< 2 Nyakati 19 >

1 Mfalme Yehoshafati wa Yuda akarudi salama kwenye jumba lake la kifalme huko Yerusalemu.
Judov kralj Józafat pa se je v miru vrnil k svoji hiši v Jeruzalem.
2 Yehu mwonaji, mwana wa Hanani, akapanda kwenda kuonana naye akamwambia Mfalme Yehoshafati, “Je, utawasaidia waovu na kuwapenda wale wanaomchukia Bwana? Kwa sababu ya jambo hili, ghadhabu ya Bwana iko juu yako.
Hananíjev sin Jehú, videc, je odšel ven, da ga sreča in kralju Józafatu rekel: »Ali naj bi pomagal brezbožnikom in ljubil tiste, ki sovražijo Gospoda? Zato je izpred Gospoda na tebi bes.
3 Hata hivyo, kuna mema yaliyoonekana kwako, kwa kuwa umeondoa katika nchi nguzo za Ashera na umeukaza moyo wako katika kumtafuta Mungu.”
Kljub temu so v tebi najdene dobre stvari v tem, da si iz dežele odvzel ašere in si svoje srce pripravil, da išče Boga.
4 Yehoshafati aliishi huko Yerusalemu, naye akatoka akaenda tena miongoni mwa watu, kuanzia Beer-Sheba hadi nchi ya vilima ya Efraimu na kuwageuza wakamrudia Bwana, Mungu wa baba zao.
Józafat je prebival v Jeruzalemu. In odšel je ponovno ven skozi ljudstvo od Beeršébe do gore Efrájim in jih vodil nazaj h Gospodu, Bogu njihovih očetov.
5 Akawaweka waamuzi katika nchi, kwenye miji yote ya Yuda yenye maboma.
Postavil je sodnike vsepovsod po deželi, po vseh utrjenih Judovih mestih, mestu za mestom
6 Akawaambia, “Angalieni kwa makini yale mtendayo, kwa kuwa hamkuhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Bwana ambaye yu pamoja nanyi kila mtoapo hukumu.
in sodnikom rekel: »Pazite, kaj počnete, kajti ne sodite za človeka, temveč za Gospoda, ki je z vami v sodbi.
7 Basi sasa hofu ya Bwana na iwe juu yenu. Hukumuni kwa uangalifu, kwa kuwa kwa Bwana Mungu wetu hakuna jambo lisilo la haki, upendeleo, wala rushwa.”
Zatorej naj bo sedaj nad vami Gospodov strah. Pazite in to storite, kajti z Gospodom, svojim Bogom, ni krivičnosti, niti oziranja na osebe, niti sprejemanja darov.
8 Pia huko Yerusalemu, Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi, makuhani na viongozi wa jamaa za Waisraeli ili kutoa hukumu kwa ajili ya Bwana na kuamua magomvi. Nao waliishi huko Yerusalemu.
Poleg tega je v Jeruzalemu Józafat postavil od Lévijevcev in od duhovnikov in od vodij Izraelovih očetov za Gospodovo sodbo in za oporekanja, ko so se vrnili v Jeruzalem.
9 Akawapa maagizo haya: “Ni lazima mtumike kwa uaminifu na kwa moyo wote katika kicho cha Bwana.
Zadolžil jih je, rekoč: »To boste delali v Gospodovem strahu, zvesto in s popolnim srcem.
10 Katika kila shauri lifikalo mbele yenu kutoka kwa ndugu zenu wale waishio katika miji, ikiwa ni la umwagaji wa damu au mambo mengine yahusuyo sheria, amri, hukumu au maagizo, inawapasa ninyi kuwaonya kwamba wasiingie katika hatia dhidi ya Bwana, la sivyo ghadhabu yake itakuja juu yenu na ndugu zenu. Tendeni hivyo, nanyi hamtatenda dhambi.
Kakršnakoli zadeva bo prišla k vam od vaših bratov, ki prebivajo v svojih mestih, med krvjo in krvjo, med postavo in zapovedjo, zakoni in sodbami, jih boste torej opozorili, da ne prestopajo zoper Gospoda in tako [ne] pride bes nad vas in nad vaše brate. To delajte in se ne boste pregrešili.
11 “Amaria kuhani mkuu atakuwa juu yenu katika jambo lolote linalomhusu Bwana naye Zebadia mwana wa Ishmaeli, kiongozi wa kabila la Yuda, atakuwa juu yenu kwa jambo lolote linalomhusu mfalme, nao Walawi watatumika kama maafisa mbele yenu. Tendeni kwa ujasiri, naye Bwana atakuwa pamoja na wale watendao vyema.”
Glejte, véliki duhovnik Amarjá je nad vami v vseh Gospodovih zadevah in Jišmaélov sin Zebadjá, vladar Judove hiše, za vse kraljeve zadeve. Prav tako bodo Lévijevci častniki pred vami. Postopajte pogumno in Gospod bo z dobrim.«

< 2 Nyakati 19 >