< 2 Nyakati 18 >

1 Basi, Yehoshafati alikuwa na mali nyingi sana na heshima. Naye akafanya urafiki na Ahabu kwa mwanawe kumwoa binti wa Ahabu.
یهوشافاط ثروت و شهرت زیادی کسب کرد و با اَخاب، پادشاه اسرائیل وصلت نمود و دختر او را به عقد پسرش درآورد.
2 Baada ya miaka kadhaa akashuka kumtembelea Ahabu huko Samaria. Ahabu akachinja ngʼombe na kondoo wengi kwa ajili yake na watu aliokuwa amefuatana nao. Kisha Ahabu akamshawishi Yehoshafati kukwea pamoja naye ili kuishambulia Ramoth-Gileadi.
چند سال بعد، یهوشافاط پادشاه یهودا برای دیدن اَخاب پادشاه اسرائیل به سامره رفت و اَخاب برای او و همراهانش مهمانی بزرگی ترتیب داد و تعداد زیادی گاو و گوسفند سر برید. در آن مهمانی اَخاب از یهوشافاط پادشاه خواست در حمله به راموت جلعاد به او کمک کند. یهوشافاط گفت: «هر چه دارم مال توست، قوم من قوم توست. من و قومم در این جنگ همراه تو خواهیم بود.
3 Ahabu mfalme wa Israeli akamuuliza Yehoshafati mfalme wa Yuda, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako. Tutakuwa pamoja nawe vitani.”
4 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
ولی خواهش می‌کنم اول با خداوند مشورت کنی.»
5 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda kwa kuwa Mungu ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
پس اَخاب پادشاه، چهارصد نفر از انبیای خود را احضار کرد و از ایشان پرسید: «آیا برای تسخیر راموت جلعاد بروم یا نه؟» همهٔ آنها یکصدا گفتند: «برو، چون خدا به تو پیروزی خواهد بخشید.»
6 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
آنگاه یهوشافاط پرسید: «آیا غیر از اینها نبی دیگری در اینجا نیست تا نظر خداوند را به ما بگوید؟»
7 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
اَخاب جواب داد: «چرا، یک نفر به اسم میکایا پسر یمله هست، که توسط او می‌توان از خدا مسئلت کرد، اما من از او نفرت دارم، چون همیشه برای من چیزهای بد پیشگویی می‌کند.» یهوشافاط گفت: «اینطور سخن نگویید!»
8 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
پس اَخاب پادشاه، یکی از افراد دربار خود را صدا زد و به او گفت: «برو و میکایا را هر چه زودتر به اینجا بیاور.»
9 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
هر دو پادشاه در میدان خرمنگاه نزدیک دروازهٔ شهر سامره با لباسهای شاهانه بر تختهای سلطنتی خود نشسته بودند و تمام انبیا در حضور ایشان پیشگویی می‌کردند.
10 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
یکی از این انبیا به نام صدقیا، پسر کنعنه، که شاخهای آهنی برای خود درست کرده بود، گفت: «خداوند می‌فرماید که با این شاخها، سوری‌ها را تار و مار خواهی کرد!»
11 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho, wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
سایر انبیا نیز با او همصدا شده، گفتند: «به راموت جلعاد حمله کن، چون خداوند تو را پیروز خواهد کرد.»
12 Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
قاصدی که به دنبال میکایا رفته بود، به او گفت: «تمام انبیا پیشگویی می‌کنند که پادشاه پیروز خواهد شد، پس تو نیز چنین پیشگویی کن.»
13 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
ولی میکایا به او گفت: «به خداوند زنده قسم، هر چه خدای من بفرماید، همان را خواهم گفت.»
14 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa watatiwa mkononi mwako.”
وقتی میکایا به حضور پادشاه رسید، اَخاب از او پرسید: «ای میکایا، آیا به راموت جلعاد حمله کنم یا نه؟» میکایا جواب داد: «البته! چرا حمله نکنی! حتماً پیروز خواهی شد!»
15 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
پادشاه به او گفت: «چند مرتبه تو را قسم بدهم که هر چه خداوند می‌گوید، همان را به من بگویی؟»
16 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
آنگاه میکایا به او گفت: «تمام قوم اسرائیل را دیدم که مثل گوسفندان بی‌شبان، روی تپه‌ها سرگردانند. خداوند فرمود: اینها صاحب ندارند. به ایشان بگو به خانه‌های خود برگردند.»
17 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu bali mabaya tu?”
اَخاب به یهوشافاط گفت: «به تو نگفتم؟ من هرگز حرف خوب از زبان این مرد نشنیده‌ام!»
18 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama upande wa kulia na wa kushoto.
بعد میکایا گفت: «به این پیغام خداوند نیز گوش دهید! خداوند را دیدم که بر تخت خود نشسته بود و فرشتگان در طرف راست و چپ او ایستاده بودند.
19 Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu, mfalme wa Israeli, ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
آنگاه خداوند فرمود: چه کسی می‌تواند اَخاب را فریب دهد تا به راموت جلعاد حمله کند و همان جا کشته شود؟ هر یک از فرشتگان نظری داد.
20 Mwishoni, roho akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’ “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’
سرانجام روحی جلو آمد و به خداوند گفت: من این کار را می‌کنم! خداوند پرسید: چگونه؟
21 “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
روح گفت: من سخنان دروغ در دهان انبیا می‌گذارم و اَخاب را گمراه می‌کنم. خداوند فرمود: تو می‌توانی او را فریب دهی، پس برو و چنین کن!»
22 “Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
آنگاه میکایای نبی گفت: «خداوند روح گمراه کننده در دهان انبیای تو گذاشته تا به تو دروغ بگویند. ولی حقیقت امر این است که خداوند می‌خواهد تو را گرفتار مصیبت سازد.»
23 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
با شنیدن این جمله، صدقیا پسر کنعنه، جلو رفت و یک سیلی محکم به صورت میکایا زد و گفت: «روح خداوند کی مرا ترک کرده و به سوی تو آمده و با تو سخن گفته است؟»
24 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
میکایا به او گفت: «آن روز که در اتاقت مخفی شوی، جواب این سؤال را خواهی یافت!»
25 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
آنگاه اَخاب پادشاه دستور داد: «میکایا را بگیرید و پیش آمون، فرماندار شهر و به نزد یوآش، پسرم ببرید.
26 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
و از قول من به ایشان بگویید که میکایا را به زندان بیفکنند و جز آب و نان چیزی به او ندهند تا من پیروز برگردم.»
27 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
میکایا به او گفت: «اگر تو زنده برگشتی، معلوم می‌شود من هر چه به تو گفتم، از جانب خداوند نبوده است.» سپس رو به حاضران کرد و گفت: «همهٔ شما شاهد باشید که من به پادشاه چه گفتم!»
28 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
با وجود این هشدارها، اَخاب پادشاه اسرائیل و یهوشافاط پادشاه یهودا به راموت جلعاد لشکرکشی کردند.
29 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
اَخاب به یهوشافاط گفت: «تو لباس شاهانهٔ خود را بپوش، ولی من لباس دیگری می‌پوشم تا کسی مرا نشناسد.» پس اَخاب با لباس مبدل به میدان جنگ رفت.
30 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
پادشاه سوریه به سرداران ارابه‌هایش دستور داده بود که به دیگران زیاد توجه نکنند، بلکه فقط با خود اَخاب بجنگند.
31 Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati, wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele, naye Bwana akamsaidia. Mungu akawaondoa kwake,
به محض اینکه سرداران ارابه‌ها یهوشافاط را دیدند گفتند: «این پادشاه اسرائیل است.» پس رفتند تا با او بجنگند، اما یهوشافاط فریاد برآورد و خداوند به او کمک کرد و آنها را از او دور ساخت،
32 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli nao wakaacha kumfuatilia.
زیرا به محض اینکه سرداران ارابه‌ها متوجه شدند که او پادشاه اسرائیل نیست، از تعقیب وی دست برداشتند.
33 Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma, mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
اما تیر یکی از سربازان به طور تصادفی از میان شکاف زرهٔ اَخاب، به او اصابت کرد. اَخاب به ارابه‌ران خود گفت: «ارابه را برگردان و مرا از میدان جنگ بیرون ببر، چون سخت مجروح شده‌ام.»
34 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye mfalme wa Israeli akajitegemeza ndani ya gari lake kuwaelekea Waaramu hadi jioni. Basi jioni yake akafa.
جنگ به اوج شدت خود رسیده بود و اَخاب نیمه جان به کمک ارابه‌ران خود، رو به سوری‌ها در ارابهٔ خود ایستاده بود. سرانجام هنگام غروب جان سپرد.

< 2 Nyakati 18 >