< 2 Nyakati 19 >
1 Mfalme Yehoshafati wa Yuda akarudi salama kwenye jumba lake la kifalme huko Yerusalemu.
Josaphat, roi de Juda, revint en paix dans sa maison à Jérusalem.
2 Yehu mwonaji, mwana wa Hanani, akapanda kwenda kuonana naye akamwambia Mfalme Yehoshafati, “Je, utawasaidia waovu na kuwapenda wale wanaomchukia Bwana? Kwa sababu ya jambo hili, ghadhabu ya Bwana iko juu yako.
Jéhu, fils de Hanani, le voyant, sortit au-devant de lui, et il dit au roi Josaphat: « Doit-on secourir le méchant, et aimes-tu ceux qui haïssent Yahweh? À cause de cela, est venue sur toi la colère, de par Yahweh.
3 Hata hivyo, kuna mema yaliyoonekana kwako, kwa kuwa umeondoa katika nchi nguzo za Ashera na umeukaza moyo wako katika kumtafuta Mungu.”
Pourtant, il s’est trouvé quelque bien en toi, car tu as fait disparaître du pays les aschérahs, et tu as appliqué ton cœur à chercher Dieu. »
4 Yehoshafati aliishi huko Yerusalemu, naye akatoka akaenda tena miongoni mwa watu, kuanzia Beer-Sheba hadi nchi ya vilima ya Efraimu na kuwageuza wakamrudia Bwana, Mungu wa baba zao.
Josaphat résida à Jérusalem; et de nouveau il visita le peuple depuis Bersabée jusqu’à la montagne d’Ephraïm, et il les ramena à Yahweh, le Dieu de leurs pères.
5 Akawaweka waamuzi katika nchi, kwenye miji yote ya Yuda yenye maboma.
Il établit des juges dans le pays, dans toutes les villes fortes de Juda, pour chaque ville.
6 Akawaambia, “Angalieni kwa makini yale mtendayo, kwa kuwa hamkuhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Bwana ambaye yu pamoja nanyi kila mtoapo hukumu.
Et il dit aux juges: « Prenez garde à ce que vous ferez, car ce n’est pas pour les hommes que vous rendrez la justice, mais c’est pour Yahweh; il sera avec vous quand vous rendrez la justice.
7 Basi sasa hofu ya Bwana na iwe juu yenu. Hukumuni kwa uangalifu, kwa kuwa kwa Bwana Mungu wetu hakuna jambo lisilo la haki, upendeleo, wala rushwa.”
Et moi maintenant, que la crainte de Yahweh soit sur vous; veillez sur vos actes, car il n’y a avec Yahweh, notre Dieu, ni iniquité, ni acception des personnes, ni acceptation des présents. »
8 Pia huko Yerusalemu, Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi, makuhani na viongozi wa jamaa za Waisraeli ili kutoa hukumu kwa ajili ya Bwana na kuamua magomvi. Nao waliishi huko Yerusalemu.
À Jérusalem aussi, quand ils revinrent dans cette ville, Josaphat établit, pour les jugements de Yahweh et pour les contestations, des lévites, des prêtres et des chefs de maisons d’Israël.
9 Akawapa maagizo haya: “Ni lazima mtumike kwa uaminifu na kwa moyo wote katika kicho cha Bwana.
Et il leur donna des ordres en ces termes: « Vous agirez ainsi en craignant Yahweh, dans la fidélité et l’intégrité du cœur.
10 Katika kila shauri lifikalo mbele yenu kutoka kwa ndugu zenu wale waishio katika miji, ikiwa ni la umwagaji wa damu au mambo mengine yahusuyo sheria, amri, hukumu au maagizo, inawapasa ninyi kuwaonya kwamba wasiingie katika hatia dhidi ya Bwana, la sivyo ghadhabu yake itakuja juu yenu na ndugu zenu. Tendeni hivyo, nanyi hamtatenda dhambi.
Dans toute cause qui viendra devant vous de la part de vos frères établis dans leurs villes, quand il s’agira de distinguer entre meurtre et meurtre, entre loi, commandement, précepte ou ordonnance, vous les éclairerez, afin qu’ils ne se rendent pas coupables envers Yahweh, et que sa colère ne vienne pas sur vous et sur vos frères. Vous agirez ainsi, et vous ne serez point coupables.
11 “Amaria kuhani mkuu atakuwa juu yenu katika jambo lolote linalomhusu Bwana naye Zebadia mwana wa Ishmaeli, kiongozi wa kabila la Yuda, atakuwa juu yenu kwa jambo lolote linalomhusu mfalme, nao Walawi watatumika kama maafisa mbele yenu. Tendeni kwa ujasiri, naye Bwana atakuwa pamoja na wale watendao vyema.”
Et voici que vous aurez à votre tête Amarias, le grand prêtre, pour toutes les affaires de Yahweh, et Zabadias, fils d’Ismaël, le prince de la maison de Juda, pour toutes les affaires du roi, et vous aurez devant vous les lévites comme officiers. Courage et à l’œuvre! et que Yahweh soit avec vous! »