< 2 Nyakati 19 >
1 Mfalme Yehoshafati wa Yuda akarudi salama kwenye jumba lake la kifalme huko Yerusalemu.
Aa le nimpoly an-kanintsiñe mb’ añ’anjomba’e e Ierosalaime añe t’Iehosafate.
2 Yehu mwonaji, mwana wa Hanani, akapanda kwenda kuonana naye akamwambia Mfalme Yehoshafati, “Je, utawasaidia waovu na kuwapenda wale wanaomchukia Bwana? Kwa sababu ya jambo hili, ghadhabu ya Bwana iko juu yako.
Le niavotse nifanalaka ama’e t’Iehò ana’ i Kananý mpioniñe, nanao ty hoe am’ Iehosafate mpanjaka: Ho nolora’o hao ty lo-tsereke; ho nikokoa’o hao ty malaiñe Iehovà? Hametsaha’ Iehovà haviñerañe!
3 Hata hivyo, kuna mema yaliyoonekana kwako, kwa kuwa umeondoa katika nchi nguzo za Ashera na umeukaza moyo wako katika kumtafuta Mungu.”
F’ie ahaoniñan-tsoa, kanao naria’o an-tane atoy o hazomangao vaho nitambozora’o arofo hitsoek’ an’ Andrianañahare.
4 Yehoshafati aliishi huko Yerusalemu, naye akatoka akaenda tena miongoni mwa watu, kuanzia Beer-Sheba hadi nchi ya vilima ya Efraimu na kuwageuza wakamrudia Bwana, Mungu wa baba zao.
Aa le nimoneñe e Ierosalaime ao t’Iehosafate naho niavotse indraike mb’am’ ondaty mifotots’ e Beersevà pak’ ambohibohi’ i Efraimeo vaho nampoli’e am’ Iehovà Andrianañaharen-droae’ iareo.
5 Akawaweka waamuzi katika nchi, kwenye miji yote ya Yuda yenye maboma.
Le nampijadoña’e mpizaka an-tane ao; amo rova-fatratse e Iehoda iabio kirova-drova,
6 Akawaambia, “Angalieni kwa makini yale mtendayo, kwa kuwa hamkuhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Bwana ambaye yu pamoja nanyi kila mtoapo hukumu.
le hoe re amo mpizakao: Ereñereo o anoe’ areoo; toe tsy ama’ ondaty ty fizaka’areo, fa ama’ Iehovà, Ie ty mañimba anahareo mizakao.
7 Basi sasa hofu ya Bwana na iwe juu yenu. Hukumuni kwa uangalifu, kwa kuwa kwa Bwana Mungu wetu hakuna jambo lisilo la haki, upendeleo, wala rushwa.”
Ee arè, te ho ama’areo ty fañeveñañe ama’ Iehovà; mitaoa vaho mitoloña; fa tsy aman-tahiñe t’Iehovà Andrianañaharen-tika ndra firihiañe ndra fandrambesam-bokàñe.
8 Pia huko Yerusalemu, Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi, makuhani na viongozi wa jamaa za Waisraeli ili kutoa hukumu kwa ajili ya Bwana na kuamua magomvi. Nao waliishi huko Yerusalemu.
Mbore nampijadoñe nte-Levy naho mpisoroñe vaho talèn’ anjomban-droae’ Israele e Ierosalaime ao t’Iehosafate ho ami’ty fizakà’ Iehovà naho ty hizakàñe o mpilie-drokoñe amo mpimoneñe e Ierosalameo.
9 Akawapa maagizo haya: “Ni lazima mtumike kwa uaminifu na kwa moyo wote katika kicho cha Bwana.
Le nafanto’e am’ iereo ty hoe: Hanoe’ areo am-pañeveñañe ama’ Iehovà o raha zao, am-pigahiñañe naho an-kaampon’arofo.
10 Katika kila shauri lifikalo mbele yenu kutoka kwa ndugu zenu wale waishio katika miji, ikiwa ni la umwagaji wa damu au mambo mengine yahusuyo sheria, amri, hukumu au maagizo, inawapasa ninyi kuwaonya kwamba wasiingie katika hatia dhidi ya Bwana, la sivyo ghadhabu yake itakuja juu yenu na ndugu zenu. Tendeni hivyo, nanyi hamtatenda dhambi.
Aa ndra mbia’ mbia te tendrek’ ama’ areo boak’ aman-drolongo’ areo mpimoneñe an-drova’ iareo ao, añivo’ ty lio naho ty lio, añivo’ t’i Hake naho ty faly, ty fañè naho ty fepètse, le ho hatahatae’ areo, ehe, tsy hanan-tahiñe am’ Iehovà, hampifetsahan-kaviñerañe ama’ areo naho aman-drolongo’ areo; ano izay, tsy hampanan-kakeo anahareo.
11 “Amaria kuhani mkuu atakuwa juu yenu katika jambo lolote linalomhusu Bwana naye Zebadia mwana wa Ishmaeli, kiongozi wa kabila la Yuda, atakuwa juu yenu kwa jambo lolote linalomhusu mfalme, nao Walawi watatumika kama maafisa mbele yenu. Tendeni kwa ujasiri, naye Bwana atakuwa pamoja na wale watendao vyema.”
Ingo, hifehe anahareo amy ze hene raha’ Iehovà t’i Amarià mpisorom-bey; naho amo raham-panjaka iabio i Zebadià, ana’ Ismaele, talèn’ anjomba Iehodà; vaho añatrefa’ areo o mpifeleke nte-Levio. Mahasibeha am-pitoloñañe le himbae’ Iehovà o vantañeo.