caath et d'entre les fils de Coré, se levèrent pour célébrer Yahweh, le Dieu d'Israël, d'une voix forte et élevée.
20 Asubuhi na mapema wakaondoka kuelekea Jangwa la Tekoa. Walipoanza safari, Yehoshafati akasimama akasema, “Nisikilizeni, enyi Yuda, na watu wa Yerusalemu! Mwaminini Bwana Mungu wenu, hivyo mtathibitika, wasadikini manabii wake nanyi mtafanikiwa.
Le lendemain, s'étant levés de bon matin, ils se mirent en marche vers le désert de Thécué. Comme ils partaient, Josaphat se tint debout et dit: " Ecoutez-moi, Juda et habitants de Jérusalem! Confiez-vous dans Yahweh, votre Dieu, et vous serez inébranlables; confiez-vous en ses prophètes, et vous aurez du succès. "
21 Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema: “Mshukuruni Bwana kwa kuwa upendo wake wadumu milele.”
Ensuite, après avoir délibéré avec le peuple, il établit des chantres qui devaient, revêtus d'ornements sacrés et marchant devant l'armée, célébrer Yahweh, en disant: " Louez Yahweh, car sa miséricorde demeure à jamais! "
22 Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.
Au moment où l'on commençait les chants et les louanges, Yahweh dressa des pièges contre les fils d'Ammon et de Moab et contre ceux de la montagne de Séïr, qui étaient venus vers Juda, et ils furent battus.
23 Watu wa Amoni na Moabu wakawainukia watu wa Mlima Seiri ili kuwaua na kuwaangamiza kabisa. Baada ya kumaliza kuwachinja watu wa Seiri, wakaangamizana wao kwa wao.
Les fils d'Ammon et de Moab se tinrent contre les habitants de la montagne de Séïr pour les massacrer et les exterminer et, quand ils en eurent fini avec les habitants de Séïr, ils s'aidèrent les uns les autres à se détruire.
24 Yuda walipofika katika mnara wa ulinzi wa jangwani, wakaliangalia lile jeshi kubwa, wakaona ni maiti tupu zimetapakaa ardhini, wala hakuna yeyote aliyenusurika.
Lorsque Juda fut arrivé sur le poste de guet du désert, ils se tournèrent vers la multitude, et ne virent que des cadavres étendus par terre, sans que personne eût échappé.
25 Hivyo Yehoshafati na watu wake wakaenda kujitwalia nyara kutoka kwao, nao wakakuta humo wingi wa mifugo, mali, nguo na vitu vya thamani, ambavyo vilikuwa vingi zaidi ya vile walivyoweza kuchukua. Wakakusanya nyara kwa siku tatu kwa sababu zilikuwa nyingi mno.
Josaphat et son peuple allèrent piller leurs dépouilles, et ils y trouvèrent d'abondantes richesses, des cadavres et des objets précieux, et ils en enlevèrent pour eux jusqu'à ne pouvoir les porter; ils mirent trois jours à piller le butin, car il était considérable.
26 Siku ya nne wakakusanyika katika Bonde la Beraka kwa maana huko ndiko walikomsifu Bwana. Ndiyo sababu linaitwa Bonde la Beraka mpaka leo.
Le quatrième jour, ils s'assemblèrent dans la vallée de Beraca; car ils y bénirent Yahweh, et c'est pourquoi ils appelèrent ce lieu vallée de Beraca, qui est son nom jusqu'à ce jour.
27 Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kwa kuwa Bwana alikuwa amewasababisha wafurahi juu ya adui zao.
Tous les hommes de Juda et de Jérusalem, ayant Josaphat à leur tête, se mirent joyeusement en route pour retourner à Jérusalem, car Yahweh les avait remplis de joie en les délivrant de leurs ennemis.
28 Wakaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni mwa Bwana wakiwa na vinubi, zeze na tarumbeta.
Ils entrèrent à Jérusalem au son des cithares, des harpes et des trompettes, vers la maison de Yahweh.
29 Hofu ya Mungu ikazipata falme zote za nchi waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa amepigana dhidi ya adui za Israeli.
La terreur de Yahweh s'empara de tous les royaumes des pays, lorsqu'ils apprirent que Yahweh avait combattu contre les ennemis d'Israël.
30 Ufalme wa Yehoshafati ukawa na amani, kwa kuwa Mungu wake alikuwa amemstarehesha pande zote.
Et le royaume de Josaphat fut tranquille, et son Dieu lui donna du repos de tous côtés.
31 Hivyo Yehoshafati akatawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala katika Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
Josaphat devint roi de Juda. Il avait trente-cinq ans lorsqu'il devint roi, et il régna vingt-cinq ans à Jérusalem. Sa mère s'appelait Azuba, fille de Selahi.
32 Alienenda katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana.
Il marcha dans la voie d'Asa, son père, et ne s'en détourna point, faisant ce qui est droit aux yeux de Yahweh.
33 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa, na watu wakawa bado hawajaelekeza mioyo yao kwa Mungu wa baba zao.
Seulement les hauts lieux ne disparurent point, et le peuple n'avait pas encore fermement attaché son cœur au Dieu de ses pères.
34 Matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Yehu mwana wa Hanani, ambazo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.
Le reste des actes de Josaphat, les premiers et les derniers, voici qu'ils sont écrits dans les Paroles de Jéhu, fils de Hanani, lesquelles sont insérées dans le livre des rois d'Israël.
35 Hatimaye Yehoshafati mfalme wa Yuda akafanya urafiki na Ahazia mfalme wa Israeli ambaye alifanya maovu sana.
Après cela, Josaphat, roi de Juda, s'associa avec Ochosias, roi d'Israël, dont la conduite était criminelle.
36 Akaungana naye kutengeneza meli nyingi za kwenda Tarshishi, nazo zilitengenezwa huko Esion-Geberi.
Il s'associa avec lui pour construire des vaisseaux destinés à aller à Tharsis, et ils construisirent les vaisseaux à Asiongaber.
37 Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akasema, “Kwa kuwa umeungana na Ahazia, Bwana ataangamiza vile mlivyotengeneza.” Zile meli zikavunjika na hazikuweza kungʼoa nanga ili kwenda Tarshishi.
Alors Eliézer, fils de Dodau, de Marésa, prophétisa contre Josaphat, en disant: " Parce que tu t'es associé avec Ochozias, Yahweh a détruit ton œuvre. " Et les vaisseaux furent brisés, et ils ne purent aller à Tharsis.

< 2 Nyakati 20 >