< 2 Nyakati 20 >
1 Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati.
After this also came the children of Moab and the children of Ammon, and with them of the Ammonites against Iehoshaphat to battell.
2 Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako kutoka Edomu tokea ngʼambo ile nyingine ya Bahari. Tayari liko Hasason-Tamari” (yaani En-Gedi).
Then there came that tolde Iehoshaphat, saying, There commeth a great multitude against thee from beyonde the Sea, out of Aram: and beholde, they bee in Hazzon Tamar, which is En-gedi.
3 Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafuta Bwana, na akatangaza kwa Yuda wote kufunga.
And Iehoshaphat feared, and set him selfe to seeke the Lord, and proclaimed a fast throughout all Iudah.
4 Watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kutafuta msaada kutoka kwa Bwana. Wakaja kutoka kila mji wa Yuda ili kumtafuta.
And Iudah gathered them selues together to aske counsel of the Lord: they came euen out of all the cities of Iudah to inquire of the Lord,
5 Kisha Yehoshafati akasimama katika kusanyiko la Yuda na Yerusalemu katika Hekalu la Bwana, mbele ya ua mpya,
And Iehoshaphat stoode in the Congregation of Iudah and Ierusalem in the house of the Lord before the new court,
6 akasema: “Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe ndiwe uliye Mungu mbinguni? Si wewe ndiwe utawalaye juu ya falme zote za mataifa? Uweza na nguvu viko mkononi mwako, wala hakuna yeyote awezaye kushindana nawe.
And saide, O Lord God of our fathers, art not thou God in heauen? and reignest not thou on all the kingdomes of the heathen? and in thine hande is power and might, and none is able to withstand thee.
7 Je, si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu, rafiki yako, hata milele?
Diddest not thou our God cast out ye inhabitants of this lande before thy people Israel, and gauest it to the seede of Abraham thy friende for euer?
8 Wameishi ndani yake na humo wamekujengea mahali patakatifu kwa ajili ya Jina lako, wakisema:
And they dwelt therein, and haue built thee a Sanctuarie therein for thy Name, saying,
9 ‘Kama maafa yakitujia, ikiwa ni upanga, hukumu, tauni, au njaa, tutasimama mbele zako, mbele ya Hekalu hili ambalo limeitwa kwa Jina lako na kukulilia katika shida yetu, nawe utatusikia na kutuokoa.’
If euill come vpon vs, as the sworde of iudgement, or pestilence, or famine, we will stande before this house and in thy presence (for thy name is in this house) and will crie vnto thee in our tribulation, and thou wilt heare and helpe.
10 “Lakini sasa hawa watu wa kutoka Amoni, Moabu na Mlima Seiri, ambao hukuwaruhusu Israeli wazivamie nchi zao wakati walitoka Misri, hivyo wakageukia mbali nao na hawakuwaangamiza,
And now beholde, the children of Ammon and Moab, and mount Seir, by whome thou wouldest not let Israel goe, when they came out of the land of Egypt: but they turned aside from them, and destroyed them not:
11 tazama jinsi wanavyotulipa kwa kuja kututupa nje ya milki uliyotupa sisi kuwa urithi.
Behold, I say, they reward vs, in comming to cast vs out of thine inheritance, which thou hast caused vs to inherit.
12 Ee Mungu wetu, je, wewe hutawahukumu? Kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kukabiliana na jeshi hili kubwa linalokuja kutushambulia. Sisi hatujui la kufanya, bali macho yetu yanakutazama wewe.”
O our God, wilt thou not iudge them? for there is no strength in vs to stand before this great multitude that commeth against vs, neither doe wee knowe what to doe: but our eyes are toward thee.
13 Watu wote wa Yuda pamoja na wake zao, watoto wao na wadogo wao wakasimama pale mbele za Bwana.
And all Iudah stoode before the Lord with their yong ones, their wiues, and their children.
14 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya mtu mmoja jina lake Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, Mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi mzao wa Asafu alipokuwa amesimama katika kusanyiko.
And Iahaziel the sonne of Zechariah the sonne of Benaiah, the sonne of Ieiel, the sonne of Mattaniah, a Leuite of the sonnes of Asaph was there, vpon whome came the Spirite of ye Lord, in the middes of the Congregation.
15 Akasema: “Sikilizeni, enyi Yuda wote nanyi nyote mkaao Yerusalemu, nawe Mfalme Yehoshafati! Hili ndilo Bwana asemalo kwenu, ‘Msiogope wala msifadhaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Kwa maana vita hivi si vyenu, bali ni vya Mungu.
And he said, Hearken ye, all Iudah, and ye inhabitantes of Ierusalem, and thou, King Iehoshaphat: thus saith the Lord vnto you, Feare you not, neither be afraide for this great multitude: for the battel is not yours, but Gods.
16 Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakwea kwa kupandia Genge la Sisi, nanyi mtawakuta mwisho wa bonde, kabla ya Jangwa la Yerueli.
To morowe goe yee downe against them: beholde, they come vp by the cleft of Ziz, and ye shall finde them at the ende of the brooke before the wildernesse of Ieruel.
17 Hamtahitaji kupigana vita hivi. Kaeni kwenye nafasi zenu, simameni imara na mkaone wokovu Bwana atakaowapatia, enyi Yuda na Yerusalemu. Msiogope, wala msifadhaike. Kesho tokeni mwende mkawakabili, naye Bwana atakuwa pamoja nanyi.’”
Ye shall not neede to fight in this battell: stand still, moue not, and behold the saluation of the Lord towardes you: O Iudah, and Ierusalem, feare ye not, neither be afraid: to morow goe out against them, and the Lord wilbe with you.
18 Yehoshafati akainamisha uso wake chini, nao watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakaanguka chini ili kuabudu mbele za Bwana.
Then Iehoshaphat bowed downe with his face to the earth, and all Iudah and the inhabitants of Ierusalem fell downe before the Lord, worshipping the Lord.
19 Ndipo baadhi ya Walawi kutoka kwa Wakohathi na kwa wana wa Kora wakasimama na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.
And the Leuites of the children of the Kohathites and of the childre of the Corhites stood vp to prayse the Lord God of Israel with a loude voyce on hie.
20 Asubuhi na mapema wakaondoka kuelekea Jangwa la Tekoa. Walipoanza safari, Yehoshafati akasimama akasema, “Nisikilizeni, enyi Yuda, na watu wa Yerusalemu! Mwaminini Bwana Mungu wenu, hivyo mtathibitika, wasadikini manabii wake nanyi mtafanikiwa.
And when they arose early in the morning, they went forth to the wildernesse of Tekoa: and as they departed, Iehoshaphat stoode and sayde, Heare ye me, O Iudah, and ye inhabitants of Ierusalem: put your trust in the Lord your God, and ye shalbe assured: beleeue his Prophets, and ye shall prosper.
21 Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema: “Mshukuruni Bwana kwa kuwa upendo wake wadumu milele.”
And when he had consulted with the people, and appoynted singers vnto the Lord, and them that should prayse him that is in the beautifull Sanctuarie, in going forth before the men of armes, and saying, Prayse ye the Lord, for his mercy lasteth for euer,
22 Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.
And when they began to shoute, and to prayse, the Lord layed ambushments against the children of Ammon, Moab, and mount Seir, which were come against Iudah, and they slewe one another.
23 Watu wa Amoni na Moabu wakawainukia watu wa Mlima Seiri ili kuwaua na kuwaangamiza kabisa. Baada ya kumaliza kuwachinja watu wa Seiri, wakaangamizana wao kwa wao.
For the children of Ammon and Moab rose against the inhabitants of mount Seir, to slay and to destroy them and when they had made an end of the inhabitantes of Seir, euery one helped to destroy another.
24 Yuda walipofika katika mnara wa ulinzi wa jangwani, wakaliangalia lile jeshi kubwa, wakaona ni maiti tupu zimetapakaa ardhini, wala hakuna yeyote aliyenusurika.
And when Iudah came towarde Mizpah in the wildernes, they looked vnto the multitude: and behold, the carkeises were fallen to the earth, and none escaped.
25 Hivyo Yehoshafati na watu wake wakaenda kujitwalia nyara kutoka kwao, nao wakakuta humo wingi wa mifugo, mali, nguo na vitu vya thamani, ambavyo vilikuwa vingi zaidi ya vile walivyoweza kuchukua. Wakakusanya nyara kwa siku tatu kwa sababu zilikuwa nyingi mno.
And when Iehoshaphat and his people came to take away the spoyle of them, they founde among them in abundance both of substance and also of bodies laden with precious iewels, which they tooke for themselues, till they could cary no more: they were three dayes in gathering of the spoyle: for it was much.
26 Siku ya nne wakakusanyika katika Bonde la Beraka kwa maana huko ndiko walikomsifu Bwana. Ndiyo sababu linaitwa Bonde la Beraka mpaka leo.
And in the fourth day they assembled themselues in the valley of Berachah: for there they blessed the Lord: therefore they called the name of that place, The valley of Berachah vnto this day.
27 Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kwa kuwa Bwana alikuwa amewasababisha wafurahi juu ya adui zao.
Then euery man of Iudah and Ierusalem returned with Iehoshaphat their head, to goe againe to Ierusalem with ioy: for the Lord had made them to reioyce ouer their enemies.
28 Wakaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni mwa Bwana wakiwa na vinubi, zeze na tarumbeta.
And they came to Ierusalem with viols and with harpes, and with trumpets, euen vnto the house of the Lord.
29 Hofu ya Mungu ikazipata falme zote za nchi waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa amepigana dhidi ya adui za Israeli.
And the feare of God was vpon all the kingdomes of the earth, whe they had heard that the Lord had fought against ye enemies of Israel.
30 Ufalme wa Yehoshafati ukawa na amani, kwa kuwa Mungu wake alikuwa amemstarehesha pande zote.
So the kingdom of Iehoshaphat was quiet, and his God gaue him rest on euery side.
31 Hivyo Yehoshafati akatawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala katika Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
And Iehoshaphat reigned ouer Iudah, and was fiue and thirtie yeere olde, when he began to reigne: and reigned fiue and twentie yeere in Ierusalem, and his mothers name was Azubah the daughter of Shilhi.
32 Alienenda katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana.
And he walked in the way of Asa his father, and departed not therefrom, doing that which was right in the sight of the Lord.
33 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa, na watu wakawa bado hawajaelekeza mioyo yao kwa Mungu wa baba zao.
Howbeit the hie places were not taken away: for the people had not yet prepared their hearts vnto the God of their fathers.
34 Matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Yehu mwana wa Hanani, ambazo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.
Concerning the rest of the actes of Iehoshaphat first and last, beholde, they are written in the booke of Iehu the sonne of Hanani, which is mentioned in the booke of the kings of Israel.
35 Hatimaye Yehoshafati mfalme wa Yuda akafanya urafiki na Ahazia mfalme wa Israeli ambaye alifanya maovu sana.
Yet after this did Iehoshaphat King of Iudah ioyne himselfe with Ahaziah King of Israel, who was giuen to do euill.
36 Akaungana naye kutengeneza meli nyingi za kwenda Tarshishi, nazo zilitengenezwa huko Esion-Geberi.
And he ioyned with him, to make ships to go to Tarshish: and they made the shippes in Ezion Gaber.
37 Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akasema, “Kwa kuwa umeungana na Ahazia, Bwana ataangamiza vile mlivyotengeneza.” Zile meli zikavunjika na hazikuweza kungʼoa nanga ili kwenda Tarshishi.
Then Eliezer ye sonne of Dodauah of Mareshah prophecied against Iehoshaphat, saying, Because thou hast ioyned thy selfe with Ahaziah, the Lord hath broken thy workes. and the shippes were broken, that they were not able to go to Tarshish.