< 2 Nyakati 19 >

1 Mfalme Yehoshafati wa Yuda akarudi salama kwenye jumba lake la kifalme huko Yerusalemu.
Yahuda Kralı Yehoşafat ise Yeruşalim'deki sarayına güvenlik içinde döndü.
2 Yehu mwonaji, mwana wa Hanani, akapanda kwenda kuonana naye akamwambia Mfalme Yehoshafati, “Je, utawasaidia waovu na kuwapenda wale wanaomchukia Bwana? Kwa sababu ya jambo hili, ghadhabu ya Bwana iko juu yako.
Hanani oğlu Bilici Yehu, Kral Yehoşafat'ı karşılamaya giderek ona şöyle dedi: “Kötülere yardım edip RAB'den nefret edenleri mi sevmen gerekir? Bunun için RAB'bin öfkesi senin üstünde olacak.
3 Hata hivyo, kuna mema yaliyoonekana kwako, kwa kuwa umeondoa katika nchi nguzo za Ashera na umeukaza moyo wako katika kumtafuta Mungu.”
Ancak, bazı iyi yönlerin de var. Ülkeden Aşera putlarını kaldırıp attın ve yürekten Tanrı'ya yönelmeye karar verdin.”
4 Yehoshafati aliishi huko Yerusalemu, naye akatoka akaenda tena miongoni mwa watu, kuanzia Beer-Sheba hadi nchi ya vilima ya Efraimu na kuwageuza wakamrudia Bwana, Mungu wa baba zao.
Yehoşafat Yeruşalim'de yaşadı. Beer-Şeva'dan Efrayim dağlık bölgesine kadar yine halkın arasında dolaşarak onları atalarının Tanrısı RAB'be döndürdü.
5 Akawaweka waamuzi katika nchi, kwenye miji yote ya Yuda yenye maboma.
Ülkeye, Yahuda'nın bütün surlu kentlerine yargıçlar atadı.
6 Akawaambia, “Angalieni kwa makini yale mtendayo, kwa kuwa hamkuhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Bwana ambaye yu pamoja nanyi kila mtoapo hukumu.
Onlara, “Yaptıklarınıza dikkat edin” dedi, “Çünkü insan adına değil, yargı verirken sizinle olan RAB adına yargılayacaksınız.
7 Basi sasa hofu ya Bwana na iwe juu yenu. Hukumuni kwa uangalifu, kwa kuwa kwa Bwana Mungu wetu hakuna jambo lisilo la haki, upendeleo, wala rushwa.”
Onun için RAB'den korkun, dikkatle yargılayın. Çünkü Tanrımız RAB kimsenin haksızlık yapmasına, kimseyi kayırmasına, rüşvet almasına göz yummaz.”
8 Pia huko Yerusalemu, Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi, makuhani na viongozi wa jamaa za Waisraeli ili kutoa hukumu kwa ajili ya Bwana na kuamua magomvi. Nao waliishi huko Yerusalemu.
RAB'bin yargılarını uygulamak, davalara bakmak için Yehoşafat Yeruşalim'e de bazı Levililer'i, kâhinleri, İsrail boy başlarını atadı. Bunlar Yeruşalim'de yaşadılar.
9 Akawapa maagizo haya: “Ni lazima mtumike kwa uaminifu na kwa moyo wote katika kicho cha Bwana.
Yehoşafat onlara şu buyrukları verdi: “Görevinizi RAB korkusuyla, bağlılıkla, bütün yüreğinizle yapmalısınız.
10 Katika kila shauri lifikalo mbele yenu kutoka kwa ndugu zenu wale waishio katika miji, ikiwa ni la umwagaji wa damu au mambo mengine yahusuyo sheria, amri, hukumu au maagizo, inawapasa ninyi kuwaonya kwamba wasiingie katika hatia dhidi ya Bwana, la sivyo ghadhabu yake itakuja juu yenu na ndugu zenu. Tendeni hivyo, nanyi hamtatenda dhambi.
Kentlerde yaşayan kardeşlerinizden gelen her davada –kan davası, Kutsal Yasa, buyruklar, kurallar ya da ilkelerle ilgili her konuda– onları RAB'be karşı suç işlememeleri için uyarın; öyle ki RAB size de kardeşlerinize de öfkelenmesin. Böyle yaparsanız suç işlememiş olursunuz.
11 “Amaria kuhani mkuu atakuwa juu yenu katika jambo lolote linalomhusu Bwana naye Zebadia mwana wa Ishmaeli, kiongozi wa kabila la Yuda, atakuwa juu yenu kwa jambo lolote linalomhusu mfalme, nao Walawi watatumika kama maafisa mbele yenu. Tendeni kwa ujasiri, naye Bwana atakuwa pamoja na wale watendao vyema.”
“RAB'be ilişkin her konuda Başkâhin Amarya, krala ilişkin her konuda ise Yahuda oymağının önderi İsmail oğlu Zevadya size başkanlık edecek. Levililer de görevli olarak size yardımcı olacaklar. Yürekli olun, bu buyrukları uygulayın. RAB doğru kişiyle olsun!”

< 2 Nyakati 19 >